CCM washambulia Wanachama wa CHADEMA

nyakonga

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2015
Posts
201
Reaction score
78
Leo muda wa saa moja jioni maeneo ya Nyakato sokoni Ilemela Mwanza. Wana CCM wakiwa wanatoka kwenye kampeni, waliamua kupiga kila waliye kutana naye njiani akiwa na Bendera ya UKAWA na hata kupiga magari na baadhi ya magari kuharibiwa na kusababisha vurugu/foreni kubwa eneo hilo bila hata kuzuiwa na Jeshi la polisi ambalo lilionekana eneo hilo.

Kitendo hiki kisipo kemewa kwa nguvu zote kitatuharibia Amani yetu tulio nayo. Na kwa sasa umezuka mtindo wa wanaccm kupiga watu hasa katika Wilaya ya Ilemela pale wanpo kuwa wanatoka katika kampeni bila sababu yoyote pale wanapokuona una kitu chochote kilicho na Maandishi ya vyama vingine (ukawa).

Tafadhali sana tunaomba Jeshi letu la Polisi lidhibiti hali hii kabla ya uchaguzi kufanyika.
 
CCM wameanza kuwa Janjaweed aisee.. Hapa ndio tunaanza kuona kazi nzuri za wana UKAWA na Lowassa.
 
Ni vizuri na wagombea wote wakemee jambo hili kwa haraka sana. Na pale Mh. Highnes Kiwia anapo pata taarifa kuwa wanachadema wanapigwa basi awe mwepesi kushughulikia swala hili kwa kuwapigia polisi na kuna wakati vijana wa ccm wanawapiga vijana wa chadema na kuwakamata na kuwafunga kamba na kuwaingiza kwenye buti ya gari kwa kisingizio cha kuzomewa bila hata kuwapeleka Polisi.
 
Mwanza ni sehemu sensitive sana kisiasa. Polisi fanyeni kazi yenu watu wa Kanda ya Ziwa huwa hawapigwi. Wanapigana.

Msiwaache wakapigana.
 
Mwanza ni sehemu sensitive sana kisiasa. Polisi fanyeni kazi yenu watu wa Kanda ya Ziwa huwa hawapigwi. Wanapigana.

Msiwaache wakapigana.

Kama vurugu za kisiasa zitatokea mwaka huu mkoa wa kwanza ni Mwanza,
Star tv ndio wahusika wakuu wa kupiga huo mgogoro
 
Sasa hivi kumezuka mtindo mbaya sana, Chadema wakifanya mkutano maeneo ya mjini, Ccm hawaruhusu kupita barabara ya Nyerere road kwa kisngizio kuwa kuna Jengo lao maeneo ya Natta na hata wakati mwingine wana wapiga wale wote wanaopita na Bendera au kofia.
 
mwaka huu nimeota jeshi la polis, tume ya uchaguzi na ccm ndo watakaoanzisha vurugu kwenye uchaguzi huu...
 

haa haa ina maana wanachadema hawawezi kujitetea mpaka waite polis haa haa...
 

haa haa huu unyonge wa chadema siungi mkono kamwe... kama mbwai na iwe mbwai..
 
Watashindwa.... tuendelee kujipanga tu... na ikishindikana tuwakabili.... hatutaanza mtu... tutawaelewa ila wasitufanye dodoki....
 
Utafiti wa haraka unaonyesha , pale wagombea wanapo kosa watu kwenye mikutano yao ya kampeni wanamua kuhamasisha vunjo bila sababu yoyote na sasa kama ni hivyo je kwenye matokeo itakuaje?
 

Wana gasp
 

Edit uondoe neno 'tukufu' maana jeshi hilo halina utukufu wowote.
 
haa haa ina maana wanachadema hawawezi kujitetea mpaka waite polis haa haa...

Chadema waliapa kufanya kampeni za kistaarabu na kuonyesha uvumilivu na ustaarabu wa hali ya juu. Sasa naona kumbe tunamuonyesha nguruwe ustaarabu nae haujui ustaarabu.

Virugu si jadi ya chadema, wataendelea kuwaita polisi..... Ila mjue yana mwisho haya.
 
Nimeheshimu maoni yenu na nimeondoa neno tukufu. Tuendelee kujadili.........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…