Mkubwa joshydama kweli hili hata tukisema tulaumiane haitasaidia sana. Ni kuwashawishi wenzetu kukubaliana na ukweli kuwa tunapoteza pesa kwenye mambo ambayo hayana tija.
Pesa za uchaguzi zikijenga shule moja ya kisasa ni bora sana. Tunaweza kulaumu Katiba, lakini siamini kama ikibadilika itabadilisha jambo hili.
Mtoa mada umesahau kitu kimoja! Kama tuamua kuacha kufanya uchaguzi huo, basi CCM watajisahau na kuweka mtu wao yeyote ambaye hatahitaji kuwajibika saana kwa hao wananchi! Na hii italeta vurugu nyingine ya kupachina maajina ya watu hata wasiotosheleza kubeba majukumu hayo. Ilivyo sasa japokuwa % kubwa ushindi unaelekea kwa CCM, CCm wanavyanye 'veting' ya kutosha ili yule wanayepleka kwa wananchi awe na kukubalika kwao. Kwani kama watapeleka tu yyeyote, kazi inaweza kuwa ngumu sana kupata ushindi kwa CCM! Hivyo chakuzi ndogo kwa muktaza huu haziepukiki!Kwanza kwa unyenyekevu mkubwa naomba msinielewe vibaya kwa kuanza na kichwa chenye ukakasi kiasi, nikaonekana natumia lugha mbaya.Ujinga ni hali ambayo inaweza kuondolewa kwa kuelimishwa, so it is not a permanent condition na isieleweke kuwa ni tusi.
Nimekuwa naangalia chaguzi ndogo kwa jicho la pili, na kujaribu kuwa realists na sio idealist. Nimefanya hivi kwa kuangalia gharama na manufaa yake, na kufikia hitimisho kuwa hizi changuzi ni kama mtindo fulani wa kutwisha mzigo wavuja jasho kuwanufaisha wanasiasa, na kuwafurahisha wahisani na jumuiya ya nchi za magharibi. Yaani ni kama tunalipia bili ya mtu ambaye anajiburudisha kwa mchezo wa kisiasa.
Kwanza nimejiuliza: Kwanini kila uchaguzi mdogo unapotokea, fedha za kuugharamia hazijawahi kukosekana? Kila ukisikia uchaguzi mdogo katika jimbo fulani, fedha zinakuwa tele. Lakini kwenye majimbo hayo hayo ya uchaguzi, unaweza kusikia fedha ambazo ni pungufu ya zile zinazotumika kugharamia uchaguzi, zinakosekena kwenye miradi kama ya ujenzi wa zahanati, madaraja, barabara, umeme, maji, shule etc …
Najiuliza kama ni kweli huwa zinakosekana au si kweli, au hali halisi ni kuwa mambo hayo yanayowagusa wananchi sio kipaumbele kama ilivyo kwa mambo ya siasa. Inawezekana sina busara za kutosha kujua hekima iliyomo ndani ya jambo hili. But I do believe we can find our own formular which can be acceptable to vyama vyote bila kufuja hela kwenye bi-elections ambazo kimsingi hazibadilishi mwelekeo wa bunge.
Pili, kwa mtu mwenye akili timamu kwa sasa atajua kabisa kuwa chaguzi ndogo zote iwe kwa Nassari, kwa Lissu au kwingine kokote, mshindi atakuwa mgombea wa CCM. Matokeo yatakuwa hiyo… kama kuna mtu atabisha basi aseme… lakini swali langu ni kuwa kwa nini tutumie mapesa mengi kwenye kufanya kitu ambacho tayari matokeo yake tunayajua? Kwanini tuzitumie akili na busara ya kutafuta njia ya kuweka mtu wa CCM, halafu pesa zote hizo tutumie kwenye jambo la kijamii litakalowanufaisha wanajimbo wote kwa muda mrefu? Au ni kwamba tunafanya mizungu kuwafurahisha wazungu wakati tunaoumia ni walipa kodi? Ninachokiona ni kuwa chaguzi hizo hazifanywi kwa ajili ya wanajimbo, au kwa ajili ya Tanzania, ni chaguzi kwa ajili ya kufurahisha nchi za magharibi, lakini kwa gharama zetu. Kweli inauma sana.
