Doctors Vs Engineers

Engineer anatakiwa awe mwepesi wa kufikiri, kufanya maamuzi makini sana.
Hufanya kazi kwa kufuata principles na akili ya ziada hutumika sana
engineer sehemu yoyote Ndo anaanza na watu wengine hufata
Mfano, waulize surveyor wanapo pita pori nene na kna wanyama wakali na bdae brudoza Ndo hufata.
Wahandisi chini ya migodi
Na baharini Na ujenzi wa mabawa kama akili sio nzuri utakufa na pressure tu
Doctor hufata principles tu haongezei ktu cha ziada.
rejea worldwide mega structure uone kazi ya uhandisi.
Viva engineer-viva engineer!
 
mbona sioni implication ya huu uzi?? ok fine, nikikubari udakitari ni mgumu then what next?? sijui tatizo ni umri ??
subiri nikuulize swali kama ulipita kidato cha nne au hata kama darasa la 4 B.
hivi mashuleni wanavyoweka debates mfano "elimu ni bora kuliko pesa" alafu wewe ukaja na mawazo yako ya then what next? sasa hapo tukuweke kwenye kundi gani la wanafunzi???
 
Hahaha...kweli...tatizo umri.
 
Mimi niko mechanical engineering first 1 . Wacha kaka nimepungua kilo 15 kwa ajili ya kusoma tu na hapa bado mitihani.
 
Nikiwafikiria hawa Newton, einstein, tesla, currie, faraday, kirchoff. Aisee engineering acha kabisa.
 
Swali very simple, huyo engineer anaweza kufanya yote hayo kama hayupo njema kiafya mfano ana matatizo ya ubongo?

Alafu kipi cha muhimu kwa uhai, Afya au hizo intervention za ki engineer?

Vyote vya muhimu., je hujui kuwa through hizo interventions Uhai na Afya can be monitored? Mgonjwa analazwa wodini, mgonjwa atahitaji vipimo kujua kama kuna internal bleeding or any ugonjwa ndani (MR-I, CT-Scan, X-ray), Mgonjwa atahitaji kuchomwa sindano and lots of things. Unafikiri hivyo vyote vimeletwa na BS?? We do respects u docs, but making yourself special over others sio kabisa. Just tunategemeana with engineering being ahead of you a bit.
 
Kwel Mkuuu Nakuunga Mkono As An Engineer i have to be smart i and my fellows Engineers.
 
Mkuu Unatumia Bia gani nikupe Ofa, Umemjibu Poa sana Huyo
 
Dokta hawezi fanya chochote bila mhandisi yani Labda mganga wa Jadi ndio anae eza asimtegemee engineer ila hawa Modern doctors huhitaji Engineering field 99℅ kufanikisha shughuli zao kuna kitu kinaitwa Automation dokta yuko marekani na anakufanyia operation ww mgongwa upo Tanzania through Engineering field
 
Nahisi ile harufuuu ya debate za form I
"Doctor is better than Teacher"

"Money is better than Education"

btw
Everything not invented by God is invented by engineers
 
Engineering ni shidah wadau sema inategemea na fakati unayo soma coz uwez ukasema industrial eng het nayo taffu
 
Mwili wa binadamu ni mashine tata Mara nyingi zaidi kuliko mashine yoyote ile unayoijua, hata miaka mitano ya medical school + internship haitoshi kukufanya ujue sana kuhusu hii mashine. Ndio maana kuna vitengo vingi sana ambavyo vinafanya kazi kwa pamoja kuhakikisha hii mashine ndogo lakini very complex inakua poa kwa sababu mtu mmoja hawezi kuijua kinagaubaga. Daktari huyu wa kawaida, MD, anajua tu summary ya hii mashine na kushughulikia matatizo ambayo ni size yake ila kila system inakua na mtaalamu wake mfano gynecology, neuroscience, dentistry, midwife, n. k. Huyo ni Daktari ambaye kazi yake ni diagnosis tu, bado hatujaingia kwenye madawa ambayo tunamkuta mfamasia ambaye naye ana kazi kubwa, maabara tunamkuta lab technologist. Afya ya mtu inahusisha watu wengi ambao wengine sijawataja hapo juu. Pia duniani ili maisha yaende tunahitaji watu wa kazi tofauti na hatuwezi sema eti kazi fulani ni zaidi ya nyingine hivyo engineering pia ni muhimu sana katika maendeleo ya binadamu kiujumla ndio maana siku izi kuna kozi ambayo inajumuisha mambo ya afya + engineering inaitwa biomedical equipment engineering. Katika maisha kila shughuli ina umuhimu hata akina alikiba na diamond(mziki) ni muhimu sana kwa sababu kupitia wao tunaburudika na kuondoa stress za maisha
 
hata smartphone au pc uliyopostia jf imetengenezwa na engineer...

daktari atatibu vipi bila kipimo kilichotengenezwa na engineer..

atajuaje kama unaumwa malaria au ukimwi, au cancer bila kutumia kipimo ambacho ni engineer amekileta...

tv, ndege, vipimo na mashine zote duniani ni engineer huyo.. hadi maghorofa unayoyaona ni engineer kahusika
 
Hiyo engineering yenyewe basi hata mngejaribu kuiclass..huwezi sema engineer ni toughest thing wakati we ni just civil engineer,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…