Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,331
CHADEMA UK TUNATOA PONGEZI KWA MAFANIKIO YA MKUTANO MKUU
Siku kadhaa zilizopita CHADEMA kikiwa ni chama kinachobeba ndoto za ukombozi za waTanzania walio wengi, kilipiga hatua kubwa na kukamilisha jambo la kihistoria. Baada ya kujenga chama kwenye ngazi na mashina, misingi, wilaya na kanda, CHADEMA ilifanya mkutano mkuu wa kuchagua viongozi wakuu wa chama kuanzia kiti cha Mwenyeki na Katibu pamoja na mabaraza ya chama.
Katika uchaguzi huo ambao uliendeshwa kitaalamu na kwa umakini mkubwa viongozi wakuu walipatikana kwa njia ya demokrasia. Hili lilikuwa ni jambo la kishujaa lililowahakikishia wale wenye duku duku kuhusu uimara wa vyama vya upinzani kama CHADEMA ukichukulia maanani namna ambavyo serikali inatumia njia za kiharamu kuviua vyama hivi either kwa kupandikiza puppets au kwa kutumia vyombo vya dola kama Policcm kuvikandamiza. Ukomavu huu wa kisiasa ni ishara kubwa kwamba sasa CHADEMA iko tayari kuishika dola na kuwabadili waTanzania na kuwapa tena heshima yao waliyokuwa wameipoteza kutokana na mlolongo wa viongozi na serikali nyepesi zilizokosa uchungu na uzalendo kupelekea kuuza nchi na kuwaacha waTanzania wakiteseka.
Sisi CHADEMA UK tunapenda kuchukua nafasi hii kuipongeza safu nzima ya ungozi kwa kupata dhamana ya kukiongoza chama. Kipekee na makusudi ya dhati kabisa, tunapenda kumpongeza kamanda Mbowe na Dr Slaa kwa kukubali tena kuipeperusha bendera ya chama wakati huu muhimu tunapoelekea uchaguzi mkuu 2015. Tunapenda kusema kwamba, imani yetu kwa viongozi hawa ni kubwa kwani ni mengi ambayo chama kimepitia chini ya safu hii imara isiyotetereka.
Tunapenda pia kuwapongeza viongozi wote wa mabaraza ya chama (BAVICHA, BAWACHA na Baraza la Wazee la CHADEMA). Mabaraza haya ambayo ni muhimili imara wa chama, ni imani yetu kwamba yamepata viongozi shupavu watakaoleta mabadiliko dhabiti na halisi ili kupambana kumtoa ccm madarakani.
Salamu zetu pia ni kwa viongozi wa ngazi mbali mbali wa chama waliochaguliwa katika hatua mbalimbali zilizokuwa na lengo la kukiimarisha chama kwenye ngazi ya msingi. Tuna Imani kwa kila mmoja yuko tayari kwa mapambano haya.
Mwisho kwa kuyatumia maneno ya Henri Ford aliyesema, "Coming together is a beginning; keeping together is a progress; and working together is a success" tunapenda kuwahakikishia kwamba CHADEMA UK itaendelea kusapoti na kufanya kazi kwa ukaribu na viongozi wote wa ngazi zote za chama kwenye harakati tulizoko sasa hivi. Sisi tunaamini kwamba kwa pamoja tutaweza. Tunaamini katika kufanya kazi kama timu moja tukiwa na lengo na madhumuni mamoja. Kwa kushirkiana kama timu (TEAM: Together Everyone Achieve More) hakuna mbalo CHADEMA itashindwa kutimiza.
Mungu ibariki CHADEMA na nchi yetu ya Tanzania.
Ofisi ya katibu - CHADEMA UK
Siku kadhaa zilizopita CHADEMA kikiwa ni chama kinachobeba ndoto za ukombozi za waTanzania walio wengi, kilipiga hatua kubwa na kukamilisha jambo la kihistoria. Baada ya kujenga chama kwenye ngazi na mashina, misingi, wilaya na kanda, CHADEMA ilifanya mkutano mkuu wa kuchagua viongozi wakuu wa chama kuanzia kiti cha Mwenyeki na Katibu pamoja na mabaraza ya chama.
Katika uchaguzi huo ambao uliendeshwa kitaalamu na kwa umakini mkubwa viongozi wakuu walipatikana kwa njia ya demokrasia. Hili lilikuwa ni jambo la kishujaa lililowahakikishia wale wenye duku duku kuhusu uimara wa vyama vya upinzani kama CHADEMA ukichukulia maanani namna ambavyo serikali inatumia njia za kiharamu kuviua vyama hivi either kwa kupandikiza puppets au kwa kutumia vyombo vya dola kama Policcm kuvikandamiza. Ukomavu huu wa kisiasa ni ishara kubwa kwamba sasa CHADEMA iko tayari kuishika dola na kuwabadili waTanzania na kuwapa tena heshima yao waliyokuwa wameipoteza kutokana na mlolongo wa viongozi na serikali nyepesi zilizokosa uchungu na uzalendo kupelekea kuuza nchi na kuwaacha waTanzania wakiteseka.
Sisi CHADEMA UK tunapenda kuchukua nafasi hii kuipongeza safu nzima ya ungozi kwa kupata dhamana ya kukiongoza chama. Kipekee na makusudi ya dhati kabisa, tunapenda kumpongeza kamanda Mbowe na Dr Slaa kwa kukubali tena kuipeperusha bendera ya chama wakati huu muhimu tunapoelekea uchaguzi mkuu 2015. Tunapenda kusema kwamba, imani yetu kwa viongozi hawa ni kubwa kwani ni mengi ambayo chama kimepitia chini ya safu hii imara isiyotetereka.
Tunapenda pia kuwapongeza viongozi wote wa mabaraza ya chama (BAVICHA, BAWACHA na Baraza la Wazee la CHADEMA). Mabaraza haya ambayo ni muhimili imara wa chama, ni imani yetu kwamba yamepata viongozi shupavu watakaoleta mabadiliko dhabiti na halisi ili kupambana kumtoa ccm madarakani.
Salamu zetu pia ni kwa viongozi wa ngazi mbali mbali wa chama waliochaguliwa katika hatua mbalimbali zilizokuwa na lengo la kukiimarisha chama kwenye ngazi ya msingi. Tuna Imani kwa kila mmoja yuko tayari kwa mapambano haya.
Mwisho kwa kuyatumia maneno ya Henri Ford aliyesema, "Coming together is a beginning; keeping together is a progress; and working together is a success" tunapenda kuwahakikishia kwamba CHADEMA UK itaendelea kusapoti na kufanya kazi kwa ukaribu na viongozi wote wa ngazi zote za chama kwenye harakati tulizoko sasa hivi. Sisi tunaamini kwamba kwa pamoja tutaweza. Tunaamini katika kufanya kazi kama timu moja tukiwa na lengo na madhumuni mamoja. Kwa kushirkiana kama timu (TEAM: Together Everyone Achieve More) hakuna mbalo CHADEMA itashindwa kutimiza.
Mungu ibariki CHADEMA na nchi yetu ya Tanzania.
Ofisi ya katibu - CHADEMA UK