CCM yatabiriwa ushindi mkubwa

CCM yatabiriwa ushindi mkubwa

elivina shambuni

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2018
Posts
461
Reaction score
295
1566566538962.png


CHAMA cha siasa cha Ada Tadea kimetoa tathmini ya hali ya kisiasa nchini na kusema vyama vya upinzani vitapata wakati mgumu kushinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao kutokana na kasi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya utekelezaji wa ilani ambao umelenga kuleta maendeleo na ustawi wa jamii.

Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Ada-Tadea, Juma Ali Khatib wakati alipozungumza na waandishi wa habari akielezea tathmini ya hali ya kisiasa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baadaye mwaka huu. Khatib amesema vyama vya upinzani vimepoteza dira na mwelekeo wa kisiasa ambapo baada ya kujikita katika utekelezaji wa ilani ya vyama vyao sasa wamekumbwa na migogoro ya kisiasa.

Amesema wananchi wengi kura zao zitaelekea kwa CCM kutokana na kasi ya maendeleo inayotokana na usimamizi wa miradi ya huduma za jamii. “Viongozi wa vyama vya upinzani tumepoteza dira na muelekeo wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na sasa tumejikita katika migogoro ya kisiasa,” amesema mwanasiasa huyo.

Alifafanua zaidi na kuongeza kwamba ni vigumu kukiondoa madarakani Chama Cha Mapinduzi ambacho viongozi wake wameonesha uwezo na ubora katika kutekeleza na kusimamia maendeleo ya jamii. Kwa mfano, alisema kwa upande wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ameonesha uwezo mkubwa katika kipindi cha miaka minne kwa kutekeleza miradi mikubwa ya miundo mbinu na nishati ya umeme.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo Tanzania inayo uwezo mkubwa wa kufua umeme na hivyo kutekeleza dhana ya sera ya viwanda inayotekelezwa hivi sasa. “Rais John Magufuli ameonesha uwezo mkubwa wa uongozi kutekeleza Ilani ya CCM katika maeneo ya miundombinu na nishati ya umeme,” aliongeza kiongozi huyo wa upinzani.

Aidha, kwa upande wa Zanzibar, alisema CCM itashinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kutokana na upinzani kutawaliwa na ubinafsi na uchu wa madaraka.

Alisema wapo viongozi wa vyama vya siasa tangu mwaka 1995 wamekuwa wakigombea nafasi ya urais, kitendo ambacho kinaonesha kutawaliwa na uchu wa madaraka na ubinafsi. “Kasi ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Zanzibar inayotekelezwa na Rais Shein bila ya wasiwasi wapinzani hawana nafasi ya kupenya na kushinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020,” alisema.
 
Mimi sina kadi ya ccm ila huyu magufuli hana mpinzani
Nipo tayari kumpigia kampeni kila kijiji ashinde 100%

Huyu magufuli ungekuwa ulaya angeheshimika sana
 
Ndugu yangu huo sio utabiri ndivyo mtakavyofanya uchaguzi itakua ni geresha tu ila ukweli matokeo yatapikwa na kuiva! Mark my words
View attachment 1188335

CHAMA cha siasa cha Ada Tadea kimetoa tathmini ya hali ya kisiasa nchini na kusema vyama vya upinzani vitapata wakati mgumu kushinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao kutokana na kasi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya utekelezaji wa ilani ambao umelenga kuleta maendeleo na ustawi wa jamii.

Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Ada-Tadea, Juma Ali Khatib wakati alipozungumza na waandishi wa habari akielezea tathmini ya hali ya kisiasa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baadaye mwaka huu. Khatib amesema vyama vya upinzani vimepoteza dira na mwelekeo wa kisiasa ambapo baada ya kujikita katika utekelezaji wa ilani ya vyama vyao sasa wamekumbwa na migogoro ya kisiasa.

Amesema wananchi wengi kura zao zitaelekea kwa CCM kutokana na kasi ya maendeleo inayotokana na usimamizi wa miradi ya huduma za jamii. “Viongozi wa vyama vya upinzani tumepoteza dira na muelekeo wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na sasa tumejikita katika migogoro ya kisiasa,” amesema mwanasiasa huyo.

Alifafanua zaidi na kuongeza kwamba ni vigumu kukiondoa madarakani Chama Cha Mapinduzi ambacho viongozi wake wameonesha uwezo na ubora katika kutekeleza na kusimamia maendeleo ya jamii. Kwa mfano, alisema kwa upande wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ameonesha uwezo mkubwa katika kipindi cha miaka minne kwa kutekeleza miradi mikubwa ya miundo mbinu na nishati ya umeme.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo Tanzania inayo uwezo mkubwa wa kufua umeme na hivyo kutekeleza dhana ya sera ya viwanda inayotekelezwa hivi sasa. “Rais John Magufuli ameonesha uwezo mkubwa wa uongozi kutekeleza Ilani ya CCM katika maeneo ya miundombinu na nishati ya umeme,” aliongeza kiongozi huyo wa upinzani.

