Clinical Medicine au Biomedical equipment engineering

Clinical Medicine au Biomedical equipment engineering

iam_Muhammad

Member
Joined
Sep 19, 2017
Posts
29
Reaction score
12
Wadau kati ya course tajwa hapo juu ipi tamu? hasa interms of fursa nyingi za ajira!
 
Diploma in Clinical medicine.
1.AJIRA
Ni kozi ya kawaida kwa miaka ya hivi sasa,ajira zipo lakini zimepungua kulinganisha na miaka ya nyuma.Unaweza kutafuta ajira kwenye zahanati au vituo vya afya vya binafsi ukakosa hii ni kutokana na wingi wa watu walio soma kozi hii kwa sasa.Mfano mwaka 2017 miezi ya mwanzo kabla serikali haijapunguza watu wa afya kidogo kwa kutoa ajira 2400 za kada ya afya, MD na CO walikuwa wanagombania vijiwe kwa mshahara ule ule.Kwahiyo usisome ukitegemea ajira haraka haraka baadaya kumaliza.Huwezi amini kuna CO walio malliza mwaka 2018 mpaka leo hawana ajira na hata zahanati za binafsi ni shida..

2.NACTE
Usipo kaza ki sawa sawa unaweza kuchukua miaka mitano bila cheti ,mtihani ya NACTE lengo ni kupunguza watu katika kozi hii.Unaruhusiwa kufanya supplimentary mara mbili tu ukifeli unarudi nyumbani bila chet..

3.KUJIENDELEZA'

Wengi waliosoma kozi hii wanalia sana maana hawa kupata GPA ya 3.5 .Wanaopata GPA kama hii ni wachache sana.Wengi walitamani kuendelea lakini ukiona GPA iko chini 3.5 baasi sahau udaktari kabisa na pengine ukasome kozi nyingine au ukarudi kureast mtihani wa form six (PCB).Hii ni baada ya serikali kufuta kozi ya ADVANCED DIPLOMA IN CLINICAL MEDICINE(AMO) ambapo walikuwa chukua kuanzia GPA ya 2.7.

HITIMISHO; Ni kozi nzuri sana ukifaulu vizuri na kwa wakati, lakini pia ukiwa nasubira ya ajira kumbuka Clincal officer anatakiwa kuwa kwenye Zahanati na kiwango kidogo kituo cha afya tu.


DIPLOMA IN BIOMEDICAL ENGINEERING

1.Utangulizi

Ni kozi ambayo imeanzishwa hivi karibuni mwaka 2012, kwa mara ya kwanza ilikuwa inatolewana chuo cha DIT na baadaye Arusha Technical.Kwa miaka nyuma hatukuwa na kozi hii katika chuo chochote hapa nchini na hivyo walio kuwa wanafanya kazi hizi walikuwa na watu waliosomea nchini kenya au wa hitimu wa Electronics walio maliza vyuo vya UDSM,ST.JOSEPH na DIT.

2.AJIRA

Tofauti na matarajio ya wengi ajira na hata field zinahitaji uvumilivu kuliko hata Clinical medicine.Hii ni kutokana kuwa ajira nyingi zinategemea serikali itangaze ajira,kwa hiyo unaweza kumaliza miaka miwili ukisubiri ajira lakini zikitoka uhakika wa kupata ni asilimia 100.Makampuni mengi ya vifaa tiba(MEDICAL EQUIPMENT SUPPLY) kama Anudha,Crown,Kasmedics,Pyramid pharm,Pasific diagnostic,Bio care. e.t.c.Wengi hawa hitaji fresh from school,wengi wamejaza wageni kutoka Kenya na India na hata hivyo hawa hitaji watu wengi unaweza kukuta wanataka watu watatu au wawili wakati wahitimiu ni wengi.Kwa sasa vyuo vinavyo toa kozi za Biomedical Engineering ni vitatu (DIT,MUST na ATC).Hospitali za binafsi nyingi hazi hitaji kabisa Bio medical Technicians baadala yake kifaa kikiharibika huita kampuni husika na kutengeneza na maisha yanasonga.Mpaka sasa Hospitali za binafsi nchi nzima zenye Bio-medical techician/engineers ni Aga khan (DSM) ,TMJ Hospital (DSM) na Regency(DSM) hata hivyo hospitali hizo ni hospitali moja tu ambayo imeajili watanzania katika kitengo hicho.

