CHADEMA na Sakata la Gas Mtwara

CHADEMA na Sakata la Gas Mtwara

MgungaMiba

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2011
Posts
999
Reaction score
816
Ikumbukwe kuwa mwaka jana mnamo mwezi wa May/June CHADEMA mara baada kuzindua M4C pale Jangwani, DSM, operesheni hiyo ilielekea mkoani Mtwara na Lindi, kwa Mkoa wa Mtwara Operesheni hii ilikwenda kwenye majimbo yote sita na Kata nyingi kwa kila jimbo zilifikiwa, ingawa kwa bahati mbaya Operesheni hii ilikatishwa katika Mkoa wa Lindi kabla haujafikiwa wote kutokana na msiba wa Mzee Bob Makani. Viongozi Wakuu takriban wote walikwenda huko.

Agenda kubwa walioikuta ikiwa na mgogoro mkubwa huko ilikuwa ni suala la bei ndogo ya Korosho na kukosekana kwa malipo ya pili ya zao hilo. Jambo ambalo lilipelekea kutokea vurugu kubwa kwa baadhi ya maeneo kama vile Tandahimba.CHADEMA iliwaambia wananchi hao kuwa kwakuwa Wabunge wao hawawatei Bungeni, basi suala hilo watalibeba wao kwenda kuwawakilisha kwenye kikao kifuatacho cha Bunge.

Lakini CHADEMA ilienda Mtwara ikiwa na Agenda yake, Gesi, wananchi wengi wa huko hawakuwa na habari nayo wala kujua thamani yake halisi zaidi ya kuisikia kwenye vyombo vya habari. CHADEMA kwa makusudi iliamua kuwazindua wananchi hao kwa kuwaambia kuwa wakati wanaumizana kupigania bei ya Korosho, mali yenye thamani ya mabillioni (Gesi ya Asili) inahamishwa kutoka kwao, nao wataachwa hivihivi wakihangaika na bei duni ya Korosho, wakati viwanda vya kuprocess Gesi hiyo vinaweza kujengwa Mtwara na wao wakanufaika.

Aidha mikataba ya ovyo na taratibu zisizo naanufaa zitasababisha Gesi hiyo kunufaisha zaidi wawekezaji hao, Mafisadi wachache Serikalini, na Wananchi wataishia kubebeshwa mzigo mzito wa madeni ya gharama ya kuisafirisha Gesi hiyo na kuendelea kubaki kwenye lindi la umaskini, kama ilivyo kwenye maeneo yenye dhahabu nyingi. Ufafanuzi ulitolewa kwa ufasaha mkubwa na nini kilipaswa kufanyika ili Gesi hiyo iweze kuwaondoa kwenye umaskini na kulinufaisha Taifa kwa ujumla.

Miezi takriban sita sasa tangu Opereshen hiyo ifanyike, Serikali ilipuuza yote yaliyosemwa, kwa maana ina akili sana, ikaendelea na ilivyotaka, ikaenda kukopa Matrillioni kutoka China kwa mikataba ambayo ni rather dubious, ili iweze kuhamisha Ges hiyo kwenda Dar, kisha bila shaka deni hilo lije lilipwe kwa kodi za Wananchi haohao wanaoonekana hawana akili, wahaini nk.

Lakini ni dhahiri Wananchi wa Mtwara, lile somo liliwaingia akilini vizuri sana, wameamka, wamekataa na Ujumbe umefika, serikali inataka haitaki itabidi ifuate ushauri wa Mzee Mkapa, wasiwaite wananchi hao ni wahaini, bali wakae nao, wazungumze nao ili muafaka upatikane, ubabe wa serikali hautasaidia kwani Wananchi wakiamua kwa pamoja wanakuwa na nguvu kuliko Serikali.

Kwa wale wanaodai CHADEMA itoe tamko, sielewi wanataka tamko gani, kwani CHADEMA ilishatoa tamko lake kuhusu Gesi kwa kishindo kikubwa wakati wa Operesheni mpaka Mkoa mzima wa Mtwara ukatikisika na sasa Wananchi wameitika, kazi iko kwa Serikali, kusuka au kunyoa!
 
Vyama vya siasa vinatakiwa kuwekeza kwenye Elimu kwa umma then umma uchagua na kuamua cha kufanya.
Hii ilikuwa ni Elimu nzuri kutolewa, tufike mahali tuwe tunahoji maslai yetu
 
Vyama vya siasa vinatakiwa kuwekeza kwenye Elimu kwa umma then umma uchagua na kuamua cha kufanya.
Hii ilikuwa ni Elimu nzuri kutolewa, tufike mahali tuwe tunahoji maslai yetu
Nina hamu na hii elimu ikatolewe kule kwetu usukumani kijiji kwa kijikiji kama walivyo fanya Mtwara na Lindi...
 
Pia Chadema walisema kutokana na wingi wa gesi ulioko ukanda wa kusini Lindi na Mtwara kujengwe chuo kikuu cha gas Mtwara kusomesha vijana katika fani ya Gas na Mafuta kuwaandaa kwaajili ya kunufaika na rasilimali hiyo kubwa! Hili jambo alisema Zitto tena Bungeni wakati akisoma makadirio na bajeti mbadala ya upinzani! Wanaodai chadema itoe tamko ni mabulula wa siasa nchini!
 
Ni kweli hakuna jambo pasipo mwanzo wake. Mimi napenda kusema wazi kuwa wanasiasa wa vyama vya upinzani hasa CHADEMA ni watu makini sana kiasi cha kuamsha watanzania kudai haki zao kwa nguvu ya umma. Kinachotakiwa ni watanzania kuiamini Chadema nchi nzima ili kukomesha dhuluma ya CCM kwa wananchi wa Tanzania. Huyu waziri wa nishati aende akajifunze kastama kea kabla ya kuanza kuwahudumia wateja ambao ni wananchi. Hivi unapowaita watu wa Mtwara hawana elimu una maana gani? UnAposema CHADEMA na marafiki zakE ni wachochezi, unajua unachosema au unarukia gari kwa mbele?

PAMOJA TUTASHINA HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE SI MTWARA TU BALI TANZANIA YOTE
 
Hapa kwetu Mwanga Mlima wote umejaa tanzanite na dhahabu wa upande usang na Ugweno,Copper na tanzanite kwa upande wa Mwanga wachina wamechimba wakatosheka wameondoka nadhani wanaenda kujipanga ili waje wanunue mlima wote wenye copper huku ndege (helcopter) za watafiti zikipita kila siku kuuzunguka mililma yote. Naingia rasmi vitani kutoa elimu hiyo naomba makamanda wa CDM mje tusaidiane ili wakija tu kwa ajili ya mikataba tuwe tayari kuwatoa korodani hao maccm tutakuwa tumeshaiva na kuelimika
 
Chadema ndio siri ya ushind wa kila kitu ipewe itubadilishie life.i love cdm
 
Back
Top Bottom