CCM na serikali yake wanamuogopa Lowassa, full stop

Majighu2015

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
2,941
Reaction score
3,964
Mkutano wa juzi wa CCM umerihirisha rasmi kuwa CCM na serikali yake wanamuogopa Laigwani. Haiwezekani kila siku watu wanaongea kwenye korido eti Lowassa fisadi. CCM na serikali yake ina vyombo vya dola lakini inaishia kupiga kelele kwenye vyombo vya habari. Huo ni uoga usio na maana,kama wana ushahidi si waende mahakamani? Na kwa busara ya hali ya juu Laigwani yupo zake kimya anawaangalia tu wanavyotapatapa. Mkutano wa juzi umedhihirisha ni kiasi gani Lowassa anaogopwa.

Mzee wa upako nae alivyohojiwa kuhusu Lowassa kutajwa sana juzi alisema hivi nanakuu "Nani! Lowassa jina lake kutajwa sana katika vikao vya CCM. Hiyo inaashiria kuwa ni mtu tishio. Ndiyo ni tishio na sizungumzi haya kwa ajili ya kujipendekeza, sihitaji ukuu wa wilaya ”

Salute kwako Lowassa, watabaki kupiga kelele tu lakini hakuna atakaekugusa.
 
Ni kweli Mkuu CCM wanamuogopa sana ndo maana walimkata mapema, CHADEMA hawamuogopi kabsa ndo Maana walichana mapema list of Shame alipofika tu Ufipa.

Mheshimu sana huyu Mzee Maana huwa anaishi maneno yake, akiwa CCM alisema "nitawashinda adui zangu ndani na nje ya chama"
 
Kwa kidhungu mtu kama yeye wanamuita Strategist...

Ana uwezo wa kum neutralize adui akawa kama kinda la njiwa..

Wataalamu wa mambo wanakwambia hivi, nina nukuu
'""Mpende ndugu yako na jirani yako kwa dhati kama unavyojipenda wewe mwenyewe, ila mpende sana na muweke karibu zaidi adui yako ili uweze kuzimiliki silaha zake ziwe zako na asiweze kukushambulia tena""
Mwisho wa siku utaishi kwa raha muatarehe maana adui umeshamzimisha..
 


Kama fisadi lako Lowasa angeogopewa si angekuwa Raisi wa JMTZ leo hii?
 
Hivi, huyu anayejiita Mzee wa upako ana umri gani? Mbona anaonekana ni mtu mzima lakini anaongea kama vijana waliozaliwa '90 na kuendelea? Yaelekea hajui siasa na wanasiasa mwaka '95 ilikuwaje. Ndo maana hajui neno ukoma liliingiaje katika siasa mwaka huo. Kama angelijua asingezungumza upuuzi huo. Mzee wa upako, Askofu Gwajima duh!! iko kazi.
 
Hata shetani anatajwa Kila dakika na wanadamu...pia anaogopwa
 
nyie ufipa ndio mnamuogopa mliandamna nchi nzima kusema yeye fisadi sasa mmemukumbatia .. shame
 
Wanamuogopa?
 
nyie ufipa ndio mnamuogopa mliandamna nchi nzima kusema yeye fisadi sasa mmemukumbatia .. shame
Walivyojua ukweli wakanyamaza...si apelekwe mahakamani?wakishindwa wananchi tufungueni kesi kama inawezekana nchi ipepesuke🙁
 
Labda tukuulize wewe. Kwanini kwenye ule mkutano lowassa alikua agenda yenu kubwa?
 
Huyo ndiyo the Great Edward Ngoyai Lowassa ndani ya Tz. na Kimataifa wanamjua fika, atawasumbua sana sana bado 2020 akiingia Magogoni watafurahi na kupiga vigelegele,ngonjera,nyimbo na vifijo kama walivyoimba katika Mutano wao Mkuu ...Tuna imani na Lowassaaaa..............................Lowassaaa kweli..................tuombeane uzima na afya njema and be Tuned.
 
Hata baadhi ya wachangiaji humu JF hawakosi mara kwa mara kumtaja Lowassa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…