Tatu, tukiangalia mbali zaidi…in realistic terms … 2020 mshindi atakuwa mgombea wa CCM kwenye kiti cha urais, labda Bunge litakuwa asilimia 90 CCM, asilimia 10 upinzani, more or less. Tujaribu kuangalia pesa zitakazotumika kwenye jambo hili ambalo tayari kimsingi liko wazi. Swali ni je, ina maana tumeshindwa kutafuta njia zetu wenyewe watanzania za gharama nafuu kufanikisha hilo? Hela ambazo zinagharamia uchaguzi zingeenda kwenye maendeleo ya jamii, naamini ingekuwa ni matumizi mazuri ya fedha kwa manufaa ya muda mrefu.
Mwanzo kabisa nimejitaja kuwa mimi ni realist na sio idealist. Kwa hiyo niseme wazi tu kuwa demokrasia ya uchaguzi hapa Tanzania naiona kama ni mizungu kwa ajili ya wazungu. Ni bora tufute ujinga, na hizo pesa tunazopeleka kwenye uchaguzi zitumike kwenye maendeleo kwenye majimbo. Bora mizungu kwa ajili ya maendeleo yetu, kuliko kwa wazungu.
Mkubwa joshydama kweli hili hata tukisema tulaumiane haitasaidia sana. Ni kuwashawishi wenzetu kukubaliana na ukweli kuwa tunapoteza pesa kwenye mambo ambayo hayana tija.
Pesa za uchaguzi zikijenga shule moja ya kisasa ni bora sana. Tunaweza kulaumu Katiba, lakini siamini kama ikibadilika itabadilisha jambo hili.
Mkuu maarifa gani unazungumzia na yanapatikana vipi? Hivi viongozi wa institutions za serikali kuside na chama badala ya nchi inatokana na kukosa maarifa kweli au ni upumbuvu wa kuzaliwa nao,sasa Kama mtu anaweza kusoma mpaka kiwango cha master degree,akapanda cheo mpaka kufikia level ya CDF au IGP na still akawa hana maarifa ya kumuwezesha kujua nani amtumikie kati ya nchi na watu wake au aliyemteua na chama chake basi tunatatizo kubwa kama taifaMkuu ni kwamba upumbavu ni zao la kutokuwa na maarifa. Maarifa yanakusaidia ujitambue kwa kiasi kikubwa sana. Ukikiosa maarifa hakika ndipo suala la ujinga na upumbavu huwa linakuja. Pindi utakapokuwa mjinga/mpumbavu hakika utashindwa kuhoji hata pale unapoona mambo hayaendi sawa kwa sababu ujinga na upumbuvu huambatana na uoga.
Ni vigumu sana ndugu yangu, watu wanatamani mno lakini mazingira ni magumu sana; CCM inalijua hili hivyo inahakikisha kila sehemu wameweka makada wao kuanzia vyombo vya usalama, wakuu wa mikoa na wilaya, Wakurugenzi wa local government pia ni makada watiifu...na kwenda mbali zaidi wamepandikiza hadi vyama vya upinzani vinavyo riport kwao..Kwani hatuwezi kutafuta utaratibu mwingine wa kuchagua viongozi, ambao hauhusishi vyama vya siasa? kama CCM ni tatizo, tukumbuke kuwa ni chama cha siasa, kikija kingine nacho kitakuwa tatizo...itakuwa ni kurudi pale pale.
Mkuu tatizo lote liko ndani ya katiba. Kwenye katiba ambayo rais hashitakiwi kwa kosa lolote akiwa madarakani, kwa vyovyote amri yake inakuwa na nguvu kuliko katiba. Katiba yetu inatoa nguvu kubwa isiyo na msingi kwa rais, ikitegemea rais atakuwa na busara. Hizi chaguzi na matokeo unayoyaona sasa ni matokeo ya nguvu isiyo na sababu ya rais.
Matokeo haya unayosema kiunyonge kwamba ccm inashinda na ni matokeo yanayojulikana ujue huko ni kuidhinisha dhuluma. Je unajua madhara ya kubariki dhuluma? Unadhani hiki anachokifanya rais huyu kisa ana mamlaka kinapaswa kupewa baraka za maneno ya kupotosha kwa kusema tunawaridhisha wazungu? Nimefedheheka kuona mtu muelewa kama ww unaongea kuhalilisha haramu kisa mshindi anafahamika, huku ukijua fika sio mshindi anayepatikana kihalali.
