Mkuu wa wilaya Tandahimba Mhe. Sebastian Waryuba amekabidhi vitambulisho kwa Wajasiliamali wadogo 50 ambavyo Msanii Harmonize wa kundi la Wasafi aliwanunulia Wajasiliamali hao.
DC Waryuba amekabidhi vitambulisho hivyo nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kumshukuru Msanii Harmonize kwa moyo wake wa upendo kwa Wajasiliamali wadogo na kumuunga mkono Rais Magufuli ambaye ndiye aliyetoa Vitambulisho hivyo.
"Sisi wana Tandahimba tunamshukuru sana Msanii Harmonize kwa kutimiza ahadi yake ya msaada wa vitambulisho 50 alivyotoa kwa Wajasiliamali na kwa kumuunga mkono Rais Magufuli. Mwenyezi Mungu azidi kumbariki Msanii Harmonize." Alisema DC Waryuba.
Mnamo Machi 16, 2019 msanii Harmonize alitoa ahadi ya kuwanunulia vitambulisho kwa Wajasiliamali 50 kwenye mkutano uliofanyika stendi ya mabasi Tandahimba ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Byakanwa alikuwa mgeni rasmi.
Sent using Jamii Forums mobile app
DC Waryuba amekabidhi vitambulisho hivyo nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kumshukuru Msanii Harmonize kwa moyo wake wa upendo kwa Wajasiliamali wadogo na kumuunga mkono Rais Magufuli ambaye ndiye aliyetoa Vitambulisho hivyo.
"Sisi wana Tandahimba tunamshukuru sana Msanii Harmonize kwa kutimiza ahadi yake ya msaada wa vitambulisho 50 alivyotoa kwa Wajasiliamali na kwa kumuunga mkono Rais Magufuli. Mwenyezi Mungu azidi kumbariki Msanii Harmonize." Alisema DC Waryuba.
Mnamo Machi 16, 2019 msanii Harmonize alitoa ahadi ya kuwanunulia vitambulisho kwa Wajasiliamali 50 kwenye mkutano uliofanyika stendi ya mabasi Tandahimba ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Byakanwa alikuwa mgeni rasmi.
Sent using Jamii Forums mobile app