Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,340
- 283,362
MKUUukisoma kwa umakini uzi huu na posti zake ndio utajua kwanini wanasema watanzania wana IQ ndogo. Kuna watu wanapost bila kusoma uzi unahusu nini, akishaona rangi ya kijani ni kuitukana ccm tu hivi hakuna mazuri yaliyofanywa na ccm au ndio mnafikiri kwa akili za kuambiwa?. Uhalisia na maana ya picha hizi hauwakilishi hali ya watanzania sababu unaweza kutumia picha hizi hizi ukatoa ujumbe ulio positive kwa CCM.
tpaul kwanini usiweke uzi wenye mambo mazuri yaliyofanya na wabunge wa chama chako? au hawajafanya lolote?View attachment 215794
Mzee Ndesa yeye alitoa hii ameweka na ushahidi kabisa hebu tupe za hao wengine
Ahsante sana Mkuu tpaul kusoma michango kama yako na wengine wengi hapa katika kulinda na kutetea maslahi ya Watanzania na Tanzania kwangu mimi ni motivation kubwa sana ya kuja hapa kila siku na kusoma misimamo yenu kuhusu mustakabali wa nchi yetu, bila michango yenu mimi siku nyingi ningekuwa nimeshasepa hapa mahali. Mbarikiwe sana wote na msichoke kuleta michango yenu ya ina mbali mbali ikiwemo picha kama hizi zinazoonyesha hali ya kusikitisha sehemu nyingi nchini mwetu.
tpaul nanyi mnakuja na ngonjera kuwa mtawapatia wananchi maisha bora kumbe ni tamaa ya kushika dola tu. hakuna namna mtaongeza vyanzo vya mapato kuweza kuwapatia watanzania wote maisha bora. picha hizi kama ungezichukua kwa mlinganisho.mfano nyumba mbovu na nyumba bora za kisasa zinazojengwa nchini kote na nssf, na nhc, shida ya maji na juhudi za kutandaza mabomba na miundombinu mingine ya maji, zahanati ya makuti na zahanati bora na zenye vifaa zilizojengwa kwa kipindi chetu hapo ungeeleweka. lakini umefanya makusudi na kujikampenia kwa kuwadanganya watanzania kuwa hali hiyo ndio uhalisia wao kumbe wao wanaona tofauti. wanasafiri kwa barabara za lami, wanalima na wanapata pembejeo kwa wakati, wanauza mazao yao kwenye vyama vyao vya ushirika wanapata umeme wa rea na tanesco, wanapata maji kupitia mamlaka zao za maji wanawapeleka watoto wao wote shule tena sasa hivi zenye maabara na mengineyo mengi tu. wanatumia vipato vyao kujijengea nyumba bora na kujiwekea umeme.hayo uliyotupia ni kaupande kamoja tu ka shilingi tupia upande mmoja wa shilingi na ulinganishe na upande wa pili wa shilingi..usiwahadae watanzania
MKUU
AGOGWE HERI YA MWAKA MPYA , HIVI ILE HADITHI YA ARI MPYA KASI MPYA NA NGUVU MPYA BADO IPO ? Au ULE UTAPELI WA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA BADO MNAUTUMIA ?
heri ya mwaka mpya na kwako pia Erythrocyte hivi maisha bora mnamaanisha kila mtu avae suti??je hizo barabara nzuri,shule na vituo vya afya hamvioni??? kama maisha bora ni mwananchi kupata ni huduma za msingi basi serikali ya chama cha mapinduzi inastahili pongezi, pia nawataarifu kuwa kuna kila dalili watanzania watakichagua chama cha mapinduzi sasa anzeni mapema mazoezi ya maandamano haramu au mtaingia msituni kuchimba dawa:A S wink:
heri ya mwaka mpya na kwako pia Erythrocyte hivi maisha bora mnamaanisha kila mtu avae suti??je hizo barabara nzuri,shule na vituo vya afya hamvioni??? kama maisha bora ni mwananchi kupata ni huduma za msingi basi serikali ya chama cha mapinduzi inastahili pongezi, pia nawataarifu kuwa kuna kila dalili watanzania watakichagua chama cha mapinduzi sasa anzeni mapema mazoezi ya maandamano haramu au mtaingia msituni kuchimba dawa:A S wink:
Huo ndio umbulula wako na chama chako. Mnaiba hela halafu mnatuambia mmeboresha maisha kwa mtanzania. Kwa mtanzania mwenye akili timamu haewezi shabikia ujinga huo[/
mpaka hapo ulipofikia ni kwa sababu ya sera nzuri chama cha mapinduzi waulize wazazi wako watakuambia
picha HIZI CHACHE SANA ( KUMBUKA KWAMBA TUKIWEKA ZOTE UTAKIMBIA NCHI ) ZILIZOMO HUMU ZIMEJIELEZA , SINA LA KUONGEZA .
