Club ya Simba yakomboa nyasi zake za Bandia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Good People

JF-Expert Member
Aug 6, 2016
945
1,819
Hatimaye Klabu ya Simba SC imelipa kodi iliyokuwa inadaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya nyasi bandia walizokuwa wamezitelekeza bandarini mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu.




kaburu1.JPG

Geofrey Nyange 'Kaburu'

Hatua hiyo imekuja baada ya TRA kutangaza kuzipiga mnada nyasi hizo endapo wangeshindwa kukomboa kwa siku 14 waliozokuwa wamepewa ambazo zilimalizika juzi Jumanne.

"Mpaka sasa tumeshalipia kodi yote ya nyasi bandia, kinachoendelea sasa hivi ni wakala wetu kumalizia taratibu za kutoa 'container' zenye nyasi hizo bandarini kwenda kuwekwa rasmi katika uwanja wetu wa Bunju". Alisema Makamu wa Rais wa klabu ya hiyo Geofrey Nyange 'Kaburu'.

Kwa upande mwingine klabu hiyo inaendelea kujiandaa na mchezo ujao wa ligi kuu dhidi ya Mbao FC unaotarajiwa kupigwa katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza Jumatatu ijayo.
 
Dar Es Salaam hakuna udongo mzuri wa ku-support hizo nyasi...na maji ni issue
Haa! sio kweli hata kidogo. Ni uvivu wetu tu. Viwanja vinajengwa jangwani na Norway kwenye barafu sembuse Dar? Halafu maji ndio usiseme tena! Maji hayamfuati mtu ila mtu ndiye anayeleta maji
 
Yanga mngezigomboa mkaenda kuhifadhi kwenye bwawa lenu LA chura pale jangwani tungepiga maombi tu mvua kama ya mwezi WA pili ije ilete mafuriko mkayakute majani sallender bridge.
 
Haa! sio kweli hata kidogo. Ni uvivu wetu tu. Viwanja vinajengwa jangwani na Norway kwenye barafu sembuse Dar? Halafu maji ndio usiseme tena! Maji hayamfuati mtu ila mtu ndiye anayeleta maji
sasa unataka tukaweke mabomba ruvu ili tupande za asili?
 
Back
Top Bottom