CHANGAMOTO ZA AJIRA KATIKA KOZI HII

1. Wahitimu asilimia kubwa hawana uwezo wa kutatua changamoto za vifaa tiba kwa usahii ,hii ni kutokana na kukosa mafunzo kwa vitendo kutoka kwenye hospitali kubwa kama MUHIMBILI,BUGANDO ,AGA KHAN NA KCMC.Wahitimu wengi wamekuwa wakisemwa vibaya na waajiri wao na hasa walioko Hospitali za serikakli.,na hivyo utawala wa hospitali hizi hulazimika kutafuta fundi kwenye kampuni wakati wanaye fundi mwajiriwa.

HITIMISHO ;Aira zipo lakini zinahitaji subira ya serikali tu,hii nikutokana kuwa na makampuni ya vifaa tiba machache na hospitali nyingi za private kutokuwa na kitengo hicho.
 
Diploma in Clinical medicine.
1.AJIRA
Ni kozi ya kawaida kwa miaka ya hivi sasa,ajira zipo lakini zimepungua kulinganisha na miaka ya nyuma.Unaweza kutafuta ajira kwenye zahanati au vituo vya afya vya binafsi ukakosa hii ni kutokana na wingi wa watu walio soma kozi hii kwa sasa.

Mfano mwaka 2017 miaezi ya mwanzo kabla serikali haijapunguza watu wa afya kidogo kwa kutoa ajira 2400 za kada ya afya MD na CO walikuwa wanagombania vijiwe kwa mshahara ule ule. Kwahiyo usisomeuktegemea ajira haraka haraka haraka baadaya kumaliza...
Nashukuru sana kwa ufafanuzi wako mzuri
 
Diploma in Clinical medicine.
1.AJIRA
Ni kozi ya kawaida kwa miaka ya hivi sasa,ajira zipo lakini zimepungua kulinganisha na miaka ya nyuma.Unaweza kutafuta ajira kwenye zahanati au vituo vya afya vya binafsi ukakosa hii ni kutokana na wingi wa watu walio soma kozi hii kwa sasa.Mfano mwaka 2017 miezi ya mwanzo kabla serikali haijapunguza watu wa afya kidogo kwa kutoa ajira 2400 za kada ya afya, MD na CO walikuwa wanagombania vijiwe kwa mshahara ule ule.Kwahiyo usisome ukitegemea ajira haraka haraka baadaya kumaliza.Huwezi amini kuna CO walio malliza mwaka 2018 mpaka leo hawana ajira na hata zahanati za binafsi ni shida.
Umemaliza kila kitu, tena hiyo Clinical Medicine ajipange, siku hizi Mitihan ya NACTE ni kila mwaka, Kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa tatu, na disco zipo za kutosha.. ila kwa ushauri wangu kama anajiweza apige Clinical Medicine, baadae rahisi kujiendeleza
 
Umenena vyema kiufupi kwa C.O kama ana mpango wa kusoma Mpaka MD aende angalau itabeba japo akaze msuli ila kama hana mpango aachane na hiyo kozi maana kwa sasa C.O hakuna kazi watu wanafanya kazi vijiweni malipo 10k per day.
Diploma in Clinical medicine.
1.AJIRA
Ni kozi ya kawaida kwa miaka ya hivi sasa,ajira zipo lakini zimepungua kulinganisha na miaka ya nyuma.Unaweza kutafuta ajira kwenye zahanati au vituo vya afya vya binafsi ukakosa hii ni kutokana na wingi wa watu walio soma kozi hii kwa sasa.Mfano mwaka 2017 miezi ya mwanzo kabla serikali haijapunguza watu wa afya kidogo kwa kutoa ajira 2400 za kada ya afya, MD na CO walikuwa wanagombania vijiwe kwa mshahara ule ule.Kwahiyo usisome ukitegemea ajira haraka haraka baadaya kumaliza.Huwezi amini kuna CO walio malliza mwaka 2018 mpaka leo hawana ajira na hata zahanati za binafsi ni shida..

