Vox Populi Vox Dei
Member
- Jun 30, 2013
- 21
- 14
Mimi ni mwana Chadema ambaye msimamo wangu juu ya chama changu hautiliwi shaka.Lakini kwa hili naomba nikiombe chama changu na viongozi wangu wa juu kuwa,wakati umefika wa kuwalipa mishahara viongozi wa Wilaya na Mikoa hasa Wenyeviti na Makatibu.
Si kweli kwamba ni viongozi wa Makao Makuu ya Chama tu ndiyo wanaofanya kazi kubwa inayostahili malipo.Kazi inayofanywa na viongozi wa ngazi za chini pia ni kubwa ambayo kuna kila sababu ya kuwalipa mishahara watu hawa. Viongozi wa mikoa na Wilaya kwa muda wamefanya kazi za chama na kuacha hata majukumu yao ya kifamilia kwa kujitolea tu.
Wakati umefika sasa chama kiwalipe mishahara ili wafanye kazi za chama kwa ari zaidi. Zile nyimbo za kuwa chama hakina fedha zimepitwa na wakati. Haiwezekani wakurugenzi wa chama makao makuu wakalipwa zaidi ya 1m halafu zikosekane hata sh laki 3 za kuwalipa viongozi wa mikoa na wilaya.
Nawasilisha.
Si kweli kwamba ni viongozi wa Makao Makuu ya Chama tu ndiyo wanaofanya kazi kubwa inayostahili malipo.Kazi inayofanywa na viongozi wa ngazi za chini pia ni kubwa ambayo kuna kila sababu ya kuwalipa mishahara watu hawa. Viongozi wa mikoa na Wilaya kwa muda wamefanya kazi za chama na kuacha hata majukumu yao ya kifamilia kwa kujitolea tu.
Wakati umefika sasa chama kiwalipe mishahara ili wafanye kazi za chama kwa ari zaidi. Zile nyimbo za kuwa chama hakina fedha zimepitwa na wakati. Haiwezekani wakurugenzi wa chama makao makuu wakalipwa zaidi ya 1m halafu zikosekane hata sh laki 3 za kuwalipa viongozi wa mikoa na wilaya.
Nawasilisha.