Huo ndio umbulula wako na chama chako. Mnaiba hela halafu mnatuambia mmeboresha maisha kwa mtanzania. Kwa mtanzania mwenye akili timamu haewezi shabikia ujinga huo[/
mpaka hapo ulipofikia ni kwa sababu ya sera nzuri chama cha mapinduzi waulize wazazi wako watakuambia
Ukisikia mkorosho namba moja ndio ww. Ungejua maisha ya hao wazazi unao wasema wanavyo taabika huko vjjlijjni usingesema hayo. Kodi zinapanda kila siku uchumi unashuka kila siku. Sera za ccm ni za kumkandamiza mlalahoi kila kunapokucha na kuiba pesa tu.
Ukisikia mkorosho namba moja ndio ww. Ungejua maisha ya hao wazazi unao wasema wanavyo taabika huko vjjlijjni usingesema hayo. Kodi zinapanda kila siku uchumi unashuka kila siku. Sera za ccm ni za kumkandamiza mlalahoi kila kunapokucha na kuiba pesa tu.
mkuu huu mgawo wa hela umewafikia watu wengi sana , huyu kijana agogwe nina mashaka naye , HAWEZI KUTOKA POVU NAMNA HII !
mkuu huu mgawo wa hela umewafikia watu wengi sana , huyu kijana agogwe nina mashaka naye , HAWEZI KUTOKA POVU NAMNA HII !
Kanatoa mapovu kama kamikunywa sumu. Katakuwa kaizi nako hako au ndio wale mbululu wa lumimba?
kwani hizo picha zimetoka kenya mkuu?yey kaleta upande huu wa shilingi na wewe lete upande mwingine wa shilingi kama upo poa
CCM imenitendea mengi mzuri
Mkuu laiza mbona unachangia kwa uoga sana, hujiamini? Tuliza akili zako upate kuelewa ujumbe ninaotaka kuufikisha kwa watanzania. Haya maswali yote uliyouliza naona umejikanaganya ama kwa makusudi au kwa kutokujua:
1. Vyanzo vya mapato vitaongezwa kwa kuzuia UFISADI wa fedha za umma tofauti na CCM wanaowatetea mafisadi kwa nguvu zao zote. Wewe hujui kwamba mabilioni ya fedha yanayopotea kila siku ni fedha za wananchi ambazo zingetumika kuwaletea maendeleo? Na je unadhani kwamba yale mabilioni ya EPA aliyoyachukua Kikwete kutoka kwa wezi wa EPA yangejenga barabara ngapi kama angeyarejesha kwa wananchi?
2. Pesa za NSSF sio za UMMA...hizi ni fedha za wanachama zinazotumiwa vibaya kujengea miundombinu ya serikali huku wenye fedha zao hawanufaiki na kitu chochote kutokana na vitega uchumi hivyo. Huoni kwamba ni UCHIZI serikali kutegemea fedha za wanachama huku ikiwaachia wezi wanajichotea fedha za umma? Aidha NHC ni shirika la umma linalojiendesha kibiashara na nyumba wanazojenga wanakaa mafisadi huku wananchi wa kawaida wakiwa hawana mahali pa kuishi. Pia, fahamu kwamba zaidi ya 50% ya nyumba zote zilizojengwa na NHC zimeishanyakuliwa na mafisadi...wamejiuzia kwa bei ya kutupa. Ina maana hata hili hilifahamu au umeamua tu kujitoa akili?
3. Shida ya maji nimeishaionglea kwenye uzi mama hapo juu...hebu tazama picha tu kama hujui kusoma. Unataka SHIDA hii ya maji niiongelee mara ngapi?
4. Ni kweli kabisa kwamba haya matatizo niliyotupia humu ni machache ukilinganisha na hali halisi ya maisha ya watanzania. Hali ya maisha ya wananchi ni mbaya kuliko hii inayoonekana kwenye picha hapo juu. Ni juzi tu mwananchi mmoja aliamua kunadi figo lake ili apate fedha za kujikimu....hali ya maisha ya wananchi ni mabaya kuliko kawaida. Nakupongeza kwa kuuona huo ukweli. Ungana na wazalendo tukaikomboe nchi kutoka mikononi mwa mwa wakoloni weusi (CCM) mwezi wa Oktoba mwaka huu wa 2015.
Kanatoa mapovu kama kamikunywa sumu. Katakuwa kaizi nako hako au ndio wale mbululu wa lumimba?
umeishiwa hoja?:cool2: