Hakuna ukabila namfahamu Fred Mwanjala ,alipoingia pale Channel 10 ilikuwa inatangaza tu Dar miaka ya 99 kama sijakosea ,tena alipelekwa pale na dada mmoja wa mtaani kwake na alijiunga na Channel kwa ngazi ya chini sana alikuwa anamsaidia Ngonyani kwenye sehemu za mitambo,kidogokidogo baada ya kuzoea mazingira ndio akaanza kujifunza utangazaji kwa kuibia kwa kuwafuata watangazaji waliokuwepo,nadhani Ngonyani ndie kamsaidia sana Fred kufika hapo alipo na ujue wakati ule Channel ten ilikuwa chini ya wahindi na yule mtaliano,hawa wengine wamepata kazi kwa juhudi zao,viongozi wa Channel 10 ni wahindi,sasa hao wahindi watawapendelaje Wanyakyusa,mbona sehemu nyingi utakuta sehemu moja au idara moja kuna watu wa kabila moja hata sita,je napo utasema kuna ukabila.Wenye mawazo hasi hupenda kuangalia vitu hasi,pole