CCM: Kwanini kisife?

umeongea mengi mazuri, yanayopaswa kufanywa na jamii nzima ya tanzania, kama ushahidi upo hakuna aliye juu ya sheria tusihukumu watu kwa kuwa fulani kaema huyu fisadi tujenge utaratibu wa kumtaka ampeleke mahakamani nae atoe ushahidi sio kutumia vyombo vya habari kulalamika na kupakana matope, sio dhambi ndugu, jamaa, watoto, mke nk kushiriki kwa pamoja shughuli za kisiasa midhali wanapitia mchakato wa kupigiwa kura si kuteuliwa[hata kama hana sifa] tusiwahukumu wanasiasa peke yao yapo maeneo mengi ktk taifa baba,mama na watoto wamekuwa wakifanya kazi pamoja wakiwa wamepitia njia halali na upendeleo hilo ndilo taifa kwa uwazi kabisa hata vyama vingine vyenye nguvu hapa nchini undugu, ujamaa , baba na mtoto wanavyo lkn cha msingi je? wanastahili wamepatikana kwa uwazi kama upendeleo ndo taifa hilo mezea. utekelezaji wa sera ukisimamiwa vzr bila shaka hata vijana kuzurura itapungua kwani fursa nyingi za kijipatia kipato zitapatikana sote kwa pamoja tuuungane kuikosoa serikali inapokosea. na jamii ikubali kupokea maagizo, amri na maonyo toka kwa serikali ili kulinda amani na utulivu.
 

Mkuu nitakupa mifano michache kabisa halafu upime ulichokiandika hapo juu kwenye red kisha tuendelee

- Suala la kuboresha huduma bora za afya na elimu zinahitaji ushahidi gani kuelewa taifa limepoteza kabisa muelekeo?

-Tumeona juzi barlo kauliwa mwanza kipi chepesi wauwaji wa barlo au kamuhanda na timu yake kule iringa kupatikana/kukamatwa?

-Kuhusian na rada unahitaji ushahidi gani kumtia chenge na timu yake kitanzini aliyesema kwa kinywa chake tusishangae vjisent vyake? Au EPA kwamba CCM na serikali yake imeshindwa kupekuwa na kuwaweka ndani wezi nk

-Kuhusu suala la fedha za huko uswisi jukumu la kupekuwa ni letu raia au la watawala tulowapa jukumu la kuongoza?

-Mambo ya siasa za udini nani anatakiwa kupeleleza na kujuwa nani amechoma makanisa kigoma, ruvuma, zanzibar nk na kwanini Kikwete alizunguuka inchi zima kuomba kura bila aibu majukwaani akitumia sera mfu ya udini? refer Omar mahita na majambia ya CUF nk

Ninamengi sana ya kueleza lakini mkuu ww kwa uelewa wako mahakama ya nyani ngedele akitia timu ya kuiba mahindi hukumu itakuwaje? Si umeona kila anapouliwa raia inasemekana ni kitu kizito chenye incha kali - nini tafri yake?


CCm inamlima wa kupanda tena wa mawe na majabali kujiweka sawa, vinginevyo propaganda hazina nafasi.
 
Tatizo walichelewa kwenda kwenye vipimo ili kubaini ugonjwa unaowasibu, wametumia muda wakipoteza na uwezo wao kwa ramli za uongo na vipimo vya kufikiri hii ni typhoid au malaria 2.
Hata baada ya kupewa ushauri nasaha hawakusikiliza, hivyo kukosa kujilinda dhidhi ya kupata maambukizi mapya, hata hawakutumia dawa za kuzuia magonjwa nyemelezi vizuri.
Sasa walipotakiwa kutumia dawa za arv, sio tu wanazitumia vibaya lakini pia wanapewa dawa 'fake' na zilizokwisha kujenga usugu na zingine zimeisha muda wake.
Matokeo si yenye kutia moyo sana, labda watalazimika kutumia '2nd line arv'
 
afya na elimu ni mambo ya msingi nakubaliana na wewe chama na serikali vilipoteza muelekeo baada ya msukosuko mkubwa wa kubadilisha waziri mkuu, binafsi naaamini Edward LOWASSA alikuwa na malengo ya makusudi kusimamia suala la elimu mf; shule za kata na malengo yake ya kuhakikisha anatatua upungufu wa waalimu,[ japokuwa taifa letu, linaathiriwa saaana na staili hii ya uongozi kufanya mabadiliko kwa kutumia fikra zao kiasi wakiondoka madarakani mipango hiyo huyeyuka] baada ya marekebisho hayo ya uongozi serikali ililala, imekosa msukumo lkn daima CCM msingi wake ni usikivu pale kinapokuwa kimepotoka japokuwa kimechelewa saana kufanya mabadiliko ya kweli[ mangula,kinana] hakika Makamba alipewa mzigo mzito alikadhalika Nape alishindwa kujua majukumu yake ni nini? na maagizo ya utendaji wake yanatoka wapi? lkn sasa naamini chama kitajenga heshima, kwa wanachama wake, wanachama wa vyama vvingine na wananchi kwa ujumla. vijisenti jamii iliwahi kumuhukumu bila kujua nini? maana yake kutumia neno hilo [vijisenti] binafsi niliamini kuwa maana yake ' mbona pesa hizi ninazo miliki mimi ni kidogo saaana ukilinganisha na za wengine; jamii ikapotoshwa wakati kumiliki fedha nyingi si tatizo suala umezipataje? Rada wazungu wamekataa hakuna tuhuma za rushwa je? tuwaadhibu tu kwa kuwa wanamiliki fedha nyingi ;hapana; tusiwaoneee nchi nzima ina watu wengi matajiri ushahidi wa wazi ukiwepo hakuna aliye juu ya sheria kumbuka mhalifu akiwa smart ktk uhalifu wake ni vigumu kumtia hatiani. EPA nchi yetu ina wanasheria wakutosha kama rais wetu alikosea kutoa kipndi cha waahalifu kurudisha fedha na waliofanya hivyo kuepuka kufunguliwa mashtaka,naamini busara ya rais kufanya hivyo ni kutokana na kugundua ushahidi ni mdogo ungeweza kuwanufahisha zaidi wahalifu na serikali isinge ambulia chochote; mahakama mkuu yaonekana huna imani na muhimili wa mahakama hivyo maamuzi yoyote yasiyokupendeza unaamini ni upendeleo kwa serikali.mauwaji ya mwangosi tayari kesi iko mahakamani, bunduki iliyotumika ni moja aliyefyatua bomu lililouwa yuko mahakamani tusubiri hukumu [utaifurahia au la] askari weeengi wameuwawa lkn kwa kuwa ni watumishi wa serikali poa tuu, tumeshuhudia mkuu wa wilaya akiwa amekwidwa akipelekwa msobemsobe [sheria mkononi hiyo ni sawa] lkn chama makini kilipaswa kutoa karipio kwa mtuhumiwa na wanachama wake kwani dola isinge tumia busara shari ingetokea.tukubaliane taifa ni letu sote tunawajibu kulilinda .
 
Kwaa nini chadema kisife? Yaani vurugu tuu uchochezi fitina kuamasiha maandamano na vita?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…