Malisa Godlisten
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 202
- 1,588
Tanzania ina ukubwa wa eneo la ardhi (total land area) mita za mraba milioni 364,915. Kenya ina ukubwa wa mita za mraba milioni 224,962, Uganda mita za mraba milioni 91,136, Rwanda mita za mraba milioni 10,169 na Burundi mita za mraba 10,745.
Tanzania peke yake ni kubwa kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Nchi za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi zikijikusanya kwa pamoja zinakuwa na jumla ya eneo la mita za mraba milioni 337,012. Wakati Tanzania peke yake ina mita za mraba milioni 364,915.
Kwa hiyo ukiigawa Tanzania utapata nchi 4 zenye ukubwa sawa na Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi na litabaki eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba milioni 27,903 ambalo linaweza kutengeneza nchi nyingine yenye ukubwa sawa na Togo.
Hii maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Tanzania ni sawa na nchi tano. Yani Tanzania ni nchi moja yenye nchi tano ndani yake.
Hivyo basi Rais anayeweza kuongoza taifa hili na kuleta maendeleo lazima awe Rais mmoja lakini mwenye akili za Marais watano. Yani awazidi akili mara tano akina Kenyatta, Museveni, Nkurunzinza na Kagame.
Marais wote wa Afrika Mashariki wanapaswa wakija Tanzania wajione ni kama wakuu wa mikoa. Na ili wajione hivyo lazima kuwe na hatua kubwa za kimaendeleo kuliko kwao.
Yani Kagame akija hapa akikuta treni za umeme (kwake hana), akikuta Hospitali za kisasa watu wanatoka Asia kuja kutibiwa hapa (kwake hakuna), akikuta Barabara za juu ktk miji mikubwa (fly overs), akikuta maslahi mazuri kwa watumishi, akikuta umeme wa uhakika na tunalipa TZS 3000 kwa mwezi, akikuta elimu ni bure kuanzia Shule ya msingi hadi chuo kikuu, lazima ajione Mkuu wa mkoa.
Lakini kama Kagame kwake ana fly overs (sisi hatuna), wanafunzi wa Rwanda wana loptop kuanzia shule ya msingi (sisi hatuna), Elimu ya sekondari bure (sisi tumeshindwa), halafu akituangalia tuna Bandari, madini, gesi, mlima K.njaro, Mbuga za wanyama etc lazima amuone Rais wetu kama "Diwani".
Jiulize Tanzania yenye rasilimali lukuki ndiyo inayoongoza kwa kukata kodi kubwa (PAYE) kwa watumishi wake kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Serikali kila mwisho wa mwezi inajikusanyia 18% ya mishahara ya watumishi kana kwamba haina chanzo kingine cha mapato zaidi ya kunyonya watumishi.
Rwanda isiyo na rasilimali nyingi kama sisi, watumishi wanalipa 6% kama kodi kwenye mishahara yao.
Yani mtumishi anayelipwa TZS 700,000/= nchini Tanzania anakatwa TZS 108,000/= kama kodi. Wakati mtumishi anayelipwa mshahara kama huo nchini Rwanda anakatwa TZS 36,000/= tu kama kodi.
Rwanda ambayo haina gesi, haina bandari, haina madini inawajali watumishi wake. Tanzania yenye gesi, mlima, madini, bandari haitaki kutoza kodi huko kote badala yake inamnyonya mtumishi kama vile serikali haina chanzo kingine cha mapato zaidi kodi za watumishi.
Hivi "logic" ya kumtoza mtumishi 18% ya kodi ni ipi wakati kuna vyanzo vingi sana vya mapato nchini? Unatoa msamaha wa kodi kwa wawekezaji wa madini, na wachimbaji wa gesi, halafu unakazana kumnyonya mtumishi. Hii ni kukosa akili.
Mwaka huu Tanzania imepoteza jumla ya TZS 4.7 Trilioni kutokana na misamaha ya kodi. Yani karibu robo ya bajeti. Makadirio ya gharama za kusomesha watoto wetu kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu kwa mwaka ni TZS 1.6 Trilioni (kwa mujibu wa Mbatia).
