CHADEMA (UKAWA), Msisahau agenda hii muhimu

CHADEMA (UKAWA), Msisahau agenda hii muhimu

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,056
Reaction score
10,729
Haikushangaza Mwalimu Nyerere alipoamua kuwageuka wana CCM wenzake na kwa kushauri na kushinikiza kuwa Nchi yetu iingie katika mfumo wa Vyama vingi.

UKWELI ni kiwa BILA UPINZANI IMARA NCHINI, Watawala wa CCM wataifilisi nchi hii. Embu hata wewe msomaji fikiri nchi hoi isingekuwa na upinzani imara hasa chini ya CHADEMA, hali ingekuwa je mfano matukio kama MEREMETA, EPA, MISHAHARA HEWA, ESCROW na mengineyo yangetupeleka wapi?

Ni kwa sababu hii nimeona niwakumbushe viongozi wetu wa Upinzani hasa Vyama vya UKAWA (Japo naamini watatafuta jina jipya sasa,), Kuwa Uchaguzi wa serikali za mitaa hauko mbali no desemba. Ni vema sasa kazi ya kitoa hamasa na elimu kwa umma ianze tena kwa kasi na kujipanga.

Vinginevyo, Tusishangae UHARAMIA wa Dodoma (BMT) ukahamia katika uchaguzi huu muhimu!
 
Huo ndio ukweli elisheni watu hasa vijana na wakina mama ili tuweze kutengeneza foundation ili tuweze kushinda uchaguzi mkuu.
Pili wabunge wenu wa sasa watembelee wadau hata kwenye vijiwe ili kuwainspire mapema watu na sio zima moto.
 
kwa uboreshaji wa daftari tayari au wananchi tunangoja ukawa wadai kwa niaba yetu vinginevyo daftari la CCM litatumika tukizubaa
 
Back
Top Bottom