Salamu zangu za mwisho wa mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 kwa CCM ni kuhusu nafasi ya naibu katibu mkuu wake Mwigulu Chemba. CCM inahitaji kumtafuta mtu makini mwenye uwezo wa kujenga chama na kufahamu taifa linataka nini kuelekea mwaka 2015. Rafiki yangu Mwigulu ni Janga Ndani ya CCM na mstakabli wa chama chake na amani ya taifa letu. Nasema hivi kwa sababu zifuatazo.
1. Hajui nini taifa linataka kuelekea mageuzi ya kidemokrasia na hana uvumilivu wa mawazo ya watu wengine. Hili linadhihirishwa na matamko yake ya kutishia watumishi wa umma kuwa wale wenye mlengo wa vyama vya upinzani watashughulikiwa. Hili tamko litawafanya watawala waovu kuwanyanyasa watumishi wa umma kwa misingi ya vyama vyao na itasabibisha maafisa utumishi, wakuu wa wilaya, RC n.k kutumia mwanya huo kuwaonea watumishi wenye mawazo tofauti kwa uhai wa taifa. Wakuu wa idara za serikali ambao si waaminifu au wanaofanya ufisadi kama mabwana ardhi katika halmashauri zetu watatumia mwanya huo kujipendekeza kwa CCM, ili wale watakaotoa siri zao za ufisadi waonekane ni wapinzani.
2. Mwigulu anapaswa kufahamu kuwa CCM ndiyo yenye watumishi wa umma ambao wanafanya siasa wakati bado ni watumishi wa serikali. CCM nchi hii ina madiwani ambao ni waalimu wa shule za sekondari na bado wanafundisha na kufanya siasa. Mwigulu anza nao hao wapo halmashauri ya wilaya ya Babati vijini na mjini.
3. Mwigulu pamoja na kwamba amepitia shule hadi kuwa na shahada ya pili ya uchumi, uwezo wake wa kujenga hoja ni mdogo ndiyo maana kwenye mikutano yake anahubiri matusi badala ya sera. Sina maana kwamba Upinzania hakuna watu wabovo kama aina ya Mwigulu, hapana, wapo ila hawajafikia cheo kama cha Mwigulu. Uwezo na busara huwa ni vya kuzaliwa, shule huwa inaongezea kidogo, hivyo hataweza kuhimili vishindo vya siasa shindani. Yeye ameaanza kuhangika na personalities za watu badala ya kujenga hoja kwanini tuna umaskini na kwanini mama zetu hawana maji. Nasema hivi si kwa kumchukia Mwigulu ni kwa kumsaidia na kukisaidia chama chake na Taifa maana atasabibisha vurugu ambazo hazina maana kwa mstakabali wa taifa letu. Mwigulu mimi namfahamu, tumefanya naye siasa ya DARUSO UDSM, bwana mdogo unapya! Tatizo lake pia amelewa vyeo!
Mimi nimeamua kuyasema haya kwa sababu ninafahamu jinsi wakuu wa idara, DC, RC wanavyojua kuonea watu kwa misingi ya kuwaonea watumishi wenye mrengo wa maono kipinzani. Mimi 2000 niliandikiwa barua ya kuitwa kwa mkuu wa wilaya eti ninasadia upinzani kampeni, na kwanini nisifukuzwe utumishi. Nilimwuliza DC wewe umejuaje? Mbona nawe ni mtumishi wa umma na bado unasaidia chama chako? Nilipewa onyo na DC ambaye si mkuu wangu wa idara.
Tanzania leo hii imebadilika sana inahitaji watu wenye maono mapana ili kujenga amani.
CCM tafuteni Naibu katibu mkuu makini.
Nawatakia heri ya mwaka mpya.
1. Hajui nini taifa linataka kuelekea mageuzi ya kidemokrasia na hana uvumilivu wa mawazo ya watu wengine. Hili linadhihirishwa na matamko yake ya kutishia watumishi wa umma kuwa wale wenye mlengo wa vyama vya upinzani watashughulikiwa. Hili tamko litawafanya watawala waovu kuwanyanyasa watumishi wa umma kwa misingi ya vyama vyao na itasabibisha maafisa utumishi, wakuu wa wilaya, RC n.k kutumia mwanya huo kuwaonea watumishi wenye mawazo tofauti kwa uhai wa taifa. Wakuu wa idara za serikali ambao si waaminifu au wanaofanya ufisadi kama mabwana ardhi katika halmashauri zetu watatumia mwanya huo kujipendekeza kwa CCM, ili wale watakaotoa siri zao za ufisadi waonekane ni wapinzani.
2. Mwigulu anapaswa kufahamu kuwa CCM ndiyo yenye watumishi wa umma ambao wanafanya siasa wakati bado ni watumishi wa serikali. CCM nchi hii ina madiwani ambao ni waalimu wa shule za sekondari na bado wanafundisha na kufanya siasa. Mwigulu anza nao hao wapo halmashauri ya wilaya ya Babati vijini na mjini.
3. Mwigulu pamoja na kwamba amepitia shule hadi kuwa na shahada ya pili ya uchumi, uwezo wake wa kujenga hoja ni mdogo ndiyo maana kwenye mikutano yake anahubiri matusi badala ya sera. Sina maana kwamba Upinzania hakuna watu wabovo kama aina ya Mwigulu, hapana, wapo ila hawajafikia cheo kama cha Mwigulu. Uwezo na busara huwa ni vya kuzaliwa, shule huwa inaongezea kidogo, hivyo hataweza kuhimili vishindo vya siasa shindani. Yeye ameaanza kuhangika na personalities za watu badala ya kujenga hoja kwanini tuna umaskini na kwanini mama zetu hawana maji. Nasema hivi si kwa kumchukia Mwigulu ni kwa kumsaidia na kukisaidia chama chake na Taifa maana atasabibisha vurugu ambazo hazina maana kwa mstakabali wa taifa letu. Mwigulu mimi namfahamu, tumefanya naye siasa ya DARUSO UDSM, bwana mdogo unapya! Tatizo lake pia amelewa vyeo!
Mimi nimeamua kuyasema haya kwa sababu ninafahamu jinsi wakuu wa idara, DC, RC wanavyojua kuonea watu kwa misingi ya kuwaonea watumishi wenye mrengo wa maono kipinzani. Mimi 2000 niliandikiwa barua ya kuitwa kwa mkuu wa wilaya eti ninasadia upinzani kampeni, na kwanini nisifukuzwe utumishi. Nilimwuliza DC wewe umejuaje? Mbona nawe ni mtumishi wa umma na bado unasaidia chama chako? Nilipewa onyo na DC ambaye si mkuu wangu wa idara.
Tanzania leo hii imebadilika sana inahitaji watu wenye maono mapana ili kujenga amani.
CCM tafuteni Naibu katibu mkuu makini.
Nawatakia heri ya mwaka mpya.