Maoni yako yanafanana na maoni yangu niliyochangia katika ile forum, mchango wangu ulikuwa hivi:
Mimi nafikiri pia mazingira tunayoishi sasa hivi yanachangia wanaume kutowapa wake zao chakula cha usiku vile ipasavyo. Zamani ilikuwa ni nadra sana kukuta mwanamke akionyesha baadhi ya maungo yake (sehemu za mwili wake). Lakini sasa hivi (wakati huu tulionao) imekuwa ni mtindo kwa wanawake kuonyesha sehemu za miili yao, wenyewe wanasema wanakwenda na wakati. Hivyo mchana kutwa mwanamume
anashinda akitazama nyuchi (sehemu za wanawake zinazoachwa wazi), iwe ofisin au njiani. Hali hii inamfanya mwanamume huyu kupoteza hamu ya kutoa chakula cha usiku kwa mkewe pindi arudipo nyumbani kwani hamu inakuwa imekwisha kwa kutazama maungo ya wanawake huko njiani. Mwanamume asipozoea kuonaona maungo ya mwanamke anakuwa na hamu ya kutoa chakula cha usiku kwa mkewe.