Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,866
- 4,253
Hili limejidhuhirisha jana kupitia taarifa ya habari ITV (saa tano usiku). Habari ya chadema ilikuwa mwisho kabisa kwa habari za kitaifa, na ya ccm ya pili toka mwisho. Nilipowatazama vigogo wa CCM tangu wanarusha mkutano wao kupitia star tv, kuanzia mzee Sif Idd, Mzee Mwinyi, hadi Magufuli, nyuso zao zimejaa hofu na sintofahamu nyingi. Wamejawa hasira.
Hata Kikwete leo kila aendako na anapoongea unamwona kabisa ana hasira. CCM pale mnazi mmoja Zanzibar walijazana sana na viongozi wao walikuwa wakiongea kwa msisitizo, ghadhabu, hofu, vitisho na sintofahamu nyingi. Hata Magufuli zile mbwembwe zake za pushapu na kadhalika zimepotea. Roho ya CCM iko mikononi mwa Magufuli na si mtu mwingine. Magufuli amechoka sana maana wote wanamtazama yeye.
Kwa upande mwingine kama ningekuwa sioni ningalijua kuwa ccm ndio wanaowania kukiondoa chama tawala madarakani. Wagombea hasa madiwani na wabunge wa ccm wanalia sana juu ya huduma mbovu kwa jamii, na kumuomba Magufuli akiingia aboreshe hayo yote. Wanamwonea Magufuli. Waharibu wengine asafishe Magufuli.
UKAWA kwao ni sherehe. Nilivyotazama jana mkutano wao wa mwisho Mwanza ilikuwa ni SAWAZISHA. Yani kwa kiburi cha chombo cha habari hata sikusikia hotuba bali ni watu wakiserebuka tu. Mbowe akiendelea kutoa maelekezo ya namna ya upigaji kura, Lowassa akicheza dansi, huku wananchi ndio wakionekana waongeaji na watoa maoni. Sasa UKAWA wanaelekea Mbeya kuweka mfuniko wa zege juu ya kaburi.
Mfuniko unaobebwa na wananchi na sio tingatinga. Ni utimilifu wa nyakati tu na hakuna lugha nyingine. Ni ngumu kuzuia kifo. Ni ngumu pia kuzuia mafuriko kwa mikono.
Pia kwa wale wagombea na wanasiasa wote waliotangulia mbele ya haki katika kipindi hiki wakiwa mstari wa mbele, bila kujali itikadi ya vyama vyao. Nawaombea kila la heri huko waendako. Mungu na awape stahili yao, Amina.
Hata Kikwete leo kila aendako na anapoongea unamwona kabisa ana hasira. CCM pale mnazi mmoja Zanzibar walijazana sana na viongozi wao walikuwa wakiongea kwa msisitizo, ghadhabu, hofu, vitisho na sintofahamu nyingi. Hata Magufuli zile mbwembwe zake za pushapu na kadhalika zimepotea. Roho ya CCM iko mikononi mwa Magufuli na si mtu mwingine. Magufuli amechoka sana maana wote wanamtazama yeye.
Kwa upande mwingine kama ningekuwa sioni ningalijua kuwa ccm ndio wanaowania kukiondoa chama tawala madarakani. Wagombea hasa madiwani na wabunge wa ccm wanalia sana juu ya huduma mbovu kwa jamii, na kumuomba Magufuli akiingia aboreshe hayo yote. Wanamwonea Magufuli. Waharibu wengine asafishe Magufuli.
UKAWA kwao ni sherehe. Nilivyotazama jana mkutano wao wa mwisho Mwanza ilikuwa ni SAWAZISHA. Yani kwa kiburi cha chombo cha habari hata sikusikia hotuba bali ni watu wakiserebuka tu. Mbowe akiendelea kutoa maelekezo ya namna ya upigaji kura, Lowassa akicheza dansi, huku wananchi ndio wakionekana waongeaji na watoa maoni. Sasa UKAWA wanaelekea Mbeya kuweka mfuniko wa zege juu ya kaburi.
Mfuniko unaobebwa na wananchi na sio tingatinga. Ni utimilifu wa nyakati tu na hakuna lugha nyingine. Ni ngumu kuzuia kifo. Ni ngumu pia kuzuia mafuriko kwa mikono.
Pia kwa wale wagombea na wanasiasa wote waliotangulia mbele ya haki katika kipindi hiki wakiwa mstari wa mbele, bila kujali itikadi ya vyama vyao. Nawaombea kila la heri huko waendako. Mungu na awape stahili yao, Amina.