Mapema leo, mgombea wa ubunge Arusha mjini kwa ticket ya CCM alikua anarudisha fomu yake kwa msimamizi wa uchaguzi Arusha.
Pamoja nae ameandamana na mgombea wa viti maalum bi Catherine Magige.
Pamoja na wanachama na wafuasi wengi Sana wa chama Cha mapinduzi kujitokeza kumsindikiza mgombea wao, wananchi wengi Sana waliacha shughuli zao ili tu wamuone na wengine wengi wamejitokeza kumsindikiza ndugu Mrisho Mashaka Gambo kurudisha fomu ya uchaguzi.
Kwa niliyoyashuhudia kwa macho, ni wazi Sasa siasa za CHADEMA ndo zinafikia kikomo Arusha mjini. Wananchi wanasema walichoka na siasa za fujo, vurugu na maandamano.
Hata hivyo wananchi wanalalamika mbunge aliyemaliza muda wake Godbless Lema alikuwa hashiriki kwenye shughuli zinazowagusa wananchi, haswa wakipata shida. Mfano waliotoa wananchi ni wakati wa janga la Moto wa soko la samunge. Mbunge hakuonekana kabisa na Wala hakuwapa pole wajasiriamali wadogowadogo waliopatwa na janga kubwa Kama lile. Hakika ni Jambo la kushtua Sana haswa ukichukulia familia nyingi za watu wa Arusha lazma utakuta Wana ndugu, jamaa ama rafiki anafanya biashara eneo la samunge. Hakika Moto ule uligusa familia nyingi Arusha.
Katika maeneo ya kaloleni, wakazi wa Soweto wanasema kamwe hawatamsahau Lema na CHADEMA kwa jinsi walivyowadanganya wakati waliposababisha fujo na vurugu katika uwanja wa Soweto. Watoto wawili Sharifa na Fatuma Jumanne waliumia na wakapelekwa katika hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya matibabu. Mbunge aliyemaliza muda wake Lema pamoja na Mbowe na CHADEMA waliwashauri wazaz wawahamishie watoto katika hospitali ya selian, kwakuwa wao watalipa bill ya waganga wote.
Watoto wale walihamishiwa pale seliani huku CHADEMA waakijua kabisa sio kweli kwamba walikuwa wamelipia pale, matokeo yake wale watoto hawakupata huduma yeyote kwakuwa Ile ni hospitality malipo Hali iliyopelekea mmoja wa mtoto kukatwa mguu na mwingine kupata ulemavu. Chama Cha Mapinduzi baada ya kupata habari Ile haraka sana iliingilia Kati na kuwapeleka watoto wale Nairobi na kuhakikisha wanatibiwa mpaka wanapona.
Bila aibu Mbowe na Lema walikuwa wanahojiwa na vyombo vya habari na kuuhadaa Uma kwamba wagonjwa wapo Nairobi huku wakijua kabisa kwamba waliwadanganya wazaz na kuwapotosha (laiti wangewaacha watoto pale hospital ya mkoa ya Mount Meru, watoto wangepatiwa huduma mapema hivyo wasingepata ulemavu), lakini pia waliuhadaa Uma wa watanzania huku wakijua hawakutoa hata Senti tano kuwahudumia watoto wale na hata hawajui wako wapi na wanaendelea vipi kwa Sasa. Watoto hao wanaendelea na masomo yao huku CCM ikiwafatilia kwa ukaribu mkubwa Sana.
Haya niliyoandika hapa ni kwa uchache sana wa malalamiko ya wakazi wa mkoa wa Arusha na vitongoji vyake dhidi ya mbunge Lema na chama chake Cha CHADEMA.
Lakini pia Wana Mengi Sana wanayompongeza Mh. Raisi Magufuli na serikali ya awamu ya tano aliyoyafanya Arusha. Miradi mingi ya pesa nyingi imekuja Arusha. Maji, umeme barabara na pia kinaa mama naa vijana wamewezeshwa kufanya biashara, hivyo kuongeza ajira Arusha. Huduma za afya haswa ya mama, mtoto na wazee zimeboreshwa Sana pamoja na kwamba Jimbo lilikuwa lipo upinzani.
Baada ya kuona umati wa watu wengi namna hiyo waliojitokeza kusupport CCM na wagombea wake, HAKIKA NIMEAMINI SIASA ZA CHADEMA SASA ZIMEFIKIA UKINGONI NA SIASA ZA LEMA ZIMEFIKIA TAMATI ARUSHA MJINI.