Wakazi wa Mnada Mpya, Kata ya Nkuhungu – Dodoma hatuna maji wiki ya 3 sasa
Jamii Forums naomba mtusaidie kufikisha ujumbe huu kwa mamlaka zinazohusika kuhusu shida ya maji ya muda mrefu.
Sisi wakazi wa Mnada Mpya, Kata ya Nkuhungu, Mtaa wa Afisa Elimu, hatuna maji wiki ya tatu sasa na hakuna msaada kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Dodoma.
Kabla ya shida hii walituwekea utaratibu wa kuwa na zamu, maji yakawa yanatoka siku ya zamu yetu lakini hali ilivyo sasa, shida ni kubwa na hata yanapotoka yanakuwa na kasi ndogo.