Challenge time na magical power

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,455
Reaction score
6,465
ZAWADI: Kaka Magical Power, naomba ushauri tafadhali, usinipuuze πŸ™

MAGICAL POWER: Sawa, sema dada. Upo salama?

ZAWADI: Sina amani kabisa. Mume wangu wa ndoa miezi mitatu, amebadilika ghafla. Hana mapenzi tena, hanigusi, halali nyumbani. Kila nikimuuliza anasema niko busy, mara kazini, mara kanisani.

MAGICAL POWER: Ulianza kuona mabadiliko lini?

ZAWADI: Ni kama wiki tatu sasa. Jana nimefuatilia kwa siri, nikagundua anaishi na mwanamke mwingine nyumba ya kupanga maeneo ya Kimara. Wamepanga kama wachumba, hadi wanashea vyombo vya ndani.

MAGICAL POWER: Subiri kidogo... Mume wako wa ndoa miezi mitatu?? 😳

ZAWADI: Ndio kaka, yaani tulivyofunga ndoa aliniahidi kila kitu. Nikauza biashara yangu nikahamia kwake. Sasa hata pesa ya matumizi hanipi. Napoishi nimebakia mtumishi asiye na mshahara wala heshima.

MAGICAL POWER: Sasa dada, unahitaji msaada wa nini? Maana hapo kuna mambo matatu: kiburi, uongo na usaliti wa kiwango cha juu.

ZAWADI: Nataka kujua, niendelee kuvumilia nikiamini ni mapito ya ndoa au nichukue hatua? Maana wazazi wangu hawajui kinachoendelea, bado wanamwona kama malaika.

MAGICAL POWER: Hapana dada, unateswa kimya kimya huku watu wakikushangilia. Hii si ndoa, ni mtego wa mateso. Uvumilivu usikufanye uendelee kuliwa maisha yako yote. Wape wazazi ukweli. Kama mwanaume hana heshima ya ndoa, basi si wa ndoa.

ZAWADI: Aisee… umenifungua akili. Nilihitaji kusikia haya. Ahsante kaka Magical Power.

MAGICAL POWER: Karibu sana. Kumbuka, usijifiche kwenye kivuli cha ndoa hadi ubaki kivuli cha mwanamke.
 
KUNANI; Magical Power habari yako, nimekuwa nakufuatilia kwa muda mrefu na mimi leo naomba unifanyie challenge kwa mume wangu amtaje huyo mwanamke mwingine nipate kaondoka nimechoka. Leo hii anatimiza wiki hayupo nyumbani, watu wananiambia wanamuona Sinza huko anaishi kwa mwanamke mwingine amefungiwa ndani huko sijui wanasema ni Jike Shupa kamfungia ama rafiki wa Jike shupa mimi sijui ila naumia.

MAGICAL POWER; Jike Shupa gani? Huyuhuyu wa nipeleke kwa Mganga nikasake wanga au?

KUNANI; Ndio ila sina uhakika mimi, nisaidie tu kumfanyia challenge ataje mwanamke anayempenda walau nipate ushahidi nikawaonyeshe nyumbani kwa sababu kwa wazazi wangu anajifanya mtakatifu, nikiwaeleza kwamba nateseka hata hawanielewi.

MAGICAL POWER; Pole sana, nipe mawasiliano yake na jina lake.

KUNANI; 07......... Anaitwa MUSTAPHA.

MAGICAL POWER; Haya sawa nakurejea.

πŸ”΄πŸ”΄πŸ”΄πŸ”΄

MAGICAL POWER; Habari kaka

MUSTAPHA; Safi, kwema?

MAGICAL POWER; Kwema, vipi umelala nini? Mbona sauti ipo chini sana au unaumwa?

MUSTAPHA; Nimelala tu, karibu

MAGICAL POWER; Asante, vipi tunaweza kuongea japo dakika mbili? (Hapo nikasikia kohozi la mwanamke akikohoa kwa uchovu pembeni yake)

MUSTAPHA; Sawa niambie

MAGICAL POWER; Asante kwa nafasi, bwana mimi naitwa Magical Power ni mshauri wa mahusiano na maisha, nimekutafuta kwa sababu kama dakika kadhaa zilizopita kuna mwanamke kanipigia simu ambaye amejitambulisha kama mpenzi wako...

MUSTAPHA; Sikia kaka sikiaaaa, tutaongea baadae nimechoka sana sasa hivi naumwa ile mbayaaaa siwezi hata kushika simu.

