King Shaat
JF-Expert Member
- Aug 30, 2013
- 863
- 835
Mara nyingi tumekuwa tukitumia hizi kompyuta zetu bila kuzingatia baadhi ya mambo ambayo ni ya muhimu sana. Ishu za kuchukulia hatua ni kama zifuatazo;-
i) Kwa wale watumiaji wa Windows XP na Windows 8.1 (kama huku'uinstall Update 1), mfahamu kuwa Microsoft wameacha ku'support hizi operating system mbili kwa maana ya kutoa Security Updates kila baada ya mwezi kama ilivyo kawaida. Windows XP walikata support tangu April 8 mwaka huu na Windows 8.1 tangu juzi tarehe 13 May.
Bila Security Updates kama kawaida, kompyuta yako itabaki ikitegemea sana Anti-virus program peke yake hivyo kuna baadhi ya ulinzi wa muhimu itakuwa inakosa na kuhatarisha usalama wa mafaili yako katika compyuta na hata usalama wa IDs zako za mtandaoni.
Hivyo basi, hakikisha kuwa una Windows ambayo iko updated kila wakati. Na hii ni rahisi Nenda kwenye Control Panel>System and Security>Windows Updates> Hapo utaweza kuangalia kama kuna updates za muhimu ili kuzi'download na kuzi'install.
ii). Ili kuhakikisha maisha marefu kwa betri ya kompyuta yako zingatia haya;-
- Si lazima utumie umeme wakati betri iko full. Mara nyingi betri unakuta ziko full lakini bado mtu ana'plug in umeme. Kwa namna hii betri itapoteza nguvu mapema.
- Chaji full charge mara moja kwa mwezi. Kama betri yako ni nzima kabisa au bado mpya, basi unaweza kutumia kompyuta yako bila umeme wa soketi mpaka betri ikifikia 49% ndo uichaji. Hii itasaidia betri kuwa na maisha marefu.
-Kama unatumia kompyuta yako kwa matumizi yatakayotumia muda mrefu au kucheza gemu, basi ondoa kabisa betri na utumie tu umeme wa moja kwa moja.
Tupeane maujanja bandugu!.
i) Kwa wale watumiaji wa Windows XP na Windows 8.1 (kama huku'uinstall Update 1), mfahamu kuwa Microsoft wameacha ku'support hizi operating system mbili kwa maana ya kutoa Security Updates kila baada ya mwezi kama ilivyo kawaida. Windows XP walikata support tangu April 8 mwaka huu na Windows 8.1 tangu juzi tarehe 13 May.
Bila Security Updates kama kawaida, kompyuta yako itabaki ikitegemea sana Anti-virus program peke yake hivyo kuna baadhi ya ulinzi wa muhimu itakuwa inakosa na kuhatarisha usalama wa mafaili yako katika compyuta na hata usalama wa IDs zako za mtandaoni.
Hivyo basi, hakikisha kuwa una Windows ambayo iko updated kila wakati. Na hii ni rahisi Nenda kwenye Control Panel>System and Security>Windows Updates> Hapo utaweza kuangalia kama kuna updates za muhimu ili kuzi'download na kuzi'install.
ii). Ili kuhakikisha maisha marefu kwa betri ya kompyuta yako zingatia haya;-
- Si lazima utumie umeme wakati betri iko full. Mara nyingi betri unakuta ziko full lakini bado mtu ana'plug in umeme. Kwa namna hii betri itapoteza nguvu mapema.
- Chaji full charge mara moja kwa mwezi. Kama betri yako ni nzima kabisa au bado mpya, basi unaweza kutumia kompyuta yako bila umeme wa soketi mpaka betri ikifikia 49% ndo uichaji. Hii itasaidia betri kuwa na maisha marefu.
-Kama unatumia kompyuta yako kwa matumizi yatakayotumia muda mrefu au kucheza gemu, basi ondoa kabisa betri na utumie tu umeme wa moja kwa moja.
Tupeane maujanja bandugu!.