Aidha, kwa upande wa Zanzibar, alisema CCM itashinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kutokana na upinzani kutawaliwa na ubinafsi na uchu wa madaraka.

Alisema wapo viongozi wa vyama vya siasa tangu mwaka 1995 wamekuwa wakigombea nafasi ya urais, kitendo ambacho kinaonesha kutawaliwa na uchu wa madaraka na ubinafsi. “Kasi ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Zanzibar inayotekelezwa na Rais Shein bila ya wasiwasi wapinzani hawana nafasi ya kupenya na kushinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020,” alisema.
 
Mtabiri mwingine huyu hapa lakini leo hii hawezi kuirudia kauli hii anajua ATAKUFA NJAA.



View attachment 1188335

CHAMA cha siasa cha Ada Tadea kimetoa tathmini ya hali ya kisiasa nchini na kusema vyama vya upinzani vitapata wakati mgumu kushinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao kutokana na kasi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya utekelezaji wa ilani ambao umelenga kuleta maendeleo na ustawi wa jamii.

Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Ada-Tadea, Juma Ali Khatib wakati alipozungumza na waandishi wa habari akielezea tathmini ya hali ya kisiasa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baadaye mwaka huu. Khatib amesema vyama vya upinzani vimepoteza dira na mwelekeo wa kisiasa ambapo baada ya kujikita katika utekelezaji wa ilani ya vyama vyao sasa wamekumbwa na migogoro ya kisiasa.

Amesema wananchi wengi kura zao zitaelekea kwa CCM kutokana na kasi ya maendeleo inayotokana na usimamizi wa miradi ya huduma za jamii. “Viongozi wa vyama vya upinzani tumepoteza dira na muelekeo wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na sasa tumejikita katika migogoro ya kisiasa,” amesema mwanasiasa huyo.

Alifafanua zaidi na kuongeza kwamba ni vigumu kukiondoa madarakani Chama Cha Mapinduzi ambacho viongozi wake wameonesha uwezo na ubora katika kutekeleza na kusimamia maendeleo ya jamii. Kwa mfano, alisema kwa upande wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ameonesha uwezo mkubwa katika kipindi cha miaka minne kwa kutekeleza miradi mikubwa ya miundo mbinu na nishati ya umeme.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo Tanzania inayo uwezo mkubwa wa kufua umeme na hivyo kutekeleza dhana ya sera ya viwanda inayotekelezwa hivi sasa. “Rais John Magufuli ameonesha uwezo mkubwa wa uongozi kutekeleza Ilani ya CCM katika maeneo ya miundombinu na nishati ya umeme,” aliongeza kiongozi huyo wa upinzani.

Aidha, kwa upande wa Zanzibar, alisema CCM itashinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kutokana na upinzani kutawaliwa na ubinafsi na uchu wa madaraka.

Alisema wapo viongozi wa vyama vya siasa tangu mwaka 1995 wamekuwa wakigombea nafasi ya urais, kitendo ambacho kinaonesha kutawaliwa na uchu wa madaraka na ubinafsi. “Kasi ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Zanzibar inayotekelezwa na Rais Shein bila ya wasiwasi wapinzani hawana nafasi ya kupenya na kushinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020,” alisema.
 
Huyu Kiongozi wa ada tadea itakua alienda likizo Papua new Guinea toka mwaka 2010 siyo bure.
 
Huu ndiyo utabiri wa kweli, siyo tathmini ya kutoka Bangladesh ya ada tadea
Mtabiri mwingine huyu hapa lakini leo hii hawezi kuirudia kauli hii anajua ATAKUFA NJAA.

 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mtabiri mwingine huyu hapa lakini leo hii hawezi kuirudia kauli hii anajua ATAKUFA NJAA.



Mkuu nakuomba hii video uitume kwa email angalau kwenye balozi za Marekani na Uingereza wajionee wenyewe vioja. Hakikisha unatoa tafasiri ili usiwape shida ya kutafuta wakalimani.
 
Sijawahi kuona wala kusikia ujinga wa kiwango hiki.
 
Saisa ya Tanzania raha sana tena sana. Nasikia kuna Chama cha Upinzani Tanzania kinaitwa TLP, mwenyekiti wa Chama chake katangaza Mwenyekiti wa Chama kingine kuwa ndo mgombea wao. Sasa sijui atahama Chama au atagombea akiwa hukohuko na wao waendelea kuimba mapambio?
 
Back
Top Bottom