mchumi tumbo
JF-Expert Member
- Mar 2, 2018
- 832
- 996
DIRISHA JINGINE UDSM:
CHUO kikuu cha Dar as Salaam kitafungua dirisha jingine la maombi udahili kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Elimu ya juu mwaka huu.
Akizungumza katika kipindi cha Jambo kinachorushwa na shirika la Utangazaji Tanzania @tbchabari, Naibu Makamu Mkuu Taaluma, Prof. Bonaventure Rutinwa amesema hadi sasa chuo kikuu cha Dar es Salaam kimeshadahili wanafunzi #7600 hivyo baada ya kikao cha Jana kati ya UDSM, TCU na Waziri Prof. Ndalichako, Sasa UDSM itatakiwa kudahili wanafunzi kulingana na uwezo wake mama ambao ni takribani wanafunzi #15000, idadi ambayo ni karibu Mara mbili ya waliodahiliwa.
Aidha dirisha hili la udahili ambalo litafunguliwa kwa siku nne hadi tano (taarifa kamili itatoka) litagusa programu zote #92 za Chuo hicho huku mwombaji akitakiwa kuomba chuo pasipo matumizi ya codes kama ilivyokuwa ikifanyika siku chache zilizopita na TCU.
Aidha dirisha hili litawahusu wanafunzi ambao;
1. Walikosa vyuo
2. Walipata tabu kutokana na changamoto za confirmation codes
3. Waliomba UDSM lakini kutokana na changamoto mbalimbali wakathibitisha vyuo vingine
Sasa wataomba nafasi hiyo kwa kuzingatia vigezo ambavyo chuo kikuu cha Dar es Salaam kinahitaji!
Katika hatua nyingine Prof. Rutinwa amezungumzia hali ya Taaluma ya Chuo na kusema kwamba hali ni nzuri ukitizama katika msimamo wa ubora wao vyuo kidunia ambapo UDSM kinafanya vizuri kusini mwa jangwa la Sahara.
Aidha kuhusu Malazi, amesema hali siyo mbaya sana, kwani serikali imejenga hostel za Magufuli huku wakiwa katika mkakati wa "tendering " kukarabati Hall 2&5
C&P
CHUO kikuu cha Dar as Salaam kitafungua dirisha jingine la maombi udahili kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Elimu ya juu mwaka huu.
Akizungumza katika kipindi cha Jambo kinachorushwa na shirika la Utangazaji Tanzania @tbchabari, Naibu Makamu Mkuu Taaluma, Prof. Bonaventure Rutinwa amesema hadi sasa chuo kikuu cha Dar es Salaam kimeshadahili wanafunzi #7600 hivyo baada ya kikao cha Jana kati ya UDSM, TCU na Waziri Prof. Ndalichako, Sasa UDSM itatakiwa kudahili wanafunzi kulingana na uwezo wake mama ambao ni takribani wanafunzi #15000, idadi ambayo ni karibu Mara mbili ya waliodahiliwa.
Aidha dirisha hili la udahili ambalo litafunguliwa kwa siku nne hadi tano (taarifa kamili itatoka) litagusa programu zote #92 za Chuo hicho huku mwombaji akitakiwa kuomba chuo pasipo matumizi ya codes kama ilivyokuwa ikifanyika siku chache zilizopita na TCU.
Aidha dirisha hili litawahusu wanafunzi ambao;
1. Walikosa vyuo
2. Walipata tabu kutokana na changamoto za confirmation codes
3. Waliomba UDSM lakini kutokana na changamoto mbalimbali wakathibitisha vyuo vingine
Sasa wataomba nafasi hiyo kwa kuzingatia vigezo ambavyo chuo kikuu cha Dar es Salaam kinahitaji!
Katika hatua nyingine Prof. Rutinwa amezungumzia hali ya Taaluma ya Chuo na kusema kwamba hali ni nzuri ukitizama katika msimamo wa ubora wao vyuo kidunia ambapo UDSM kinafanya vizuri kusini mwa jangwa la Sahara.
Aidha kuhusu Malazi, amesema hali siyo mbaya sana, kwani serikali imejenga hostel za Magufuli huku wakiwa katika mkakati wa "tendering " kukarabati Hall 2&5
C&P