GE2025 CCM Isipo chukua hatua mapema itaangamia muda sio mrefu

GE2025 CCM Isipo chukua hatua mapema itaangamia muda sio mrefu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Kiboko.

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2013
Posts
2,896
Reaction score
1,214
Habari za mchana wanabodi,

Nipende kutoa angalizo kwa chama tawala, kwa haya yanayoendelea kwenye chaguzi zao za kura ya maoni kupata wabunge, wawakilishi na madiwani.

RUSHWA imekuwa ndo kigezo cha mtia nia kupata kura za wajumbe. Mfano hai jimboni Ukerewe mkoa wa Mwanza, kuna mtia nia anaitwa Dkt Switbert Mkama aliewahi kuwa naibu katibu mkuu na mkurugenzi wa fedha na mipango, anatoa rushwa nje nje na hakuna hatua yoyote anachukuliwa.

Mkama amewanunua viongozi wa CCM wilaya kuanzia mwenyekiti, katibu mpka ngazi za chini kabsa, hii inamfanya afanye chochote anachotaka pasna kuchukuliwa hatua yoyote.

Jimbo la Ukerewe ni miongoni mwa majimbo machache ndani ya mkoa wa Mwanza ambayo ndani ya miaka 30 toka kuanzishwa chaguzi za vyama vingi limeshatoka Mbunge toka upinzani kwa vipindi viwili, yaan 2010 na 2015.

Nitoe rai kwa CCM, kutuma ujumbe maalumu kuhakiki zoezi zima la kura za maoni nchi nzima ili kujihakikishia kabla ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo baadae mwezi wa kumi.

Asante.
 
Nitoe rai kwa CCM, kutuma ujumbe maalumu kuhakiki zoezi zima la kura za maoni nchi nzima ili kujihakikishia kabla ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo baadae mwezi wa kumi.
Kwamba ngedere watumwe kwenda kudhibiti nyani kwa kosa la kula na kuharibu mahindi shambani??

Wote wapo hivyo bro, tulia..

 
Inajulikana hiyo, mchakato wote umejaa rushwa tupu. Kama usipomwaga mzigo kazi yako itakuwa ngumu sana, Hadi Sasa kama taifa tumeshafeli vibaya mno, Kwa jinsi tunavyokwenda Hali itazidi kuwa mbaya labda litokee gharika kama lile la Great Flood lizoe uchafu wote na hatimaye tuanze upya...
 
Habari za mchana wanabodi,

Nipende kutoa angalizo kwa chama tawala, kwa haya yanayoendelea kwenye chaguzi zao za kura ya maoni kupata wabunge, wawakilishi na madiwani.

RUSHWA imekuwa ndo kigezo cha mtia nia kupata kura za wajumbe. Mfano hai jimboni Ukerewe mkoa wa Mwanza, kuna mtia nia anaitwa Dkt Switbert Mkama aliewahi kuwa naibu katibu mkuu na mkurugenzi wa fedha na mipango, anatoa rushwa nje nje na hakuna hatua yoyote anachukuliwa.

Mkama amewanunua viongozi wa CCM wilaya kuanzia mwenyekiti, katibu mpka ngazi za chini kabsa, hii inamfanya afanye chochote anachotaka pasna kuchukuliwa hatua yoyote.

Jimbo la Ukerewe ni miongoni mwa majimbo machache ndani ya mkoa wa Mwanza ambayo ndani ya miaka 30 toka kuanzishwa chaguzi za vyama vingi limeshatoka Mbunge toka upinzani kwa vipindi viwili, yaan 2010 na 2015.

Nitoe rai kwa CCM, kutuma ujumbe maalumu kuhakiki zoezi zima la kura za maoni nchi nzima ili kujihakikishia kabla ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo baadae mwezi wa kumi.

Asante.
Ife mara ngapi labda useme ifufuke
 
We msaliti pambana tu na hali yako, wakati unasaliti upinzani kwa kuunga mkono juhudi za CCM kupitia Magufuli hukuyajua hayo? Tumia mafao yako ya ubunge sasa uhonge kama wenzako.
 
We msaliti pambana tu na hali yako, wakati unasaliti upinzani kwa kuunga mkono juhudi za CCM kupitia Magufuli hukuyajua hayo? Tumia mafao yako ya ubunge sasa uhonge kama wenzako.
Jenga hoja ndugu.
 
Back
Top Bottom