nadhani mjadala huu unafanywa na watu ambao hawakuweppo wakati akina DJ JD wako active kwenye fani. hao mnaowataja siku hizi sioni umahiri wao. ukitaka kuhakikisha hilo angalia kwenye hizo radio station zenu na tv. utagundua kuwa kila alikopita JD na wenzake wa kizazi chake ( kina Rankim, fast Eddie, Misanya,Master T , prince Baina kamukulu- young Millionaire nk), vipindi walivyovianzisha vimebaki hivyohivyo hadi leo na wale walioanzisha vipya kwenye vituo vipya waliiga mfumo uleule waliouacha. kama unabisha fanya utafiti wewe mwenyewe utaona ukweli. kama hao wa siku hizi ni wakali mbona wanashindwa kuja na jipya kwenye fani? kuna mtu hapo juu kawaita music selectors, kama kuna kaukweli vile. hivi si nasikia matangazo ya watu kutaka kukumbushwa Tazara, Pink coconut, silent inn! hii maana yake nini? kuna mapungufu kwenye entertainment indusrty? au ya kale dhahabu?! ni mtazamo wangu.