Mkuu baada ya uchaguzi tukifanya cost benefit analysis utakuja kujua kuwa i am more realaistic. Ni bora kuwe na njia ya sisi kunufaika na hizo hela, kuliko kuwanufaisha wanasiasa.
wazo lako bayaCheap is expensive yes, but new is even more expensive. Ukweli ni kuwa ni hatari kuwanyima watu haki ya kuchagua kiongozi wanayemtaka.
Lakini kama kiongozi atakayechaguliwa tayari tunamfahamu, kwanini asisimikwe tu, na hizo hela tutumie kwenye mengine kama maji, dawa, barabara ... ?
Kwa mfano huo uchaguzi usipofanyika una uhakika gani kuwa hizo pesa zitaelekezwa kwenye kwenye miradi?Mkuu baada ya uchaguzi tukifanya cost benefit analysis utakuja kujua kuwa i am more realaistic. Ni bora kuwe na njia ya sisi kunufaika na hizo hela, kuliko kuwanufaisha wanasiasa.
cyo ramli, wala ramli chonganishi, mtoa mada anaongea fact. Ni ufujaji wa hela za mlipa kodi, chama kitakachotoa washindi ni cha muunganiko wa TANU na ASP.ikiwa akili ya Mtanzania inaanza kujadili ushindi wa ccm kabla ya chaguzi kufanyika, tukiri tu tumefikia hatua mbaya sana, kwamba mtu anatoa hadi asilimia ya ushindi kumpa huyu na asilimia ya kushindwa kumpa yule!!!! halafu anatetea yeye ni m realistic kweli!!!! Naamini kabisa kauli ya kiongozi mmoja wa dini kuwa Watanzania walio wengi sasa tumebaki kupiga ramli tu, Tupo hatarini sana.
Umeeleza kwa ufupi lakini hukuacha kitu, mwenye akili na atambue. Umefunga mjadala.Tabia ya watanzania kuwa makondoo ni mifumo ya maisha inayowalea kuanzia kwenye familia hadi shuleni.
Mtoto anakulia katika mazingira ya kumjaza uoga hadi anakuwa mtu mzima ni mtu hasiyejiamini.
Ili kuweza kubadili huu ujinga wa watanzania wengi ni lazima mabadiliko yaanzie ngazi ya familia. Demokrasia ya kweli ianzie kwenye familia zetu.
SWALA LA UCHAGUZI LITABAKI PALE PALE EITHER LIWE LA KIMIZENGWE AU NAMNA SAHIHI. CHAGUZI NI SWALA LA KIDEMOKRASIA KWA JAMII INAYOAMINI USHIRIKI WA MWANANCHI KUCHAGUA KIONGOZI MWAKILISHI AU YEYE BINAFSI KUPATA FURSA YA KUWAKILISHA JAMII YAKE KWAHIYO KUFUTWA AU UCHAGUZI USIFANYIKE NI KISOCHOINGIA AKILINI KWANI TAIFA LETU SIO LA KIFALME/UMALKIA, TUNAONGOZWA NA KATIBA NA SHERIA ZINAZOLINDA UHURU WETU.Kwanza kwa unyenyekevu mkubwa naomba msinielewe vibaya kwa kuanza na kichwa chenye ukakasi kiasi, nikaonekana natumia lugha mbaya.Ujinga ni hali ambayo inaweza kuondolewa kwa kuelimishwa, so it is not a permanent condition na isieleweke kuwa ni tusi.
Nimekuwa naangalia chaguzi ndogo kwa jicho la pili, na kujaribu kuwa realists na sio idealist. Nimefanya hivi kwa kuangalia gharama na manufaa yake, na kufikia hitimisho kuwa hizi changuzi ni kama mtindo fulani wa kutwisha mzigo wavuja jasho kuwanufaisha wanasiasa, na kuwafurahisha wahisani na jumuiya ya nchi za magharibi. Yaani ni kama tunalipia bili ya mtu ambaye anajiburudisha kwa mchezo wa kisiasa.
