Katika mfululizo wa mizunguko hii nimebahatika kuwasikiliza wanasiasa hawa wa CHADEMA.
Naomba nikubali kwamba wana uwezo wa kupanga hoja. Hawa siyo wachekeshaji kama katibu wa chama tawala au hata mwenyekiti wake.
Wanatoa hotuba za kisiasa zinazoweza kuwasisimua watu wa ufahamu tofauti, siyo ngonjera.