2.NACTE
Usipo kaza ki sawa sawa unaweza kuchukua miaka mitano bila cheti ,mtihani ya NACTE lengo ni kupunguza watu katika kozi hii.Unaruhusiwa kufanya supplimentary mara mbili tu ukifeli unarudi nyumbani bila chet..

3.KUJIENDELEZA'

Wengi waliosoma kozi hii wanalia sana maana hawa kupata GPA ya 3.5 .Wanaopata GPA kama hii ni wachache sana.Wengi walitamani kuendelea lakini ukiona GPA iko chini 3.5 baasi sahau udaktari kabisa na pengine ukasome kozi nyingine au ukarudi kureast mtihani wa form six (PCB).Hii ni baada ya serikali kufuta kozi ya ADVANCED DIPLOMA IN CLINICAL MEDICINE(AMO) ambapo walikuwa chukua kuanzia GPA ya 2.7.

HITIMISHO; Ni kozi nzuri sana ukifaulu vizuri na kwa wakati, lakini pia ukiwa nasubira ya ajira kumbuka Clincal officer anatakiwa kuwa kwenye Zahanati na kiwango kidogo kituo cha afya tu.


DIPLOMA IN BIOMEDICAL ENGINEERING

1.Utangulizi

Ni kozi ambayo imeanzishwa hivi karibuni mwaka 2012, kwa mara ya kwanza ilikuwa inatolewana chuo cha DIT na baadaye Arusha Technical.Kwa miaka nyuma hatukuwa na kozi hii katika chuo chochote hapa nchini na hivyo walio kuwa wanafanya kazi hizi walikuwa na watu waliosomea nchini kenya au wa hitimu wa Electronics walio maliza vyuo vya UDSM,ST.JOSEPH na DIT.

2.AJIRA

Tofauti na matarajio ya wengi ajira na hata field zinahitaji uvumilivu kuliko hata Clinical medicine.Hii ni kutokana kuwa ajira nyingi zinategemea serikali itangaze ajira,kwa hiyo unaweza kumaliza miaka miwili ukisubiri ajira lakini zikitoka uhakika wa kupata ni asilimia 100.Makampuni mengi ya vifaa tiba(MEDICAL EQUIPMENT SUPPLY) kama Anudha,Crown,Kasmedics,Pyramid pharm,Pasific diagnostic,Bio care. e.t.c.Wengi hawa hitaji fresh from school,wengi wamejaza wageni kutoka Kenya na India na hata hivyo hawa hitaji watu wengi unaweza kukuta wanataka watu watatu au wawili wakati wahitimiu ni wengi.Kwa sasa vyuo vinavyo toa kozi za Biomedical Engineering ni vitatu (DIT,MUST na ATC).Hospitali za binafsi nyingi hazi hitaji kabisa Bio medical Technicians baadala yake kifaa kikiharibika huita kampuni husika na kutengeneza na maisha yanasonga.Mpaka sasa Hospitali za binafsi nchi nzima zenye Bio-medical techician/engineers ni Aga khan (DSM) ,TMJ Hospital (DSM) na Regency(DSM) hata hivyo hospitali hizo ni hospitali moja tu ambayo imeajili watanzania katika kitengo hicho.

