Wakati mafisadi wakitoa ahadi za matumaini na kufukuzana na kuwania kukimbilia ikulu, wanachama wa CHADEMA Kata ya Kashai Jimbo la Bukoba wao wameamua kutoa msaada wa vifaa vya kujifungulia wakina mama wajawazito katika kliniki.
Vifaa hivyo ni mabeseni 300, gloves 1,000, mipira ya plastic 300, jik maboksi kadhaa na kuahidi kuisaidia zaidi zahanati hiyo ili itoke katika matatizo mengi wanayokutana nayo wananchi.
Hao manesi walioonekana pichani wakipokea msaada wana maswali ya kujibu kwa mkuu wa wilaya, mkurugenzi wa halmashauri na baraza la madiwani!! Patachimbika.
Wakati wa kujitafutia umefika kila mahali mtajifanya nyie ni wakarimu na mnasikitishwa na kuumizwa na matatizo ya watanzania wakati ndugu zenu kibao wanazurura hawana kazi wala mitaji ya kufanya biashara, hamna kitu mtapata tumeshawazoe:thumbdown:
Wakati wa kujitafutia umefika kila mahali mtajifanya nyie ni wakarimu na mnasikitishwa na kuumizwa na matatizo ya watanzania wakati ndugu zenu kibao wanazurura hawana kazi wala mitaji ya kufanya biashara, hamna kitu mtapata tumeshawazoe:thumbdown:
Kitu special katika tukio hili ni aina ya msaada, yaani ni vitu simple na vinavyotakiwa na kutumiwa na watu wa kawaida lakini hapo serikali italeta ngonjela za 'tunasubiri mchakato ukamilike' nk.