singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,538
Dk. Slaa ambaye ni nadra sana kutofika Makao Makuu ya Chadema Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam, hajakanyaga eneo hilo wiki nzima sasa na tayari pengo lake limeanza kuonekana.
Pengo la kwanza la Dk. Slaa lilionekana jana wakati wa hafla ya kuchukua fomu za urais kwa aliyekuwa kada wa CCM na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond, Edward Lowassa.
Lowassa aliyejiunga na Chadema Jumanne ya wiki hii ni mwanachama pekee wa chama hicho aliyechukua fomu za urais hadi jana, ingawa mchakato huo ulikuwa wazi tangu wiki iliyopita.
Baadaye vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) utawashindanisha wawakilishi wa vyama hivyo ili apatikane mgombea mmoja ingawa pia taarifa zilizowahi kuandikwa na gazeti dada na hili, Raia Mwema, ziliweka bayana kwamba Ukawa ujumla wao wamekwishakukubaliana Lowassa awe mgombea wao wa urais.
Raia Tanzania liliwasilli Mtaa wa Ufipa saa nne asubuhi na kukuta watu wakiupamba mtaa huo tayari kwa mapokezi ya Lowassa.
Lowassa aliwasili ofisini hapo mchana, akapokewa na viongozi wa Chadema, huku wanachama waliokuwapo hapo wakiimba: "Tuna imani na Lowassa! Oyaa oyaaa oyaaaa! Lowassa kweeli! Kweeli…"
Kwa mujibu wa taratibu, mtangaza nia huyo alitakiwa kutia saini kitabu cha wageni katika ofisi ya Katibu Mkuu wa Chadema.
Kwa kuwa mwenye ofisi hiyo, Dk. Slaa hakuwepo wala Naibu wake Tanzania Bara; John Mnyika, ambaye ndiye anayeonekana kufanya shughuli nyingi za ofisi hiyo, ilibidi Naibu Katibu Mkuu upande wa Zanzibar, Salum Mwalimu, ampokee Lowassa.
Hata wakati wa utoaji fomu za urais, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ndiye aliyemkabidhi fomu akisaidiwa na Tundu Lissu pamoja na Mwalimu.
Katika hali iliyoibua maswali mengi, Naibu Katibu Mkuu Bara, Mnyika, hajaonekana hadharani na kazi zake sasa zikifanywa na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Mwalimu, tangu siku ya kutambuliswa kwake katika Hoteli ya Bahari Beach bila kutolewa maelezo ya kina.
Gazeti hili limekuwa likimtafuta Mnyika kutoa ufafanuzi juu ya kutokuwapo kwake katika tukio "muhimu" la kumkaribisha Lowassa na hata kumpatia fomu ya kuwania urais, lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda kwani hadi simu zake za mkononi hazikuwa zikipatikana.
Chanzo: Raia Mwema
Pengo la kwanza la Dk. Slaa lilionekana jana wakati wa hafla ya kuchukua fomu za urais kwa aliyekuwa kada wa CCM na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond, Edward Lowassa.
Lowassa aliyejiunga na Chadema Jumanne ya wiki hii ni mwanachama pekee wa chama hicho aliyechukua fomu za urais hadi jana, ingawa mchakato huo ulikuwa wazi tangu wiki iliyopita.
Baadaye vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) utawashindanisha wawakilishi wa vyama hivyo ili apatikane mgombea mmoja ingawa pia taarifa zilizowahi kuandikwa na gazeti dada na hili, Raia Mwema, ziliweka bayana kwamba Ukawa ujumla wao wamekwishakukubaliana Lowassa awe mgombea wao wa urais.
Raia Tanzania liliwasilli Mtaa wa Ufipa saa nne asubuhi na kukuta watu wakiupamba mtaa huo tayari kwa mapokezi ya Lowassa.
Lowassa aliwasili ofisini hapo mchana, akapokewa na viongozi wa Chadema, huku wanachama waliokuwapo hapo wakiimba: "Tuna imani na Lowassa! Oyaa oyaaa oyaaaa! Lowassa kweeli! Kweeli…"
Kwa mujibu wa taratibu, mtangaza nia huyo alitakiwa kutia saini kitabu cha wageni katika ofisi ya Katibu Mkuu wa Chadema.
Kwa kuwa mwenye ofisi hiyo, Dk. Slaa hakuwepo wala Naibu wake Tanzania Bara; John Mnyika, ambaye ndiye anayeonekana kufanya shughuli nyingi za ofisi hiyo, ilibidi Naibu Katibu Mkuu upande wa Zanzibar, Salum Mwalimu, ampokee Lowassa.
Hata wakati wa utoaji fomu za urais, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ndiye aliyemkabidhi fomu akisaidiwa na Tundu Lissu pamoja na Mwalimu.
Katika hali iliyoibua maswali mengi, Naibu Katibu Mkuu Bara, Mnyika, hajaonekana hadharani na kazi zake sasa zikifanywa na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Mwalimu, tangu siku ya kutambuliswa kwake katika Hoteli ya Bahari Beach bila kutolewa maelezo ya kina.
Gazeti hili limekuwa likimtafuta Mnyika kutoa ufafanuzi juu ya kutokuwapo kwake katika tukio "muhimu" la kumkaribisha Lowassa na hata kumpatia fomu ya kuwania urais, lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda kwani hadi simu zake za mkononi hazikuwa zikipatikana.
Chanzo: Raia Mwema