CCM na Mwenyekiti JPM wana Haki ya kutamba katika Chaguzi zote!!!

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
6,697
9,048
Ni kweli CCM wana haki ya kutamba kwa ushindi wa kishindo kwa chaguzi ndogo za Ubunge jimbo la Dimani Zanzibar na Kata 21 kati ya 22 huko Bara!

CCM na Mwenyekiti wao JPM wana haki ya kutamba kwa ushindi huu kwa vile Tume za Uchaguzi(NEC) kwa Tanzania Bara na ZEC kwa Tanzania Visiwani ni mali za CCM!

Nasema hivi kwasababu Wenyekiti na Wakurugenzi wa NEC/ZEC wote ni wateule wa Mwenyekiti na M/Mwenyekiti wa CCM kwa Bara na Visiwani ambao ndiyo Ma-Rais kwa pande 2 za Muungano! Katika mazingira kama haya kusema Tanzania tuna Uchaguzi ulio HURU NA HAKI hakika ni kudanganyana! Ni kuendelea kuwafanya Watanzania kuwa ni watu mazuzu wasiojitambua!
Sasa tunataka Tume Huru ya Uchaguzi sasa na si vinginevo!
Moderators naomba huu uzi msi uunganishe na ule unaohusu Tume Huru ya Uchaguzi maana inapoteza content iliyomo humu.
 
Back
Top Bottom