Chereko chereko na freestyle

mkorinto

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2014
Posts
32,066
Reaction score
39,512
Ndugu zangu members wa JF mnaopenda kufurahia siku muhimu katika maisha yenu, Harusi kuna kipindi mahsusi kwa shughuli hio TBC1 kila Jumapili saa moja kamili usiku. Kuna matangazo ya bidhaa ya kike (freestyle) nadhani ni wadhamini wa kipindi hicho.

Tatizo langu sio kubwa, ila ni namna wao Chereko Chereko wanavyomtangaza huyo mdhamini wao. Ni kwa kumhoji bibi harusi au msimamizi kwamba amekuwa akitumia nini katika maisha yake, inabidi aseme ni freestyle, tena inabidi aseme kabisa kuwa amevaa wakati huo wa shughuli hiyo, jamani! Hili si ni mambo ya siri, Au!?

Kwahiyo watazamaji wote tujue sasa kuwa bibi harusi yuko kwenye unajimu siku hiyo dah! imekaa kiudhalilishaji hii.
Ndio tatizo langu tu.

Natumai mmo humu.
 
Hivi km bibi harusi yupo kwny zile siku mhimu za kuvaa freestyle siku ya harusi yake huwa kunakuwa na honeymoon tena hapo?
 
Hivi km bibi harusi yupo kwny zile siku mhimu za kuvaa freestyle siku ya harusi yake huwa kunakuwa na honeymoon tena hapo?

Ndio hapo huwa najiuliza maswali lukuki baada ya wao kunionyesha bibi harusi aliyevaa freestyle.
 
Hivi km bibi harusi yupo kwny zile siku mhimu za kuvaa freestyle siku ya harusi yake huwa kunakuwa na honeymoon tena hapo?
kwani honeymoon lazima kugongana, mshagongana mara ngapi kwa hiyo miaka mitano mkiwa wachumba, mpaka demu alikuwa anakuja kwako week end na kulala mpaka monday morning, na wengine mlikuwa mnaishi pamoja kwa mwaka,ikibaki mwezi mmoja kabla ya harusi ndo anahamia kwa shangazi eti kufundwa. ndoa zamani bwana. Wewe kwenye chereko ushaona marangapi harusi za mabinti? asilimia sabini wanaoolewa ni above 30yrs na asilimia siti wanamimba.
 
Ndio hapo huwa najiuliza maswali lukuki baada ya wao kunionyesha bibi harusi aliyevaa freestyle.

Jamani zile zinavaliwa kama kinga tuu...Bi harusi anaweza kupata mshtuko mambo yakaharibika...Shela jeupe lile...

Au furaha kupita kiasi ya Siku ile inaweza haribu mamboo...lazima ajiandae mapema...
 
Jamani zile zinavaliwa kama kinga tuu...Bi harusi anaweza kupata mshtuko mambo yakaharibika...Shela jeupe lile...

Au furaha kupita kiasi ya Siku ile inaweza haribu mamboo...lazima ajiandae mapema...


Ahaa kumbe anaweza akavaa huku hayupo angani.

Tatizo sisi watazamaji kujua kuwa huyu kim nana tunayemuangalia katupia.kiasi flani inaondoa uhuru au vip?
 
Ahaa kumbe anaweza akavaa huku hayupo angani.

Tatizo sisi watazamaji kujua kuwa huyu kim nana tunayemuangalia katupia.kiasi flani inaondoa uhuru au vip?

Yeah inaondoa Uhuru na navyojua tukiwa wasichana tulikuwa tunaambiwa tuhakikishe MTU yoyote hajui..hata kaka zako...

Sasa hii ya kujitangaza mbele ya kadamnasi ni habari nyingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…