Dawa ya mawe ya tonsez

Whitney Houston

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2019
Posts
237
Reaction score
444
Habari wakuu.

Kwa anaefahamu tiba ya mawe ya tonsezi !tonsil stones! naomba anisaidie.aidha ya kienyeji au ya hospitalini. haziniumi ila ni hayo mawe tu ndo yananisumbua,na kunikera kwasababu yana harufu mbaya.

Huwa yanajirudia mara kwa mara, huwa najaribu kutumia maji ya chumvi, hydrogen peroxide, dawa ya meno ya kawaida kujisafisha mara kwa mara lakini havisaidii.
 
Tusaidiwe tu dawa kwa kweli maana siku tatu zilizopita nilikuwa nasikia maumivu nikahisi NI maji ya baridi ninayokunywa kwa joto hili, jana usiku lilitoka moja kubwa mkuu ni kubwa pale pale.na maumivu yakaisha, mwenye dawa msaada tafadhali
 
Husabaishwa na nini tonsil stone
 
Polee sana mkuu. Mm pia nilikua nasumbuliwa na tonsil stones.. Nilisukutua na chumvi lakini wapi? Dokta akaniambia ni bacterial infection iyoo nitumie dawa inaitwa Azithromycin( AZUMA as a trade name) 1x2 for 3dayz. Baada ya kumaliza dozi siku ya 4 vikapotea mpka leo ni mzima sina tena. Kwaio na ww fanya ivo naamini utapona. ukipona usisahau kuleta mrejesho apa mkuu.
 
Ni ugonjwa unaoathiri kinundu Cha kooni,kwa kawaida kinundu hiki huvimba,kuwa chekundu na kuuma wkt wa kumeza kitu chochote hata mate.
someni Kitabu cha DAWA ZA SHAMBANI kina maelezo mengi kuhusu magonjwa na tiba zake.kipo insta maisha na uhusiano
Unachanganya Mambo Tonsil Stones sio hicho unachoelezea.

Acha kupotosha!

Msome vizuri mleta mada utaelewa anachoeleezea sio hicho unachoelezea wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…