Dogo anataka PCB kachaguliwa HGL

Justdr

Member
Joined
Jun 1, 2021
Posts
53
Reaction score
104
Mwenye anaweza kunisaidia please!

..kuna dogo amemaliza f4 na kuchaguliwa high school HGL
Unfortunately enough dogo hana interest kabisa na masomo ya arts ..yeye ni hama asome PCB au aende college kozi za afya(kozi za afya hapa barrier uchumi unabana hataweza).
Sasa naomba anayeweza kunisaidia akapata shule ya serikali PCB tuwasiliane ,
Phone 0629595248.
Dogo matokeo yake haya hapa
Yuko na II ya 19
CIVICS - 'C'
HIST - 'C'
GEO - 'C'
KISW - 'C'
ENGL - 'A'
PHY - 'D'
CHEM - 'C'
BIO - 'C'
B/MATH - 'D'

Hata ushauri pia,

Don't hesitate to contact me ili dogo hatimize ndoto zake
 
Nikiwa naenda form5 (private) nilikataliwa kabisa kusoma science. Nilichotaka ni sayansi no more no less. Nikaambiwa nisome HGL. Kweli nikaenda arts (lengo lilikua ni kuingia shule) ila nilipofika tu niliingia kwenye kipindi cha history mara moja tu!

Nikaenda kwa headmaster nikamwambia nataka kusoma Pure math, akashangaa! Arts to math? Akakataa!! Akasema wewe kasome HGE! Nikasema sawa!

Kesho yake nikaenda kwa academic master nikamwambia natala kusoma sayansi, akaniagalia usoni kwa sekunde kadhaa, then akasema sawa, akanibadilishia kombi!

Tokea hiyo siku mpaka namaliza nilikua mmoja ya wanafunzi wanaoongoza darasa.

Necta ya six nikapiga zangu 1 swaaafi kabisa.. nikaenda chuo..

Kwa sasa mimi ni injinia somewhere!!

Lesson: Angalia moyoni mwako, kama unaweza unachotaka basi simamia kitu unachoamini!!

NB: Kama serikalini akikosa nafasi mpeleni shule za private ila ahakikishe anajiamini na anauhakika wa kitu anachotaka kusoma!
 
Kuhusu PCB muulize Ndugai atakueleza ilichomfanyia.
Peleka ujinga wako huko. Ni commitment tu hakuna jambo gumu. Unataka kujifanya ndo weweeeeeeee. Dogo akasome Mchepuo wa ndoto zake na atafaulu
 
Hiyo english ndo imemfanya apelekwe huko'A',Tamisemi wana dawati la kushughulikia hayo malalamiko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…