Sasa huo uzalendo wa kweli kwa upande wa upinzani bado nina mashaka nao. Kwangu mimi naona bado wana deni la kwa namna gani wafanye ili niridhike kua sasa wanaweza kuongoza nchi na kunisahaulishe yale waliyoyafanya mwaka 2015 kwenye uteuzi wa mgombea wao wa nafasi ya urais.
Binafsi nina imani nao tu kwenye nafasi za ubunge na nyingine za chini. Lakini kwenye kuongoza nchi bado hua nahisi wanaweza kurudisha nyuma hata haya maendeleo tuliyonayo.
NB: Kuongoza nchi kama Tanzania sio kitu rahisi, kumbuka hata Mh.Magu alipigwa sana mawe wakati wa uongozi wake na hii ilitokana na mapenzi pamoja n.a. uzalendo aliokua nao kwenye nchi yake..