Kwanza nimejiuliza: Kwanini kila uchaguzi mdogo unapotokea, fedha za kuugharamia hazijawahi kukosekana? Kila ukisikia uchaguzi mdogo katika jimbo fulani, fedha zinakuwa tele. Lakini kwenye majimbo hayo hayo ya uchaguzi, unaweza kusikia fedha ambazo ni pungufu ya zile zinazotumika kugharamia uchaguzi, zinakosekena kwenye miradi kama ya ujenzi wa zahanati, madaraja, barabara, umeme, maji, shule etc …
Najiuliza kama ni kweli huwa zinakosekana au si kweli, au hali halisi ni kuwa mambo hayo yanayowagusa wananchi sio kipaumbele kama ilivyo kwa mambo ya siasa. Inawezekana sina busara za kutosha kujua hekima iliyomo ndani ya jambo hili. But I do believe we can find our own formular which can be acceptable to vyama vyote bila kufuja hela kwenye bi-elections ambazo kimsingi hazibadilishi mwelekeo wa bunge.
Pili, kwa mtu mwenye akili timamu kwa sasa atajua kabisa kuwa chaguzi ndogo zote iwe kwa Nassari, kwa Lissu au kwingine kokote, mshindi atakuwa mgombea wa CCM. Matokeo yatakuwa hiyo… kama kuna mtu atabisha basi aseme… lakini swali langu ni kuwa kwa nini tutumie mapesa mengi kwenye kufanya kitu ambacho tayari matokeo yake tunayajua? Kwanini tuzitumie akili na busara ya kutafuta njia ya kuweka mtu wa CCM, halafu pesa zote hizo tutumie kwenye jambo la kijamii litakalowanufaisha wanajimbo wote kwa muda mrefu? Au ni kwamba tunafanya mizungu kuwafurahisha wazungu wakati tunaoumia ni walipa kodi? Ninachokiona ni kuwa chaguzi hizo hazifanywi kwa ajili ya wanajimbo, au kwa ajili ya Tanzania, ni chaguzi kwa ajili ya kufurahisha nchi za magharibi, lakini kwa gharama zetu. Kweli inauma sana.
Tatu, tukiangalia mbali zaidi…in realistic terms … 2020 mshindi atakuwa mgombea wa CCM kwenye kiti cha urais, labda Bunge litakuwa asilimia 90 CCM, asilimia 10 upinzani, more or less. Tujaribu kuangalia pesa zitakazotumika kwenye jambo hili ambalo tayari kimsingi liko wazi. Swali ni je, ina maana tumeshindwa kutafuta njia zetu wenyewe watanzania za gharama nafuu kufanikisha hilo? Hela ambazo zinagharamia uchaguzi zingeenda kwenye maendeleo ya jamii, naamini ingekuwa ni matumizi mazuri ya fedha kwa manufaa ya muda mrefu.
Mwanzo kabisa nimejitaja kuwa mimi ni realist na sio idealist. Kwa hiyo niseme wazi tu kuwa demokrasia ya uchaguzi hapa Tanzania naiona kama ni mizungu kwa ajili ya wazungu. Ni bora tufute ujinga, na hizo pesa tunazopeleka kwenye uchaguzi zitumike kwenye maendeleo kwenye majimbo. Bora mizungu kwa ajili ya maendeleo yetu, kuliko kwa wazungu.
Mkuu hapo TU ndipo ambapo waafrica tunazingua kwenye kukariri kuwa demokrasia Ni uchaguzi TU(Tena kwenye nafasi za uongozi wasiasa)...SWALA LA UCHAGUZI LITABAKI PALE PALE EITHER LIWE LA KIMIZENGWE AU NAMNA SAHIHI. CHAGUZI NI SWALA LA KIDEMOKRASIA KWA JAMII INAYOAMINI USHIRIKI WA MWANANCHI KUCHAGUA KIONGOZI MWAKILISHI AU YEYE BINAFSI KUPATA FURSA YA KUWAKILISHA JAMII YAKE KWAHIYO KUFUTWA AU UCHAGUZI USIFANYIKE NI KISOCHOINGIA AKILINI KWANI TAIFA LETU SIO LA KIFALME/UMALKIA, TUNAONGOZWA NA KATIBA NA SHERIA ZINAZOLINDA UHURU WETU.