Crdb hii ni kero................you need to change plz....!!!

Hata mimi nadhani bado crdb ni bank nzuri sana, mumy go online utaenjoy...nadhani hayo ni mapungufu madogo madogo ya kufanyia kazi (housekeeping)

Mkuu na sisi tulikuwa tunaisifu CRDB kabla ya mikasa kutukuta. Hayo ya teller ni madogo, bank inadai kutoa huduma za kibenki cha ajabu ukihitaji hizo huduma usumbufu utakaopata utalazimika kwenda kutafuta hizo huduma kwingine.
 
Kweli wakuu wadada wa CRDB tellers wanajiona sana!mimi siku moja nilimuwekea mtu hela haopo CRDB Premier branch,nimempa elfu 50,kaingiza elfu 5!kisa alikua anaongea na simu mara ooh swt,habari za tangu jana!anacheka tu na mimi namtizama!ana bahati angeongeza sifuri iwe laki 5 ndio mwisho wake wa kazi ungekua ni siku hiyo!

Wanajitahid kuboa kwa kweli
 
Wallah CRDB wanatia hasira<br />
Niliomba kuunganisha na huduma ya online banking (nipo mkoa), majibu yalivyokuja wamenipa username na password zisizofanya kazi! nimeenda local branch hakuna wanalojua kuhusu hiyo huduma!mtu nayetakiwa kuwasiliana naye panapo shida ni Sarah Nzowa (Yupo dar), kichekesho ni kwamba branch nzima hakuna mtu mwenye simu yake ya kiganjani, na kwenye barua hakuna contact yoyote,...HATA S.L.P!
<br />



NI KWELI KAKA,HATA MIMI NILIPATA UZOEFU HUOHUO KAKA,MIMI WALINIAMBIA PALE LUMUMBA KWAMBA NAHITAJI KUWA MTEJA WA VODA ILI NIPATE HUDUMA YA KIBENKI KWENYE SIMU,ITS DISGUSTING!!!
<br />
 
Tatizo ni kwamba hao wafanyakazi hawana motivation ya kutosha,ukumbuke wakati mkuu wa bank anatamba kukua kwa bank na faida kubwa,wafanyakazi wanalipwa kidogo sana tena ukizingatia mfumuko wa bei manake ni kwamba kila kukicha hao wafanyakazi shida zinaongezeka kwani uwezo wa fedha wanazopata unapungua.Hawana jinsi inabidi wajiendee hivyo hivyo kwani hawana jinsi nyingine ya kujipatia kipato.Niliwahi kufanya kazi hiyo bank,siku MD anatangaza mafanikio ya bank anayekuwa na furaha kweli ni yeye na wala si wafanyakazi walio wengi,inaumiza sana pale wanapokuwa wamefanya kazi sana kuifikisha bank ilipo wakati bank haiwajali vya kutosha na kutambua mchango wao kikamilifu.Mie niliamua kuondoka nikaachana na mambo ya kutimiza ndoto za watu sasa hivi natimiza ndoto zangu mwenyewe,naamka na furaha na kulala na furaha kila siku.
 
Hii bank huwa naambiwa ni one of the best and efficient banks in Tanganyika, in short ndo bank nzuri ya kwanza ya kizalendo kwa huduma tanganyika sasa kama hao staff wao wameanza kuleta marangi basi itaanguka muda si mrefu/ at least kupungukiwa wateja hasa wa mjini!

Nimehama kuitumia akaunti yangu ya CRDB, wamebadilika ghafla na kuwa wabaya kuliko benki yoyote unayoifahamu. Kuanzia hao staff ukiingia ndani utawekwa pending kama kiazi cha juzi. Huduma mbovu kabisa. Ukija kwenye akaunti kama ulichukua mkopo kupitia kwa mwajiri ndio utajuta. Hela yoyote inayoingia kwenye akaunti yako wanakusanya tu pamoja na wanayopelekewa na mwajiri toka kwenye mshahara wako. Na mbaya zaidi, ukienda ATM kuchukua unakuta imefungwa. Ukiingia ndani kufuatilia utajuta jinsi utakavyowekwa kiporo. Imenitokea mara 2 kabla ya kusitisha kupitishia huko hela, na safari zote 2 akaunti ilifunguliwa baada ya siku 2 za kufuatilia. Hela iliyochakachuliwa ilirudishwa lakini ni baada ya siku 3. Sasa kama una dharula ya ghafla unakimbia ATM ya CRDB, utajuta kujiunga nao.

Binafsi kwangu hii benki imeshindwa vibaya.
 
Msiseme mabank tu, mawizarani mmefika ? Taasisi zingine za serikali je including TRA ? Vp kuhusu mahospitalini nako mmeenda ? Kiujumla Tanzania hakuna sehemu yenye customer care nzuri zaidi ya bar, na ndio maana Watanzania tunapenda kushinda bar angalau kurelease stress !!

:crazy:
 
Msiseme mabank tu, mawizarani mmefika ? Taasisi zingine za serikali je including TRA ? Vp kuhusu mahospitalini nako mmeenda ? Kiujumla Tanzania hakuna sehemu yenye customer care nzuri zaidi ya bar, na ndio maana Watanzania tunapenda kushinda bar angalau kurelease stress !!

:crazy:

You have to love JF!!
 
Back
Top Bottom