MAGICAL POWER; Iyeee!! wewe tena 😳 lakini nimekuuliza kama una muda umesema unao, shida nini zaidi?

CHEPUKO; Honey!! pokea simu hiyooo

MUSTAPHA; Achana nae huyu mzinguaji tuuu

CHEPUKO; Pokea simu nakwambiaaa nimesikia kila kitu

MUSTAPHA; Achana nae bwanaaa!! We mbona unapenda kuanzisha ugomvi usio na maana!!! Huyu si ni mwanaume sasa unataka usikie nini!!

CHEPUKO; Ni mwanaume ndio ila nimesikia anasema ametumwa na mpenzi wako, huyo kaka yupo siriasi kabisa wala sio chizi mpaka akufate wewe, pokea simuuuu honey!!

MUSTAPHA; Sipokei sasa fanya unachotaka

CHEPUKO; Pokeaaa

MUSTAPHA; Sipokeiii

CHEPUKO; Pokeaaaaa nakwambia

MUSTAPHA; Baby come down please πŸ™ 😩 😫 😭

CHEPUKO; Toka ndani kwangu tokaa!!! gerautiiiii

MAGICAL POWER; Jamani mgombane taratibu eeeh!!!

CHEPUKO; Nani amekutuma kaka niambie

MAGICAL POWER; Kuna mwanamke yuko Nzega huyo bwana kampa ujauzito sasa amefika Dar anampigia simu hapokei, ndio kanituma hapa nimpigie akampokee Ubungo. Alafu huyo bwana ana mke au wewe ndiye mke wake? Maana kwa maelezo ya huyu mchepuko wa Nzega anasema anajua kama huyo MUSTAPHA ni mume wa mtu lakini anachotaka yeye ni ujauzito kulelewa na amuoe ampangie chumba.

CHEPUKO; Anyiiiiiiii 😭😭😭😫 anyiiii😭 anyiiiii 😭 leo ndio mwanzo na mwisho kuja hapa nyumbani!!!! Una mke? Nakuuliza una mke?

MUSTAPHA; Sina mke bwana huyo anakudanganya hata simjui.

MAGICAL POWER; Mimi naenda zangu jamani, tulikuwepo πŸšΆβ€β™‚οΈπŸšΆβ€β™‚οΈ

πŸ”΄πŸ”΄πŸ”΄

MAGICAL POWER; Uko wapi sasa hivi?

KUNANI; Najiandaa nikaoge, umeongea nae?

MAGICAL POWER; Ndio, lakini nimekutana na kitu sio kizuri, sijui mapokeo yako yatakuwaje na binafsi nisingependa kukutumia ukiwa mwenyewe.

KUNANI; We nieleze tuuu nina watoto hapa

MAGICAL POWER; Nataka mtu mzima sio watoto

KUNANI; Sawa, ngoja nimuite rafiki yangu aje, ila si nitakuwa natoa siri za familia Magical Power.

MAGICAL POWER; Hilo nalo neno, watu hawaaminiki, nakutumia ila uwe ngangali na itafutika baada ya kumaliza kuisikiliza sitamani ukae nayo.

KUNANI; Magical Power mimi nataka kuondoka hapa nimechoka, nimelipia ili nipate ushahidi, mimi huenda nipo siriasi kuliko watu wote waliokuja kufanya challenge kwako, hii challenge kwangu ni muhimu kupita maelezo, ni muhimu mnooo. Naweza sema ni Mungu ameamua kusikia maombi yanguuuu ninayomuomba kila siku.

KUNANI; Sawa hamna shida, nakutumia.

KUNANI; Sawa baba.

πŸ”΄ BAADA YA KUSIKILIZA VOICE WHATSAPP πŸ‘‡πŸ»

KUNANI; Ashukuriwe Mungu wa Majeshi, asante sana Magical Power, huyu ni Mungu ameamua kujibu ombi langu, nimemuomba nimelia sana, naomba usiifute kwa sababu anaweza kuja kukagua simu yangu akikutana nayo atanipiga ataifuta nitakosa ushahidi. Ila wanaume!! sasa kwanini ananizuia kuondoka na ananifanyia hiviii!!!? 😞 ila asante sana, huu ni ushindi kwangu.

MAGICAL POWER; Pole sana, utanipa mrejesho kwa kitakachotokea baada ya hapa, ila naomba uwe ngangali usiumizwe na hiyo voice.

KUNANI; Sawa kaka nashukuru.

MAGICAL POWER; Haya asante. Bye
πŸ‘‹
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…