CUF yapinga rasmi matokeo Jimbo la Mbagala

CUF yapinga rasmi matokeo Jimbo la Mbagala

TAWA

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2013
Posts
3,674
Reaction score
1,572
Chama cha Wananchi (CUF) kimeuweka rehani ushindi wa mbunge mteule wa Jimbo la Mbagala kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Issa Mangungu, baada ya kufungua kesi kikipinga matokeo yaliyompa ushindi huo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2015 ilifunguliwa jana na aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo kupitia CUF, Kondo Bungo, dhidi ya Mangungu, Msimamizi wa Uchaguzi (Returning Officer- RO) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Hiyo ni kesi ya kwanza ya uchaguzi kufunguliwa kupinga matokeo ya ubunge kwa majimbo ya Dar es Salaam.

Katika kesi hiyo, Bungo anapinga matokeo yaliyompa ushindi Mangungu, huku akiiomba Mahakama Kuu itamke kuwa uchaguzi huo ulikuwa batili.

Miongoni mwa madai yake ni kwamba uchaguzi huo uligubikwa na kasoro nyingi na ukiukwaji wa taratibu, kanuni na sheria za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), na kwamba ukiukwaji huo wa sheria umeathiri matokeo ya uchaguzi huo.

Kwa mujibu wa hati ya madai yake aliyoiwasilisha mahakamani hapo, Bungo anadai kuwa mdaiwa wa pili (RO) alimteua na kumpangia kituo cha uchaguzi katika vituo vya upigaji kura, kata ya Kiburugwa ofisa ambaye ni ndugu wa mdaiwa wa kwanza (Mangungu).

Bungo anadai kuwa ofisa huyo ambaye ni ndugu wa mdaiwa wa kwanza, aliendesha uchaguzi pasi usawa na hivyo kuathiri uchaguzi huo.

Vilevile, Bungo anadai kuwa RO aliunda na kutambulisha kituo hewa cha uchaguzi kilichoitwa Makuka Kusini 4A, katika Kata ya Mbagala Kuu, jambo ambalo liliathiri uchaguzi.

Bungo anaendelea kudai kuwa RO na wasaidizi wake kinyume cha sheria waliruhusu mabango ya mdaiwa wa kwanza kubakia katika vituo vya kupigia kura vya kata za Kiburugwa, Tuangoma na Mbagala Kuu, licha ya malalamiko ya mawakala wake.


Chanzo:
Mwananchi
 
Safi sana. Ccm walichofanya mbagala ni uhuni usiokubalika na yoyote popote
 
Hao wanajisumbua tu! sidhani kama watapata ushindi kwa style hii.
Yangu maskio, ntaskia tu kitakachoendelea
 
Usimtukane mamba kabla hujavuka mto hivi nyie si ndo mlisema mahakama zote za TZ ni za CCM na zinaipendelea ccm sasa iweje leo mkimbilie huko?
 
Kwa hiyo mahakama zetu hazitendi haki!?

Nenda kawaulize kila kitu kwanini walipatiza cha ccm eti pilisiccm, tbccm, mahakama wakasema ya ccm sasa leo akili zimekaa sawa wanajifanya kwenda ha ha ha ha acheni hizo,
 
Tutakwenda mahakamani huku tukiwa na hofu juu ya majaji ambao karibu wote ni wateule wa mkwere. Jaji alikuwa Mchome na wengine waliopita, walipiga chini Premji wa ccm Kigoma bila hofu. Kwa hasira za ccm, tofauti na wanavyofanyia majaji wengine, Mh. Jaji Mchome muda wa kustaafu ulipofika hawakumuongezea hata lisaa. Tutaendelea kupambana kwa mfumo huu huu mbovu mpaka hapo watanzania watapofumbuka macho kuwa ccm ni mfumo ovu usiostahili kuwepo chini ya jua.
 
Nenda kawaulize kila kitu kwanini walipatiza cha ccm eti pilisiccm, tbccm, mahakama wakasema ya ccm sasa leo akili zimekaa sawa wanajifanya kwenda ha ha ha ha acheni hizo,

Hivi ile dozi yako ya kichaa cha mbwa ukishamaliza?
 
Nenda kawaulize kila kitu kwanini walipatiza cha ccm eti pilisiccm, tbccm, mahakama wakasema ya ccm sasa leo akili zimekaa sawa wanajifanya kwenda ha ha ha ha acheni hizo,
kuwa msomi...fikiria japo kwa kichwa leo...siyo mahakama zote/mahakimu au majaji ni pro CCM...wengine ni wadilifu siyo vibaka wa siasa...sasa ulitaka aende wapi? so stupid and raw!! nimekuchukia ghafla
 
Jamani fanyeni masiala na vyama vyote lakini sio cuf......na mashabiki wakeee,........ ...

Mwaka 2005 walianzisha mzozo hatari pale kidongo chekundu na polisiii hadi igp mahita alijuzulu ,
 
Iwekwe akaunti maalum ili tuweze kuchangia gharama za kesi .
 
Jamani fanyeni masiala na vyama vyote lakini sio cuf......na mashabiki wakeee,........ ...

Mwaka 2005 walianzisha mzozo hatari pale kidongo chekundu na polisiii hadi igp mahita alijuzulu ,

Naunga mkono hoja
 
Back
Top Bottom