CCM Mbeya hakieleweki, kumechafuka

CCM Mbeya hakieleweki, kumechafuka

RECEIPT

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2013
Posts
284
Reaction score
198
Hali ya kisiasa mkoani Mbeya kwa sasa ni mbaya hali inayompelekea makamo wa Mwenyekiti Philp Mangula kutua tena kesho. Ikumbukwe Mangula alikuwa na ziara mkoani humo ni mwezi mmoja tu umepita.

Chanzo cha habari hizi kimepata ratiba ya Philp Mangula ya siku nane mkoani mbeya inayoanza kesho. Taarifa za ndani zinasema kwamba Mangula anakuja huku kukiwa ni migogoro ya kichama ktk wilaya za Mbozi, Kyela, Ileje, Mbeya vijijini na Mbeya mjini. Hata hivyo Mgogoro mkubwa ni ule wa Mbozi na Ileje ambao unasemekana unapa UKAWA 75% za ushindi kama watasimamisha mgombea.

Kwa mjibu wa taarifa za ndani za chama cha Mapinduzi, wanachama wengi wamedai chanzo cha migogoro yote ni udhaifu wa Mwenyekiti wa mkoa ambaye ameshindwa kuimdu nafasi hiyo na kuishia kuunda makundi ya urais na Ubunge. Zambi ambaye ndiye Mwenyekiti wa mkoa huo wilayani kwake amekabwa koo ilivyo na Kada mmoja aliyefahamika kwa jina moja kuwa ni Mwenisongole ambaye pia ni MNEC wa Mbozi. Taarifa zinasema kwamba hali hiyo inamfanya Mh Zambi kutoelewana na MNEC na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao wanamuunga mkono Mwenisongold.

Mgogoro mwingine mkubwa ni ule wa Ileje uliopelekea Mh Zambi na kamati yake ya siasa kuvunja kamati ya siasa ya wilaya ya Ileje akiwepo mwenyekiti. Wachambuzi wa Mambo ya siasa wanasema kuwa kamati ya siasa ilivunjwa ili kufifisha nguvu ya Mh Janet Mbene, Naibu waziri wa Viwanda ambaye inasemekana wananchi wanamtaka achukue jimbo hilo.

Mgogoro huo umekuwa wa aina yake kwani baadhi ya vijiji na mitaa wananchi wamegoma kuchukua fomu za kuwania nafasi za serikali za mitaa. Wananchi waliowengi wanasema kuwa Zambi hawezi kuwachagulia mtu wa kuwasaidia. Wamesema wanasubiria kwa hamu uchaguzi wa serikali za mitaa ili wawapigie kura ukawa kama shinikizo la kupuuzwa. Wameendelea kusema kwamba, hata kama Mbene atanyimwa furusa ya kugombea kamwe hawawezi kuipa CCM Kura na watampa mtu yeyote hata kama ni kivuri.

Tulipomtafta Katibu wa CCM MKOA hakuweza kupokea simu tulipokuwa tunataka kujua udharura wa ziara ya Mangula tena Mbeya, wakati DC wa Ileje alisema hii migogoro imeshanichosha, labda watu wakifa ndipo chama kitasikiliza matakwa ya watu.
 
hai hai moto kolea , unguza CCM sambaratisha kabisa uwezo wake, waanachama wawakimbie, kuwe na ugomvi wa kudumu miongoni mwao mpaka watakapokuwa wameondoka madarakani, waongezeana chuki kwa kuchukulia wake na nyumba ndogo, watakapojaribu kuchakachua waumbuke. AMEN.
 
Mbeya kuna maccm? Kama bado wapo wanaumwa ugongwa wa UKAWA
 
Hali ya kisiasa mkoani Mbeya kwa sasa ni mbaya hali inayompelekea makamo wa Mwenyekiti Philp Mangula kutua tena kesho. Ikumbukwe Mangula alikuwa na ziara mkoani humo ni mwezi mmoja tu umepita.

