CCM Tujiulize, Hawa Watu Wanatuonaje ama Wanatuchukuliaje?

CCM Tujiulize, Hawa Watu Wanatuonaje ama Wanatuchukuliaje?

1954tanu

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
1,038
Reaction score
487
Imekuwa kawaida sana kuchukua watu huku na kuwapeleka kule kunako mikutano yetu ya kampeni za kisiasa. Watu hawa hubebwa kwa kila aina ya usafiri: mabasi makubwa na madogo, malori, matrekta, power tiller na mwingineo. Huku tuki walipa malipo ya kuhudhuria kwao elfu tano tano, elfu mbili mbili, sare, kofia TShirt nakadhalika.

Watu awa hawa walihudhuria ama watahudhuria mkutano mwingine wa mgombea wa upinzani wakijihudhurisha wenyewe. Wanaenda kwa miguu yao tena pasipo kulipwa chochote kwa umbali ule ule tuliowabeba kwa magari.

Hawa watu wanatuonaje; wanatuchukuliaje?

Kwamba tumechanganyikiwa? Ama ghafla tu tumewapenda sana? ama watuonee huruma tumekosa watu? ama sisi ni mazuzu fulani hivi? ama tumekuwa mabuzi, tumejipeleka tuchunwe? ama sasa ndio tunaanza kuona umuhimu wao? ama sisi ni mabwege fulani hivi, kwa hiyo wanatugida?

Halafu jioni ama siku ifuatayo, wanajiona kwenye vyombo vya habari "mafuriko" makubwa wamkubali mgombea wetu. Na huku wangali wanajua jinsi walivyofurikishwa,hawa hawakufurika eti! Wanatuonaje fikrani mwao? Wanamwonaje mgombea wetu anavyo jishebedua mbele ya watu waliofurikishwa?

Tusaidiane. Isije ikawa ni "Tumgidie -----" ya marehemu John Rutahayasingwa kwenye yale magazeti ya Mzalendo Enzi zile..
 
Toka lini umekuwa mwanaCCM?

11243638_1619925658277540_6823470039063086561_n.jpg


11954765_1619926598277446_7250682606156853672_n.jpg
 
Ni kwa sababu sera zao tushaziozoea kuwa hua hazitekelezeki kila mwaka wa uchaguzi ahadi ndo hizo hizo, ndo maana watu wanalazimishwa kwenda kwa magali na zawadi juu.
Watu tunataka mabadiliko wao hawaelewi wamekalia na vipaumbele tu
 
Imekuwa kawaida sana kuchukua watu huku na kuwapeleka kule kunako mikutano yetu ya kampeni za kisiasa. Watu hawa hubebwa kwa kila aina ya usafiri: mabasi makubwa na madogo, malori, matrekta, power tiller na mwingineo. Huku tuki walipa malipo ya kuhudhuria kwao elfu tano tano, elfu mbili mbili, sare, kofia TShirt nakadhalika.

Watu awa hawa walihudhuria ama watahudhuria mkutano mwingine wa mgombea wa upinzani wakijihudhurisha wenyewe. Wanaenda kwa miguu yao tena pasipo kulipwa chochote kwa umbali ule ule tuliowabeba kwa magari.

Hawa watu wanatuonaje; wanatuchukuliaje?

Kwamba tumechanganyikiwa? Ama ghafla tu tumewapenda sana? ama watuonee huruma tumekosa watu? ama sisi ni mazuzu fulani hivi? ama tumekuwa mabuzi, tumejipeleka tuchunwe? ama sasa ndio tunaanza kuona umuhimu wao? ama sisi ni mabwege fulani hivi, kwa hiyo wanatugida?

Halafu jioni ama siku ifuatayo, wanajiona kwenye vyombo vya habari "mafuriko" makubwa wamkubali mgombea wetu. Na huku wangali wanajua jinsi walivyofurikishwa,hawa hawakufurika eti! Wanatuonaje fikrani mwao? Wanamwonaje mgombea wetu anavyo jishebedua mbele ya watu waliofurikishwa?

Tusaidiane. Isije ikawa ni "Tumgidie -----" ya marehemu John Rutahayasingwa kwenye yale magazeti ya Mzalendo Enzi zile..


Mkuu ukweli ni kwamba kitengo chetu cha propaganda hapa Lumumba basi tumeishiwa na ubunifu. Hatuelewi ni kwanini lakini tunaomba msaada wenu hali mbaya kuliko mnavyofikiria.
 
Kimsingi tunawachukilieni kama maboya, so tunaenda nanyi kiboyaboya ili msistuke mapema kabla ya kufanya 'seize'!
 
mnatufurikisha ili tuje kumsikiliza Nape anamtukana mtu mwenye umri sawa na baba yake na kumuita marehemu angali hai sasa je sisi mnaotubeba kwenye matrekta huko kwenye vikao vyenu vya siri mnatuitaje mizoga, maiti au nyambore (samahani nyambore ni samaki waliooza)
 
Back
Top Bottom