Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,321
- 9,745
Ndugu zangu Watanzania,
Nimepenyezewa taarifa kuwa CHADEMA hakukaliki wala hakuendeki wala hakupangiki mikakati ya aina yoyote ile. Hii ni baada ya ujio wa Makonda kuonekana kuwa tishio kwa uhai wa chama hicho cha upinzani ambacho kinaendelea kusambaratika na kudhoofika kila uchwao.
Inasemekana kikao cha dharura cha kamati kuu kinakwenda kuitishwa muda wowote ule kujadili namna ya kukabiliana na nguvu kubwa na ushawishi wa Makonda ulionekana kuteka mijadala ya kisiasa hapa nchini na kuonekana kuwa na nguvu ya ushawishi kwa wananchi wanaopenda siku zote mtu na kiongozi wa maamuzi magumu, ujasiri na kujiamini aina ya Paul Makonda.
Mtoa taarifa wangu amenieleza kuwa viongozi wote kwa sasa ndani ya kamati kuu ya CHADEMA hadi kanda wamevurugwa akili na kuchanganyikiwa ghafla kutokana na ujio wa Makonda unaoendelea kuzima taarifa zao na kukiweka chama cha mapinduzi midomoni mwa watanzania muda wote.
Kwa sasa CHADEMA haieleweki kama ipo stoo au kabatini au mfukoni mwa Mwenyekiti mwenyewe, haieleweki nini kinaendelea juu ya CHADEMA maana Makonda kateka anga lote la siasa na kuvishika mateka vyama vyote vya upinzani ambapo mpaka muda huu vipo chini ya ulinzi mkali sana wa komandoo na jasusi wa siasa ndugu Paul Makonda huku vikiwa mikono juu kichwa chini mwendo wa mateka.
Mtoa taarifa wangu anasema viongozi mbalimbali wa CHADEMA wanataka wakutane kwa dharura ili waone wafanyeje kumkabili Makonda, wengine wakadai kuwa GIA ya kumchafua kwa tuhuma za uzushi imegonga mwamba masikioni mwa watanzania na badala yake ameendelea kuchanja mbuga katika mioyo ya Watanzania ambao wameonekana kuwa na shauku kubwa sana ya kumsikiliza Makonda na kutaka aanze ziara zake mikoani anakosubiliwa kwa hamu kubwa sana ili wamlaki kwa kishindo.
Wanajiuliza kama hajaanza ziara za mikoani tayari jina lake limeshatangulia na kuwatetemesha watu na kuteka mijdala yote mitaani na watu kuwa na hamu ya kumuona na kumsikiliza ,vipi akifika na kuanza kuvurumisha makombora? Nani atasalimika? CHADEMA itaficha wapi sura zao? Habari zao zitasikika wapi? Nani ataandika au kutangaza habari za chadema katika magazeti na hata TVs?
Inasemekana CHADEMA wapo katika wakati mgumu sana na hawaelewi wafanye nini hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa CHADEMA inapenda sana kutembelea matukio tukio ya mpito. Kwa hakika Makonda anawalaza na viatu chadema nzima kwa sasa. Hawahemi wala kupumua, ni roho juu juu tu kama wagonjwa mahututi.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Nimepenyezewa taarifa kuwa CHADEMA hakukaliki wala hakuendeki wala hakupangiki mikakati ya aina yoyote ile. Hii ni baada ya ujio wa Makonda kuonekana kuwa tishio kwa uhai wa chama hicho cha upinzani ambacho kinaendelea kusambaratika na kudhoofika kila uchwao.
Inasemekana kikao cha dharura cha kamati kuu kinakwenda kuitishwa muda wowote ule kujadili namna ya kukabiliana na nguvu kubwa na ushawishi wa Makonda ulionekana kuteka mijadala ya kisiasa hapa nchini na kuonekana kuwa na nguvu ya ushawishi kwa wananchi wanaopenda siku zote mtu na kiongozi wa maamuzi magumu, ujasiri na kujiamini aina ya Paul Makonda.
Mtoa taarifa wangu amenieleza kuwa viongozi wote kwa sasa ndani ya kamati kuu ya CHADEMA hadi kanda wamevurugwa akili na kuchanganyikiwa ghafla kutokana na ujio wa Makonda unaoendelea kuzima taarifa zao na kukiweka chama cha mapinduzi midomoni mwa watanzania muda wote.
Kwa sasa CHADEMA haieleweki kama ipo stoo au kabatini au mfukoni mwa Mwenyekiti mwenyewe, haieleweki nini kinaendelea juu ya CHADEMA maana Makonda kateka anga lote la siasa na kuvishika mateka vyama vyote vya upinzani ambapo mpaka muda huu vipo chini ya ulinzi mkali sana wa komandoo na jasusi wa siasa ndugu Paul Makonda huku vikiwa mikono juu kichwa chini mwendo wa mateka.
Mtoa taarifa wangu anasema viongozi mbalimbali wa CHADEMA wanataka wakutane kwa dharura ili waone wafanyeje kumkabili Makonda, wengine wakadai kuwa GIA ya kumchafua kwa tuhuma za uzushi imegonga mwamba masikioni mwa watanzania na badala yake ameendelea kuchanja mbuga katika mioyo ya Watanzania ambao wameonekana kuwa na shauku kubwa sana ya kumsikiliza Makonda na kutaka aanze ziara zake mikoani anakosubiliwa kwa hamu kubwa sana ili wamlaki kwa kishindo.
Wanajiuliza kama hajaanza ziara za mikoani tayari jina lake limeshatangulia na kuwatetemesha watu na kuteka mijdala yote mitaani na watu kuwa na hamu ya kumuona na kumsikiliza ,vipi akifika na kuanza kuvurumisha makombora? Nani atasalimika? CHADEMA itaficha wapi sura zao? Habari zao zitasikika wapi? Nani ataandika au kutangaza habari za chadema katika magazeti na hata TVs?
Inasemekana CHADEMA wapo katika wakati mgumu sana na hawaelewi wafanye nini hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa CHADEMA inapenda sana kutembelea matukio tukio ya mpito. Kwa hakika Makonda anawalaza na viatu chadema nzima kwa sasa. Hawahemi wala kupumua, ni roho juu juu tu kama wagonjwa mahututi.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.