CHADEMA YA SASA SIYO ILE YA ZAMANI

gwamaka aswile

Senior Member
Mar 26, 2015
186
106
CHADEMA YA SASA SIYO ILE YA ZAMANI
Ni muhimu kuanzia mbali mahala fulani. Twaweza kuanzia kuiangalia CHADEMA kabla ya michakato ya uchaguzi. Jinsi ilivyokuwa ikipambana na ufisadi. Tukaifuatilia CHADEMA wakati wa uchaguzi na hasa mchakato wa kumpata mgombea urais.
Hapo tukaona jinsi CHADEMA ilipomtosa mtu aliyetarajiwa na wengi kugombea urais na kumzoa a;liyekuwa anatuhumiwa kuongoza ufisadi. Hapo kuna daraja ambalo CHADEMA au ng'ambo ile siyo CHADEMA ya ng'ambo hii.
Uchaguzi umemalizika Serikali imeingia madarakani. Nguvu ya kupinga matokeo ilikuwa ndogo. Sijui kama anajua kwa nini ni ndogo. 2010 kila kona matokeo ya uchaguzi ya Rais yalinung'unikiwa. Kwa sasa siyo. Wenye akili walielewa.
Kama ndivyo tukianzia CHADEMA YA toka kukatisha daraja na kauli za mbowe tunajiuliza swali: Toka kukatisha daraja nililolieleza tunaiona CHADEMA au tunamuona Mbowe? Huenda chadema iliisha kabla ya uteuzi wa mgombea urais na sasa tunashughulika na Mbowe. Au labda CHADEMA haikuwahi kuwapo siku zote tulikuwa na Mbowe.
Nakumbuka tulivyomshabulia Zitto. Huenda alikuwa ameona (wakati ule) tunachokiona (sasa).
naihurumia Tanzania.
 
Wala sijaahangaika kusoma contents, kichwa cha habari kimejitosheleza kwa mimi kukujibu kwamba hata Ccm ya sasa siyo ile ya zamani.
Ccm ya zamani ulikuwa ni ya mkulima na mfanyakazi lakini Ccm ya sasa ni ya wezi kuanzia ngazi ya shina mpaka Taifa.
 
ni kweli sishaangai chadema ya sasa imebebwa na mafisadi tofauti na ilivyokuwa zamani
 
CHADEMA YA SASA SIYO ILE YA ZAMANI
Ni muhimu kuanzia mbali mahala fulani. Twaweza kuanzia kuiangalia CHADEMA kabla ya michakato ya uchaguzi. Jinsi ilivyokuwa ikipambana na ufisadi. Tukaifuatilia CHADEMA wakati wa uchaguzi na hasa mchakato wa kumpata mgombea urais.
Hapo tukaona jinsi CHADEMA ilipomtosa mtu aliyetarajiwa na wengi kugombea urais na kumzoa a;liyekuwa anatuhumiwa kuongoza ufisadi. Hapo kuna daraja ambalo CHADEMA au ng'ambo ile siyo CHADEMA ya ng'ambo hii.
Uchaguzi umemalizika Serikali imeingia madarakani. Nguvu ya kupinga matokeo ilikuwa ndogo. Sijui kama anajua kwa nini ni ndogo. 2010 kila kona matokeo ya uchaguzi ya Rais yalinung'unikiwa. Kwa sasa siyo. Wenye akili walielewa.
Kama ndivyo tukianzia CHADEMA YA toka kukatisha daraja na kauli za mbowe tunajiuliza swali: Toka kukatisha daraja nililolieleza tunaiona CHADEMA au tunamuona Mbowe? Huenda chadema iliisha kabla ya uteuzi wa mgombea urais na sasa tunashughulika na Mbowe. Au labda CHADEMA haikuwahi kuwapo siku zote tulikuwa na Mbowe.
Nakumbuka tulivyomshabulia Zitto. Huenda alikuwa ameona (wakati ule) tunachokiona (sasa).
naihurumia Tanzania.
Baada ya kumpokea fisadi Lowassa Chadema kwasasa tofauti yetu na CCM ni rangi za bendera tu.
 
Back
Top Bottom