CHANGAMOTO ZA AJIRA KATIKA KOZI HII

1. Wahitimu asilimia kubwa hawana uwezo wa kutatua changamoto za vifaa tiba kwa usahii ,hii ni kutokana na kukosa mafunzo kwa vitendo kutoka kwenye hospitali kubwa kama MUHIMBILI,BUGANDO ,AGA KHAN NA KCMC.Wahitimu wengi wamekuwa wakisemwa vibaya na waajiri wao na hasa walioko Hospitali za serikakli.,na hivyo utawala wa hospitali hizi hulazimika kutafuta fundi kwenye kampuni wakati wanaye fundi mwajiriwa.

HITIMISHO ;Aira zipo lakini zinahitaji subira ya serikali tu,hii nikutokana kuwa na makampuni ya vifaa tiba machache na hospitali nyingi za private kutokuwa na kitengo hicho.
 
Umenena vyema kiufupi kwa C.O kama ana mpango wa kusoma Mpaka MD aende angalau itabeba japo akaze msuli ila kama hana mpango aachane na hiyo kozi maana kwa sasa C.O hakuna kazi watu wanafanya kazi vijiweni malipo 10k per day.

Sure ,kwa hali ya ajira ya sasa bora hata Clinical officer anaweza kupata kijiwe hata cha 10k kwa siku,kwa kumshikia mtu per shift au kuajiliiwa kabisa.Sasa Bio-medical equipment techinician hata kama serikali haijatangaza ajira ujue hakuna kijiwe kabisa ,njaa mwanzo mwisho
 
Umemaliza kila kitu, tena hiyo Clinical Medicine ajipange, siku hizi Mitihan ya NACTE ni kila mwaka, Kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa tatu, na disco zipo za kutosha.. ila kwa ushauri wangu kama anajiweza apige Clinical Medicine, baadae rahisi kujiendeleza

Ha ha ha Clinical medicine ndiyo kozi ngumu kijiendeleza baada ya kumaliza kwa sababu zifuatazo

1. Kufaulu kwake kunahitaji jitihada za hali ya juu under NACTE exam ,ukumbuke kuna written na clinical exam sasa hata kama uko vizuri hii ya clinical unaweza kukutana na examiner mkuda kutoka Nacte marks anakupa anazo taka.Kwa maana hiyo kupata ufaulu wa GPA 3.5 ni habari nyingine ingawa inawezekana kabisa.

2. Vyuo vya kua upgrade kutoka CO- MD viko vichache kwa sasa ukumbuke vyuo vilivyo kuwa na namba CO kuliko fresh from school (FORM SIX )vilikuwa ni IMTU,KIU na ST.FRANCIS -IFAKARA vyote hivi vimesha kula pin ya TCU vilivyo baki kama MUHAS,CUHAS,UDOM,KCMC vinapendelea idadi nyingi ya form six kuliko CO

3. ADA ,Vyuo ambavyo vina ushindani mdogo na ni rahisi CO kupata vina ada kubwa sana mfano ni HKMU 6M per year,ST JOSEPH 5M ,kumbuka CO uwezo wa kupata mkopo kutoka loans board ni mdogo na kama kwenu hazipo unaweza kuishia njian.

4. Miaka ya kusoma,Wenzetu Kenya,Uganda na Rwanda walianzisha Bachelor of clinical medicine and surgery kwa miaka mitatu(3YRS) kwa mtu aliye maliza Diploma in clinica medicine hii ni kutokana kuwa kuna watu umri wanaona umeenda na miaka sita kwao itakuwa kama kupoteza muda.Tanzania kuna kipindi issue hiyo ililetwa lakini inasemakana MAT walikataa kabisa kitu cha namna hiyo kwa Tanazania.
 
Nimechaguliwa biomedical engineering anayeifahamu naba anieleweshe vizuri ndakuwa nafanya kazi wapi na vipi changamoto ya ajira?
 
Imewahi kujadiliwa humu mara kadhaa. Ukichangamsha macho ukapokea kurasa kadha, bilashaka utaziona threads za Biomedical engineering
 
Back
Top Bottom