Nikukumbushe
JF-Expert Member
- Jun 4, 2013
- 2,602
- 408
Ama kweli kila lililo na mwanzo halikosi kuwa na mwisho. Kitendo cha aibu alichofanyiwa Jaji Joseph Warioba ni kundi lingine linaloibuka ndani ya CCM,ni kundi la wazalendo wa kweli,ni kundi la watu wenye busara,ni kundi la watu waliofanya kazi karibu sana na mwalimu Nyerere.
Nakumbuka siku ya mdahalo,Warioba alisema,kuna watu wanatumia vibaya jina la mwalimu katika kufanikisha maslahi yao. Ni mwalimu huyu huyu tuliyefanya naye kazi au ni mwalimu mwingine?
Alihoji Warioba.
Warioba alisema,mwalimu amekufa akiliamini na kulitetea azimio la Arusha. Je,mwalimu angekuwepo angeruhusu watu kuwa na akaunti nje ya nchi,mwalimu angekuwepo angepinga uwepo wa maadili ya viongozi kwenye katiba,alihoji Warioba. Au mnamzungumzia mwalimu mwingine sio huyu ninaye mfahamu na kufanya naye kazi.
Kauli ya Sitta.
Sitta yeye anasema,Warioba alijitakia. Kwa tafsiri yake ni kwamba kilichomtokea Warioba kilistahili. Sitta anasahau kuwa yanayotokea hapa kiini kikubwa ni yeye. Kauli ya Sitta ni ya kulaaniwa na mtu yeyote aliye na utu na anajali utu wa wengine.
Kauli ya W. Malechela.
Yeye anasema,iweje mtu yuko CCM aendelee kupinga serikali? Iweje aendelee kupinga wakati anapata mafao yake kwa mgongo wa CCM? Alihoji.Ninachokijua mafao ayapatayo Warioba ni haki yake kikatiba na sio suala la U-CCM.Nauliza swali,je iwapo Warioba atarudisha kadi ya CCM mafao yake yatasitishwa au ataendelea kupewa?
Bali na kundi la Warioba,kuna kundi la mbabe Sitta,Lowassa,Membe nk.
CCM lazima ife,na hii ni dalili za kuanguka kwa CCM. Kipimo ni katika chaguzi zijazo. CCM haiwezi kuwadharau,kuwapiga,kuwatukana,kuwakejeli wazee wenye heshima na busara ikabaki salama,hakuna.
Nakumbuka siku ya mdahalo,Warioba alisema,kuna watu wanatumia vibaya jina la mwalimu katika kufanikisha maslahi yao. Ni mwalimu huyu huyu tuliyefanya naye kazi au ni mwalimu mwingine?
Alihoji Warioba.
Warioba alisema,mwalimu amekufa akiliamini na kulitetea azimio la Arusha. Je,mwalimu angekuwepo angeruhusu watu kuwa na akaunti nje ya nchi,mwalimu angekuwepo angepinga uwepo wa maadili ya viongozi kwenye katiba,alihoji Warioba. Au mnamzungumzia mwalimu mwingine sio huyu ninaye mfahamu na kufanya naye kazi.
Kauli ya Sitta.
Sitta yeye anasema,Warioba alijitakia. Kwa tafsiri yake ni kwamba kilichomtokea Warioba kilistahili. Sitta anasahau kuwa yanayotokea hapa kiini kikubwa ni yeye. Kauli ya Sitta ni ya kulaaniwa na mtu yeyote aliye na utu na anajali utu wa wengine.
Kauli ya W. Malechela.
Yeye anasema,iweje mtu yuko CCM aendelee kupinga serikali? Iweje aendelee kupinga wakati anapata mafao yake kwa mgongo wa CCM? Alihoji.Ninachokijua mafao ayapatayo Warioba ni haki yake kikatiba na sio suala la U-CCM.Nauliza swali,je iwapo Warioba atarudisha kadi ya CCM mafao yake yatasitishwa au ataendelea kupewa?
Bali na kundi la Warioba,kuna kundi la mbabe Sitta,Lowassa,Membe nk.
CCM lazima ife,na hii ni dalili za kuanguka kwa CCM. Kipimo ni katika chaguzi zijazo. CCM haiwezi kuwadharau,kuwapiga,kuwatukana,kuwakejeli wazee wenye heshima na busara ikabaki salama,hakuna.