Mzee Mwanakijiji ingekuwa vema sana ungemshauri @Nnauye Jr aache matusi anayomtukana Dr Slaa.Kwa matusi anayomtukana Dr Slaa sishangai watu kuchimba familia ya Nape na kuona kama amefundishwa yale maadili ya kiafrika.
Haiwezekani kwa kijana mdogo kama huyu kumtukana matusi mtu wa rika la Dr Slaa.Ni lazima mtu wa aina hiyo awe ameathirika kisaikolojia.
Hata Obama kuna watu walimshuku kama kazaliwa Marekani, kuna wengine walimshuku kuwa ni muislam na wengine walijadili kuwa ana mtoto wa nje ya ndoa.
Ukishakuwa public figure lazima tukujadili tu hata uwe nani. Tatizo la wabongo ni kwamba akijadiliwa Dr Slaa na mchumba wake Josephine mnaona sio siasa. Akijadiliwa Nape kuwa amtafute baba yake mnasema haitakiwi. Kila mtu ambaye ni public figure lazima tumjadili hata kama wengine hamtaki
ukiona adui yako anaoga kwenye maji machafu na wewe unaingia kuoga ili umkomoe au ili angalau ufanane naye!... "mbona wote tuko wachafu" ndilo jibu?
Yawezekana mwaka huo wa kumbukumbu Nape alikuwa bado hajazaliwa!!! JF kwa upekenyuzi bwana!
Sawasawa kabisa. CCM wakitukana ni sawa, ila CDM ikisema ukweli tatizo? ama kweli watz waoga wa kusema ukweli. Amelianzisha alinywe
Kwa NAPE mambo ya familia yake ni sawa yajadiliwe lakini kwa babu enu SLAA ya kuiba mke na kujikopesha ni personal hayatakiwi kujadiliwa.CHADEMA mmeisha kwakweli.mwaka wenu huu hamna pakutokea!
Mtu mzima haitahiji kushauriwa; mambo mengine mtu unafunzwa na maisha na ulimwengu na hekima. Nape ni mtu mzima.
CDM nilikuwa nawaamini ila kwa hili mmenisikitisha. Hivi watu na akili zenu mnawaita waandishi wa habari na kutoa pumba hivi. Hoja ilikuwa ni kutujulisha kwa nini CDM haitakufa basi na siyo haya mambo ya kihuni yalio na ushahidi mwepesi. Hili mmechemka na ili mrudishe heshima yenu muombeni Nape radhi. Chizi kachukua nguo zenu nyie mkatoka barabarani mnamkimbiza sasa sisi tutawaoneje??????????
CCM wakiruka kwenye genge na CDM waruke ili wote wawe sawa!?
Hayo unayosema ni sawa na yule mwizi aliyejipaka kinyesi ili asikamatwe ................... kama akingia huko kwenye maji machafu basi inabidi umfuate na ummalizie hukohuko!!
can we focus on issue at hand and burry this 'mipasho politics'. show the people why CDM haifi. Tujibu hoja za msingi.period.
Sasa kwenye hili Nape kafanyanini?? hahusiki na hawezi kubadilisha ni tofauti na hiyo mifano yakoMKJJ,
Siasa za maji taka zimeanzishwa na CCM....................... sasa kama swala la Slaa kuacha upadri ni issue, kuwa na mchumba ni issue kwa nini hili lisiwe issue?? Watanzania wanapenda mipasho kwa hiyo wape mipasho!! Ndiyo maana CCM wanazunguka na taarabu nchi nzima wakati wa kapeni!!
Kuna tofauti, CCM wanaruka kwenye genge la uongo, CDM wanarukia genge la ukweli ili kuwakomboa watanzania kutokana na genge la wanaotengeneza uongo.
Chadema mmeishapotezwa mmelazimishwa kucheza siasa za udaku na nyie mmekubali.
Sasa kwenye hili Nape kafanyanini?? hahusiki na hawezi kubadilisha ni tofauti na hiyo mifano yako