CRDB Bank mpaka kanisani!

sioni shida kwa watu wa bank kwenda kanisani kumshukuru Mungu. Pale hawajafanya biashara yoyote wameenda kumshukuru Mungu. Mbona NBC ishakuwa bank ya kiislam.
 
Jamani, tusidanganyane!
Ni wazi kabisa kwa maelezo ya mleta mada crdb waliomba misa.
Utaratibu huu wa kuomba misa sina shida nao, ishu ni je crdb ilitoa maelekezo kama hayo ili yafanyike pia msikitini?...vinginevyo itakuwa si sahihi kumshukuru Mungu wa Kanisa huku Allah akisahauliwa, maana benki ina WATEJA wa dini zote kuu!!
 
We endelea kushangaa wenzio wana barikiwa na kufanikiwa siku zote, Tumeamriwa tuwe na moyo wa shukurani, Utakua si binadamu usie na shukurani, Mbona hata hao wanasiasa wanaomba Makanisa ya ombee taifa. mbona huhoji Dini inapotumika mahakamani na kwenye viapo? Chako choko changu chetu, Acha ubinafsi na usirudie kushangaa uwepo wa MUNGU kila Mahala KILA KITU NI MALI YAKE MUNGU.
 
Hivi CRDB haina wateja waislam??

Hivi CRDB in Christian Bank???

Je nini maana ya PLC -Public Liability Company??
 
Watanzania tulivyo na maneno mengi...! Yani hapa basi utaanza udini,siasa,kejeli na mambo mengine kibao yasiyoeleweka!
Lakini kitaalamu hapa hilo ni tangazo la biashara ndani ya kanisa...na kama ni hivyo basi na makampuni mengine yatakuja kuomba na mwisho wa siku tutakuta mpaka mabango kanisani..
 
bank ya kichaga kanisa la kichaga
 
Ile misa iliombwa na wafanyakazi wa crdb tu,wala sio benki!
 

Kwenye Red kumenifurahisha na litakuwa Tangazo zuli sana,Lakini hatari
 
Kwa wakatoliki kuomba misa kwa ajili ya shukrani ni jambo la kawaida, hata wao wana benki yao inaitwa mkombozi. Kama mtu binafsi anaweza kuomba misa kwa ajili ya mafanikio aliyopata, je kwa nini iwe kosa kwa benki kuomba misa wakati wateja wake hufanya hivo kwa mafanikio waliyopata? Tafakari zaidi
 

Actually kuna tatizo kubwa, na contrary to your claim, CRBD badala ya kuimarisha umoja wa Watanzania/ wateja wao, inawagawanya.

Waislam watauliza kwa nini shughuli za benki isiyo na dini zipelekwe kanisani? Mgogoro unaanzia hapo.
 
Waliamini kwamba Kristo ndio kweli,ndio mwanga,ndio mafanikio na kila kitu!
 
Waliamini kwamba Kristo ndio kweli,ndio mwanga,ndio mafanikio na kila kitu!

Hii si moja ya kanuni ya banking.

As a matter of fact Kristo (au hadithi zake kwa sisi tusioamini kwamba alikuwepo kikweli) alikuwa hapendi watoza ushuru ambao kwa dunia yetu ya leo wako pamoja na watoza riba.

Umemsoma Kristo vizuri na kujua attitude yake kuhusu fedha (msingi wa banking).

Umesoma alivyoparaganya waliojaribu kufanya biashara katika "nyumba ya baba yake" ?

Umesoma alivyosema kuhusu "Mpeni Kaisari vya Kaisari na mungu vya mungu"?

Kwa nini watu wanataka kuchanganya biashara na dini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…