Ni kweli, kwa kuwa alikuwa na walinzi wazuri, lakini ikiwa mfungaji anafunga na huko nyuma mabeki na kipa wanaruhusu magoli yaingie inakuwa hakuna maana, mfano Geita gold walitoa mfungaji bora last season lakini waliruhusu kufungwa pia ndiyo maana hawakuweza kutwaa ubingwa hata kama walikuwa na mfungaji bora. Na kitu kingine ikiwa timu ina mfungaji zaidi ya mmoja usitegemee pakatokea na mfungaji bora wa ligi katika timu hiyo.