CCM Arumeru kimenuka

CCM Arumeru kimenuka

kibogo

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
9,739
Reaction score
4,745
Nimeshuhudia katika Taarifa ya Habari ITV ni katika kikao cha Balaza la madiwani. Madiwani wa CCM akiwemo mwenyekiti wa Halmashauri wamesema Iwapo serikali haitachukua hatua juu ya mgogolo wa Ardhi uliopo huko baina ya wananchi na wawekezaji basi wao wote watarudisha kadi za CCM na kujivua uanachama na hawataishia hapo pia watawashawishi wanachama wote wa CCM katika kata zao kurudisha kadi za CCM. Na ili kuweka msisitizo wameunda tume ya madiwani kadhaa ambao wataenda kuonana na Rais na yasipotolewa majibu sahihi wanachukua huo uamuzi mgumu.
 
Wacha kinuke, ccm wanawaona raia wa nchi hii kama viatu....

go to hell ccm!
 
Nimeshuhudia katika Taarifa ya Habari ITV ni katika kikao cha Balaza la madiwani. Madiwani wa CCM akiwemo mwenyekiti wa Halmashauri wamesema Iwapo serikali haitachukua hatua juu ya mgogolo wa Ardhi uliopo huko baina ya wananchi na wawekezaji basi wao wote watarudisha kadi za CCM na kujivua uanachama na hawataishia hapo pia watawashawishi wanachama wote wa CCM katika kata zao kurudisha kadi za CCM. Na ili kuweka msisitizo wameunda tume ya madiwani kadhaa ambao wataenda kuonana na Rais na yasipotolewa majibu sahihi wanachukua huo uamuzi mgumu.

hawana ubavu wa kuhama hao,kwan leo ndo wanajua kuwa serikal ya ccm ndo waanzilishi wa migogoro ya ardhi? Kama viwanja na mashamba makubwa yameuzwa ama kupewa viongoz wakubwa,wao atahoji nn???? Wahame sasa hv tuwaone wachoka
 
Suala la ardhi hapa arumeru ni tatizo linalohitaji ufumbuzi wa haraka sana, wageni wanamiliki maeneo makubwa sana, mtu mmoja anamiliki hadi ekari mia tano halafu eneo halitumiki kwa shughuli yoyote, kuna haja ya haya maeneo yanayomilikiwa na hawa watu tunaowaita wawekezaji lakini hawayatumii kugawiwa kwa wananchi
 
watasikilizwa na serikali yao sikivu...
 
Hzo kadi ndo zmeshikilia hyo ardhi? Ardhi imelaaniwa' wafanye mambo mengine, hyo ardhi wamwachie anayeing'ang'ania waone kama akifa ataibeba aende nayo'
 
Ni vizuri, maana inatakiwa wafanye kazi kama viongozi waliochaguliwa na wananchi na siyo kufanya kazi kwa mamlaka ya nchama kinavyotaka.
 
Go to hell ccm! Chama cha mashamba.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Hii ni njaa tu mashamba wanatodai ni ngumu kupewa mfano dolly estate ile imejengwa na mabilionea mapaka wengine wamefuga nembo ya taifa garden kwao
 
Hii ni njaa tu mashamba wanatodai ni ngumu kupewa mfano dolly estate ile imejengwa na mabilionea mapaka wengine wamefuga nembo ya taifa garden kwao
Kwa hiyo kama wakigoma kutekelezewa hicho wanachokihitaji ndio wamesema watarudisha Kadi za CCM wao na wananchi wanaowaongoza ambao ni wanachama wa CCM, swali la msingi je CCM itakuwa tayari kupoteza Wanachama kwa ajili ya kuwalinda hawa Vibaraka?
 
Back
Top Bottom