Maana yake ni kwamba tukipunguza misamaha ya kodi kwa mwaka mmoja tu, tunapata hela za kutosha kusomesha wanafunzi wote wa shule za msingi hadi chuo kikuu kwa miaka miwili. Lakini serikali ya CCM haiwezi kuliona hili kwa sababu ya akili ndogo.
Mtumishi yoyote anayeiunga mkono CCM yafaa akapimwe akili. Imagine wewe ni mwalimu unalipwa 700,000/=. Kodi tu ni 108,000/=, Pensheni 70,000/= (10%), UWT 21,000/= (03%), mwisho wa siku unapokea 498,000/=. Serikali ya CCM inakunyonya bila huruma na wewe unakenua meno kusema "ccm mbele kwa mbele".
Bado hujalipa kodi ya pango, ulipe maji, umeme, ada ya wanao shule, nauli, chakula, mavazi, etc. Hivi kwanini usiwe maskini?? Kwanini usikope kabla ya tar.05?? Hivi unadhani waalimu wanapenda kuwa na "vidaftari" vya mkopo kwenye maduka ya kina mangi? Serikali ya CCM ndio inawalazimisha kudhalilika.
Sasa mwaka huu iwe mwisho. Uwezo wa kufanya mabadiliko uko mikononi mwako. Mchague Lowassa kuwa Rais wako uone mabadiliko. CCM imetutesa miaka 50 sasa yatosha. Let them rest in peace.
Magufuli hana uwezo wowote wa kufanya mabadiliko yoyote ndani ya CCM. Haiwezekani CCM hii iliyowatesa watanzania zaidi ya miaka 50 leo ilete neema kwa sababu ya Magufuli.
Hakuna "theory" yoyote ya kisayansi duniani inayoweza kudhibitisha kuwa Gari bovu lililoshindwa kutembea kwa miaka 50, linaweza kukimbia speed 120 likipata dereva mpya.
SAY NO TO CCM. Tunataka Rais mwenye akili za marais watano, ili marais wengine wa Afrika Mashariki wakimuona wamuogope na wamheshimu kwa kasi ya maendeleo atakayotuletea. Na Rais huyo ni Edward Ngoyai Lowassa peke yake. CCM Imechoka, tuitoe.!
Tanzania peke yake ni kubwa kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Nchi za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi zikijikusanya kwa pamoja zinakuwa na jumla ya eneo la mita za mraba milioni 337,012. Wakati Tanzania peke yake ina mita za mraba milioni 364,915.
Kwa hiyo ukiigawa Tanzania utapata nchi 4 zenye ukubwa sawa na Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi na litabaki eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba milioni 27,903 ambalo linaweza kutengeneza nchi nyingine yenye ukubwa sawa na Togo.
Hii maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Tanzania ni sawa na nchi tano. Yani Tanzania ni nchi moja yenye nchi tano ndani yake.
Hivyo basi Rais anayeweza kuongoza taifa hili na kuleta maendeleo lazima awe Rais mmoja lakini mwenye akili za Marais watano. Yani awazidi akili mara tano akina Kenyatta, Museveni, Nkurunzinza na Kagame.
Marais wote wa Afrika Mashariki wanapaswa wakija Tanzania wajione ni kama wakuu wa mikoa. Na ili wajione hivyo lazima kuwe na hatua kubwa za kimaendeleo kuliko kwao.
Yani Kagame akija hapa akikuta treni za umeme (kwake hana), akikuta Hospitali za kisasa watu wanatoka Asia kuja kutibiwa hapa (kwake hakuna), akikuta Barabara za juu ktk miji mikubwa (fly overs), akikuta maslahi mazuri kwa watumishi, akikuta umeme wa uhakika na tunalipa TZS 3000 kwa mwezi, akikuta elimu ni bure kuanzia Shule ya msingi hadi chuo kikuu, lazima ajione Mkuu wa mkoa.
Lakini kama Kagame kwake ana fly overs (sisi hatuna), wanafunzi wa Rwanda wana loptop kuanzia shule ya msingi (sisi hatuna), Elimu ya sekondari bure (sisi tumeshindwa), halafu akituangalia tuna Bandari, madini, gesi, mlima K.njaro, Mbuga za wanyama etc lazima amuone Rais wetu kama "Diwani".
