Dkt. Kimei ashiriki zoezi la kukabidhi madarasa 85 kwa shule za sekondari Wilayani Moshi

Moshi News

New Member
Oct 1, 2021
1
2
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh. Abbas Juma Kayanda, ameongoza viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi kupokea Vyumba vya Madarasa 85 vilivyokamilika kwa asilimia 100%.

Katika Hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari ya Himo mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Madarasa yote 85 kupitia fedha za UVIKO 19.

Mhe. Dkt Kimei (Mb) amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kupatikana kwa Fedha zote ambazo ni zaidi ya Bilioni 1.7. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Vunjo tunasema Ahsante Mhe. Rais kwa Fedha hizi Kwasasa tuna uhakika wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wataenda Shule bila shida. Pia, amewapongeza watendaji kwa ushirikiano wao kufanikisha Kukamilika kwa Mradi huo kwa wakati na ubora Mkubwa.
IMG_20211229_174120_005.jpg
IMG-20211229-WA0103.jpg
IMG-20211229-WA0096.jpg
IMG-20211229-WA0100.jpg
IMG-20211229-WA0099.jpg
IMG-20211229-WA0101.jpg
IMG_20211229_174120_118.jpg
IMG_20211229_174120_204.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh. Abbas Juma Kayanda, ameongoza viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi kupokea Vyumba vya Madarasa 85 vilivyokamilika kwa asilimia 100%.

Katika Hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari ya Himo mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Madarasa yote 85 kupitia fedha za UVIKO 19.

Mhe. Dkt Kimei (Mb) amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kupatikana kwa Fedha zote ambazo ni zaidi ya Bilioni 1.7. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Vunjo tunasema Ahsante Mhe. Rais kwa Fedha hizi Kwasasa tuna uhakika wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wataenda Shule bila shida. Pia, amewapongeza watendaji kwa ushirikiano wao kufanikisha Kukamilika kwa Mradi huo kwa wakati na ubora Mkubwa.View attachment 2061958View attachment 2061959View attachment 2061960View attachment 2061962View attachment 2061961View attachment 2061963View attachment 2061964View attachment 2061965
Naona darasa Moja, tupiamo tupicha picha na tujina twa shule zilizo nufaika. Kwa faida ya wadanganyika na wanufaika wanafunzi Kwa Nia ya kujenga hamasa, kwani watanzania wanaeleweka Kwa janjajanja zaidi wanasiihasa.
 
"Mhe. Dkt Kimei (Mb) amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kupatikana kwa Fedha zote ambazo ni zaidi ya Bilioni 1.7. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Vunjo tunasema Ahsante Mhe. Rais kwa Fedha hizi Kwasasa tuna uhakika wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wataenda Shule bila shida. Pia, amewapongeza watendaji kwa ushirikiano wao kufanikisha Kukamilika kwa Mradi huo kwa wakati na ubora Mkubwa."

Pongezi ni muhimu lakini shukrani zimetajwa ni kana kwamba pesa ni za muheshimiwa


Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Ila mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni! Hili la madarasa Mama amecheza sana! Jambo ambalo kila mwaka nilikuwa najiuliza ni kwamba inakuwaje shule zikifunguliwa ndo tunaanza kukimbizana kujenga madarasa as if tulikuwa hatufahamu mahitaji ya madarasa ya mwaka mpya wa masomo ni kiasi gani! Nadhani safari hii litakuwa limeisha lile suala la kukimbizana kimbizana wakati shule zimeshafunguliwa. Na kwavile kazi imefanyika bila mihemuko, naona madarasa mengi yana ubora, at least kwa kuangalia picha!
 
Kwa madarasa 18,000 iwapo kila darasa litachukua watoto 45 kwa mwaka,sawa na watoto 810,000 kwa mwaka watapata Elimu katika mazingira mazuri na ya kisasa. Bado kuna watu wanaona mama hakuna anachofanya. Hivi watanzania mnamtaka mtu ambaye atawafanyia nini?
 
Ila mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni! Hili la madarasa Mama amecheza sana! Jambo ambalo kila mwaka nilikuwa najiuliza ni kwamba inakuwaje shule zikifunguliwa ndo tunaanza kukimbizana kujenga madarasa as if tulikuwa hatufahamu mahitaji ya madarasa ya mwaka mpya wa masomo ni kiasi gani! Nadhani safari hii litakuwa limeisha lile suala la kukimbizana kimbizana wakati shule zimeshafunguliwa. Na kwavile kazi imefanyika bila mihemuko, naona madarasa mengi yana ubora, at least kwa kuangalia picha!
Tupeni uthibitisho japo kwa picha na maeno, wanasiihasa hawaaminiki kamwe na watendaji chini ya ccm.
 
Kila siku tunasikia habari za madarasa mbona hamtuambii idadi ya walimu mliongeza kuendana na ongezeko la wanafunzi kwa sasa?
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh. Abbas Juma Kayanda, ameongoza viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi kupokea Vyumba vya Madarasa 85 vilivyokamilika kwa asilimia 100%.

Katika Hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari ya Himo mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Madarasa yote 85 kupitia fedha za UVIKO 19.

Mhe. Dkt Kimei (Mb) amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kupatikana kwa Fedha zote ambazo ni zaidi ya Bilioni 1.7. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Vunjo tunasema Ahsante Mhe. Rais kwa Fedha hizi Kwasasa tuna uhakika wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wataenda Shule bila shida. Pia, amewapongeza watendaji kwa ushirikiano wao kufanikisha Kukamilika kwa Mradi huo kwa wakati na ubora Mkubwa.View attachment 2061958View attachment 2061959View attachment 2061960View attachment 2061962View attachment 2061961View attachment 2061963View attachment 2061964View attachment 2061965
Watanzania tumshukuru Mungu kwa kutupa viongozi wenye upendo na uzalendo wa kweli kwa nchi yetu.
 
Sasa waanze kujenga shule mpya na kidato cha tano naona hawaongelei kabisa.
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh. Abbas Juma Kayanda, ameongoza viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi kupokea Vyumba vya Madarasa 85 vilivyokamilika kwa asilimia 100%.

Katika Hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari ya Himo mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Madarasa yote 85 kupitia fedha za UVIKO 19.

Mhe. Dkt Kimei (Mb) amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kupatikana kwa Fedha zote ambazo ni zaidi ya Bilioni 1.7. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Vunjo tunasema Ahsante Mhe. Rais kwa Fedha hizi Kwasasa tuna uhakika wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wataenda Shule bila shida. Pia, amewapongeza watendaji kwa ushirikiano wao kufanikisha Kukamilika kwa Mradi huo kwa wakati na ubora Mkubwa.View attachment 2061958View attachment 2061959View attachment 2061960View attachment 2061962View attachment 2061961View attachment 2061963View attachment 2061964View attachment 2061965
Ng'araaa CCM Ng'araaaa
 
Tupeni uthibitisho japo kwa picha na maeno, wanasiihasa hawaaminiki kamwe na watendaji chini ya ccm.
Uthibitisho wa nini ndugu?! Kama ni picha za madarasa, mara kwa mara huwa naziona kule Twitter kwa wana-CCM wenyewe pamoja na kwenye akaunti ya TAMISEMI
 
Uthibitisho wa nini ndugu?! Kama ni picha za madarasa, mara kwa mara huwa naziona kule Twitter kwa wana-CCM wenyewe pamoja na kwenye akaunti ya TAMISEMI
Wote matapeli/wanachukua chako mapema(ccm) kwanini isiwe kwa watanzania wote.
 
Back
Top Bottom