wanahaha hao,
Na hii naambiwa ni mikakati yao
kuna ujumbe unasambaa kwa magrup ya ccm NA NI SIRI
CCM YETU, TUILINDE
Ndugu watanzania na wanachama wa CCM, zomea zomea kwa watu wanaovaa sare za Chama chetu imeanza rasmi bila kificho na kuanzia juzi UKAWA walipotangaza mgombea wao hali imekuwa mbaya zaidi.
Tunaomba makada wetu wote kutoingiwa na hofu na Kuendelea kuvaa sare za chama chetu na kutembea kwa makundi ili kuepuka dhahama inayoweza kutokea kwa kuvaa nguo za chama chetu _ CCM
Viongozi wote wa CCM kwenye mikutano yote ya CCM,toeni vitisho kwenye hotuba zenu kama Rais alivyotoa vitisho kwenye hotuba yake ya juzi Ofisi ndogo ya chama Lumumba.
Kwa kutoa kauli za vitisho itasaidia kuwafanya watanzania wasijitokeze kwenye kupiga kura kwa wingi na kufanya zoezi la uchakachuaji kuwa rais zaidi, kwa sababu kama mnavyojua bila uchakachuaji mwaka huu kushinda ni ndoto.
Tunatumia kila idara tulizonazo kuhakikisha UKAWA inapasuka vipande vipande, hivyo viongozi wote wa chama chetu endeleeni kuwaaminisha wananchi kuwa UKAWA ni wapenda madaraka na wao kwa wao wanagombana na hii itafanya wananchi wasio wafuatiliaji wa mambo kuamini na kuzidi kukipa ushindi chama chetu CCM
Popote pale kwenye mwanya wa kukusanya vitambulisho Vya kupigia kura tufanye hivyo na tutapeana maelekezo ya namna ya kuvitumia vitambulisho hivyo hapo baadaye
Tuhakikishe kwa namna yoyote tunamwingiza Magufuli Ikulu maana ni mtu pekee mwenye uwezo wa kulinda chama chetu na mfumo wake kwa kuwa hakijui chama na sisi ndiyo tutamweka madarakani hivyo hata thubutu kuongoza ajuavyo yeye, ni lazima atafwata matakwa ya chama hata kwa yale yasiyo kuwa na maslahi mapana ya nchi na haya ndiyo makubaliano yetu
UJUMBE HUU NI WA SIRI NA TUSIUSAMBAZE KWENYE MAGROUP YA NJE, USAMBAZWE KWENYE MAGROUP YOTE YA CHAMA CHETU
MAKAO MAKUU YA CHAMA CHA MAPINDUZI DODOMA