Chanzo cha habari hizi kimepata ratiba ya Philp Mangula ya siku nane mkoani mbeya inayoanza kesho. Taarifa za ndani zinasema kwamba Mangula anakuja huku kukiwa ni migogoro ya kichama ktk wilaya za Mbozi, Kyela, Ileje, Mbeya vijijini na Mbeya mjini. Hata hivyo Mgogoro mkubwa ni ule wa Mbozi na Ileje ambao unasemekana unapa UKAWA 75% za ushindi kama watasimamisha mgombea.

Kwa mjibu wa taarifa za ndani za chama cha Mapinduzi, wanachama wengi wamedai chanzo cha migogoro yote ni udhaifu wa Mwenyekiti wa mkoa ambaye ameshindwa kuimdu nafasi hiyo na kuishia kuunda makundi ya urais na Ubunge. Zambi ambaye ndiye Mwenyekiti wa mkoa huo wilayani kwake amekabwa koo ilivyo na Kada mmoja aliyefahamika kwa jina moja kuwa ni Mwenisongole ambaye pia ni MNEC wa Mbozi. Taarifa zinasema kwamba hali hiyo inamfanya Mh Zambi kutoelewana na MNEC na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao wanamuunga mkono Mwenisongold.

Mgogoro mwingine mkubwa ni ule wa Ileje uliopelekea Mh Zambi na kamati yake ya siasa kuvunja kamati ya siasa ya wilaya ya Ileje akiwepo mwenyekiti. Wachambuzi wa Mambo ya siasa wanasema kuwa kamati ya siasa ilivunjwa ili kufifisha nguvu ya Mh Janet Mbene, Naibu waziri wa Viwanda ambaye inasemekana wananchi wanamtaka achukue jimbo hilo. Mgogoro huo umekua wa aina yake kwani baadhi ya vijiji na mitaa wananchi wamegoma kuchukua fomu za kuwania nafasi za serikali za mitaa. Wananchi waliowengi wanasema kuwa Zambi hawezi kuwachagulia mtu wa kuwasaidia. Wamesema wanasubiria kwa hamu uchaguzi wa serikali za mitaa ili wawapigie kura ukawa kama shinikizo la kupuuzwa. Wameendelea kusema kwamba, hata kama Mbene atanyimwa furusa ya kugombea kamwe hawawezi kuipa CCM Kura na watampa mtu yeyote hata kama ni kivuri.

Tulipomtafta Katibu wa CCM MKOA hakuweza kupokea simu tulipokuwa tunataka kujua udharura wa ziara ya Mangula tena Mbeya, wakati DC wa Ileje alisema hii migogoro imeshanichosha, labda watu wakifa ndipo chama kitasikiliza matakwa ya watu.

nabado maccm hadi mkome
.
 
mpaka kufikia disemba 2014 hapatakuwa na ccm mkoa wote wa mbeya , KYELA KAZI YA KUUA CCM INAENDA VIZURI MNO !
 
Huyo anaye mchafua Mhe, Zambi ni Huyo anaye jifanya kamkaba koo kumbe anajitekenya mwenyewe. Zambi ubunge atashinda na ndio maana Mtela aliamua kujisalimisha. Huyo Mwenisongole ndio anaye hangaika na makundi ya Urais leo kwa Lowasa kesho kwa Pinda mara kwa Wasira. Mwenisongole ni Sheeeeedah kwenye siasa za Mbeya
 
Ilipendekezwa na Rasimu ya Warioba, Ministers wasichaguliwe toka ktk Wabunge...,
Mh J Mbene nae huyoo ileje kwao. Je kabla ya unaibu waziri, Ileje hakuiona?
Ni kwel wana Mbeya huwa ni watu wenye msimamo usiyoyumba. Vituko vitazidi sana CCM, kuelekea G E 2015!
 
Zambi hafai hata kuwa mwenyekiti wa mtaa! Sembuse mwenyekiti wa ccm mbeya!
 
Back
Top Bottom