Jiulize Tanzania yenye rasilimali lukuki ndiyo inayoongoza kwa kukata kodi kubwa (PAYE) kwa watumishi wake kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Serikali kila mwisho wa mwezi inajikusanyia 18% ya mishahara ya watumishi kana kwamba haina chanzo kingine cha mapato zaidi ya kunyonya watumishi.
Rwanda isiyo na rasilimali nyingi kama sisi, watumishi wanalipa 6% kama kodi kwenye mishahara yao.
Yani mtumishi anayelipwa TZS 700,000/= nchini Tanzania anakatwa TZS 108,000/= kama kodi. Wakati mtumishi anayelipwa mshahara kama huo nchini Rwanda anakatwa TZS 36,000/= tu kama kodi.
Rwanda ambayo haina gesi, haina bandari, haina madini inawajali watumishi wake. Tanzania yenye gesi, mlima, madini, bandari haitaki kutoza kodi huko kote badala yake inamnyonya mtumishi kama vile serikali haina chanzo kingine cha mapato zaidi kodi za watumishi.
Hivi "logic" ya kumtoza mtumishi 18% ya kodi ni ipi wakati kuna vyanzo vingi sana vya mapato nchini? Unatoa msamaha wa kodi kwa wawekezaji wa madini, na wachimbaji wa gesi, halafu unakazana kumnyonya mtumishi. Hii ni kukosa akili.
Mwaka huu Tanzania imepoteza jumla ya TZS 4.7 Trilioni kutokana na misamaha ya kodi. Yani karibu robo ya bajeti. Makadirio ya gharama za kusomesha watoto wetu kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu kwa mwaka ni TZS 1.6 Trilioni (kwa mujibu wa Mbatia).
Maana yake ni kwamba tukipunguza misamaha ya kodi kwa mwaka mmoja tu, tunapata hela za kutosha kusomesha wanafunzi wote wa shule za msingi hadi chuo kikuu kwa miaka miwili. Lakini serikali ya CCM haiwezi kuliona hili kwa sababu ya akili ndogo.
Mtumishi yoyote anayeiunga mkono CCM yafaa akapimwe akili. Imagine wewe ni mwalimu unalipwa 700,000/=. Kodi tu ni 108,000/=, Pensheni 70,000/= (10%), UWT 21,000/= (03%), mwisho wa siku unapokea 498,000/=. Serikali ya CCM inakunyonya bila huruma na wewe unakenua meno kusema "ccm mbele kwa mbele".
Bado hujalipa kodi ya pango, ulipe maji, umeme, ada ya wanao shule, nauli, chakula, mavazi, etc. Hivi kwanini usiwe maskini?? Kwanini usikope kabla ya tar.05?? Hivi unadhani waalimu wanapenda kuwa na "vidaftari" vya mkopo kwenye maduka ya kina mangi? Serikali ya CCM ndio inawalazimisha kudhalilika.
Sasa mwaka huu iwe mwisho. Uwezo wa kufanya mabadiliko uko mikononi mwako. Mchague Lowassa kuwa Rais wako uone mabadiliko. CCM imetutesa miaka 50 sasa yatosha. Let them rest in peace.
Magufuli hana uwezo wowote wa kufanya mabadiliko yoyote ndani ya CCM. Haiwezekani CCM hii iliyowatesa watanzania zaidi ya miaka 50 leo ilete neema kwa sababu ya Magufuli.
Hakuna "theory" yoyote ya kisayansi duniani inayoweza kudhibitisha kuwa Gari bovu lililoshindwa kutembea kwa miaka 50, linaweza kukimbia speed 120 likipata dereva mpya.
SAY NO TO CCM. Tunataka Rais mwenye akili za marais watano, ili marais wengine wa Afrika Mashariki wakimuona wamuogope na wamheshimu kwa kasi ya maendeleo atakayotuletea. Na Rais huyo ni Edward Ngoyai Lowassa peke yake. CCM Imechoka, tuitoe.!