CCM wakubali badaliko rasmi

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
761
Reaction score
6,985
Kuwa CCM Ni Kazi Ngumu Sana Ndugu Zangu, ila tunabadilika haraka kuliko mnavyotuchukulia, kwa mfano:

Mwaka Juzi Tulishangilia Watumishi Walio Na Vyeti Feki Kufukuzwa, Leo Wamerudishwa Kazini Tunashangilia Tena.

Juzi Tulishangilia Tozo Zilivyowekwa Leo Tozo Zimepunguzwa Tunashangilia Tena,

Tulisimama na Mwenyekiti kwamba hakuna Corona Tanzania, leo tumesimama na Mwenyekiti mpya kwamba corona ipo na chanjo ni muhimu

Tulisimama na spika kwamba wanaotaka kuchanjwa ni vibaraka wa mabeberu na kuwafukuza bungeni, leo tumewafukuza Bungeni waliotukumbusha msimamo wetu wa jana.

Tulishangilia Sabaya anachapa kazi, tukamzomea alipotumbuliwa, tunashangilia Tena kwamba alitishiwa kuuwawa na Mbowe.

Kwa namna tunavyobadilika kwa kasi hata wapinzani zetu awawezi kufikia Kasi hiiπŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†
 
Hiyo ndio kijani bwana.
 
Leta ushahidi wa haya yote unayosema bila kusahau kuwa tupo awamu ya 6 na sio ile ya Mi5 tena
 
CCM kumejaa watu wajinga sn
 
Huku kijanini ni marufuku kufikiri kwa akili zetu,mwenye nzengo akisema hakuna kumbishia.Halafu,sie tulifundwa tukafundika si adabu kusema mkubwa kajamba.Hivyo tuacheni tudemke na mkwaju ngoma wetu
 
Kumbe umekwisha hama upinzani? Karibu sana CCM.
tunaambiwa "kitu pekee ambacho unatakiwa ukitegemee ni kubadilika"
 
Ccm kama misukule vile yaani. Huku wapo huko wapo na pale wapo.
 
JUMUIYA YA WAZAZI CCM tunashukuru kutuzalia UVCCM (IGP alishasema Wazazi na Watoto wa hovyo hovyo)..
 
Na kichwa maji anasema Yesu alioa na tukagonga meza kushangilia
 
Kuna mambo inabidi uwe na akili ya mwendawazimu ili uweze kinafanya...
 
Raha sana kuishi Tanzania, nchi ya watu kinyonga na vigeugeu wasiojielewa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…