GE2025 Devotha Minja: CHADEMA, CUF na ACT tuungane adui yetu ni CCM

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Haina utofauti na UKAWA ambayo bado ilishindwa na hicho kichama cha Mafisadi CCM, hivyo siyo tu kuungana bali mikakati makini inahitajika kumnyanganya mtu tonge wakati na yeye ana njaa ni kipengele

Huyu Devotha mwenyewe kakimbia Chadema kwenda Chaumma alafu tena anataka waungane kwa nini asingebaki huko chadema asisitize vyama vya upinzani kuungana kukataa huu uchaguzi ubatili
---------------
Mgombea mwenza Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Devotha Minja ameviomba vyama vya upinzani Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ACT- Wazalendo na Chama cha Wananchi (CUF) kuunganisha nguvu ili kukiondoa Chama cha Mapinduzi (CCM) madarakani

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Kirumba Sokoni wilayani Ilemela, Minja amesema adui wa vyama vya upinzani ni CCM hivyo waunganishe nguvu kikitoa madarakani ili kuleta mabadiliko na maendeleo nchini

"Sasa ndugu zangu CHADEMA, CUF, ACT - Wazalendo tuunganisheni nguvu adui yetu ni CCM, kuna watu wanawaambia watu wasusie uchaguzi hawa majamaa ukiwasusia uchaguzi ndio kwanza wanalala usingizi, wanachekelea wanabaki wenyewe," amesema Minja

Aidha, Mgombea Ubunge kupitia CHAUMMA Jimbo la Ilemela, Veronica Mgeta amedai ni wakati wa wananchi kufanya mabadiliko na kukipa nafasi Chama hicho kuongoza nchi angalau kwa Miaka mitano ili kutatua matatizo ya wananchi


Your browser is not able to display this video.
 
Ukawa ulikuwa na nguvu 2015 sana ila walipo ingiza tamaa tu ndio msambaratiko ulipo anzia sijui kama utatokea muunganiko kama ule
 
Leo ndio hata wale waliosaliti harakati za ukombozi wanajua adui yetu na adui wataifa ni nani basi tumechelewa sana.Ingekuwa mapema hata zile hila za Chaubwabwa na washirika wao zisingefanyika!
 
Kuna Catherine huyu dada alikutwa na nini baada ya Uchaguzi sijui wataishi vipi?
Nilikua na matumaini naye siku moja atamtoa abood. Ila amejua kijidhalilisha. Hii NRNE imeonesha namna gani viongozi wengi wapo after kula yao
 
ACT NA CUF Wataungana pindi rais ni mkristo. Tusichoshane.
 
Hao wapinzani wangekua na nia hiyo kweli wala wasingekua na vyama zaidi ya 15.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…