Business opportunity

Sijakuelewa hapo kujiunga na nyinyi ni bure. BURE kivipi? Hata forever living ni bure lakini ni lazima ununue products ili uwe member. Unaweza kujiunga bure halafu iweje?unakaa bila kununua products? GNLD najua ndiyo huwa kuna joining fee na fee ya ku renew kila mwaka. Ndugu yangu katika kusaka mafanikio hakuna kitu kirahisi ama sivyo kila mtu angekuwa tajiri hapa duniani. Lakini matajiri ni kiduchu tu na itaendelea kuwa hivyo mpaka mwisho wa nyakati.
Mimi nadhani labda ulikuwa na upline mbaya wakati upo FLP au wewe ni mtu wa kukata tamaa mapema kabla hujajifunza kila kitu na labda vilevile unataka kupata mafanikio kirahisirahisi.
Mbona ma upline wengi wanatoa masaada mkubwa sana kwa downlines...kwenye biashara ya network marketing bila ya kumsaidia na kumpa ujanja downline wako wewe utafanikiwa vipi?

Top distributor wa flp africa(John Ekperigin) nilikwenda kumuona mwenyewe JB belmont hotel alipokuja na jamaa alieleza vitu vizuri tu. Nataka unijibu hili swali. Hivi kwenye network marketing unaweza kufanikiwa vipi bila kuwa coach downlines wako wa copy kile unachokifanya wewe?
Hii siyo biashara ya chapati ya kufichana siri ya viungo. Hii ni biashara ya kushikana mkono, kuleana, kusaidiana mpaka hapo downline wako atakapoweza kusimama mwenyewe na yeye kuanza kuduplicate tricks and techniques zako kwa downlines wake. Duplication of Efforts.
Mimi nadhani unahitaji kutulia hata kwenye hiyo kampuni yako. Nadhani kinacho count sanavkwenye hii biashara sidhani ni ubora wa bidhaa au marketing plan. Kinachocount sana ni wewe mwenyewe ni mtu wa aina gani. kama ni mtu wa kukimbiakimbia utashindwa tu hata kwenye hiyo kampuni yako mpya. Maana watu wanaofanikiwa kwenye haya makampuni ni wale wanaonaamua kweli kujifunza na kufanya hii biashara kwa jinsi inavyotakiwa.
 
Kama upline wako alikuficha kitu ili afanikiwe yeye tu basi hiyo siyo MLM. Ni biashara ya maandazi. Msingi mkuu wa kufanikiw ktk MLM ni kuwaonyesha downlines wako kila kitu kinachokufanya wewe ufanikiwe. Usipowaonyesha unavyofanikiwa je wewe utafanikiwaje?
soma article hapo chini
 

Hahaha acha ucheshi wewe.....ndio mnavyodanganyana millenium towers na jb belmont hivyo ?? For your info kuna lots of secrets hata mwenye kampuni mwenyewe Rex Maughan anajua katika mfumo wa ulipaji (we call it breakage of bonuses)....najua fika huwezi fanikiwa kwenye network marketing bila ku coach downlines wako...but kwenye upande wa qualifications ya zile safari na vyeo vyenu kuna namna mnaibiwa kwa muda mrefu tu...(It's like kwenye ile kazi mnayo fanya kuna kiasi kingi cha fedha kinakatwa na kampuni kinyemela ndio hiyo mnalipiwa hizo safari ambayo bado ni ndogo sana ukilinganisha na faida mlioitengenezea kampuni) nyie mnafanya tu bila kujua tu. Uchunguzi hamfanyi kwenye marketing plan mnapelekwa tu....Hebu nikuulize, Ni kwanini msipofikisha 4CC za kila mwezi bonus zenu wanapewa watu wa juu yenu ? (Huo ni wizi mkubwa, kwetu sisi hamna hiyo unachotakiwa kufanya ni kua active kwa ule mwezi tena kwa pesa ndogo sana ili upewe bonus yako)

Kwanini katika ku qualify vyeo kama supervisor, asst. manager, manager, senior, soaring etc katika kile kipindi cha miezi miwili ya ku qualify usipofikisha kile kiwango...wanafuta zile point/case credit za mwezi wa nyuma (mwanzo) na mwezi ujao unaanza upya ?? Zile point na zile pesa zinaenda wapi ?? kama sio wizi na unyanyasaji ni nini ?? (Kwetu sisi hatuna hiyo, usipofikisha kiwango cha ku qualify vyeo...point zako milele yote hazifutwi...unachotakiwa kufanya ni kuzimalizia kwa muda wowote zinabaki vile vile na hela yako unatunziwa na kupewa haraka utakapo maliza point zako)....Kuhusu kujenga timu....unatakiwa kutafuta watu wawili tu wanawekwa kulia na kushoto kwako....kama utaongeza wengine wanashushwa na system chini ya wale wawili hivyo hivyo kwa kila mtu......(Note: Ukiingiza wengi yan zaidi ya wawili watakua your personal sponsored distributors ambao watakuingizia pesa zaidi)....kila mmoja anatakiwa kujenga team mbili tu upto infinity level (bila ya kikomo). Na yale mauzo yatahesabiwa kwa watu wote kwenye team yako....unachotakiwa ni ku activate tu tena kwa pesa ndogo upewe bonus yako. Ukiingiza watu wengi zaidi wewe binafsi bonus inaongezeka zaidi ingawa kila mtu anafaidika kwenye team yako...(Thats TRUE LEVERAGE (nguvu na msaada wa wenzio)) cio kama kampuni zingine hupewi hata sumni. Nafahamu hakuna kazi rahisi...issue ni kwamba mfumo wetu uko fair, malipo na mazingira yake ni mazuri. Tunafanya kazi iliyo fair (yenye haki) na rahisi kuelewa kisha tunalipwa kila wiki na kwa mwezi pia (yani malipo hutolewa mapema )...Ukilinganisha na nyie kazi ni ngumu zaidi, hakuna ki inua mgongo, point na pesa hupotea kinyemela, malipo ni kidogo alaf huchelewa !! Unaonaje hiyo ??

Marketing plan yetu ni simple and friendly unaweza jiunga kwa muda mfupi na ukapata pesa nzuri tu mwanzoni kama ya kukutia hamasa na motisha uzidi fanya kazi kwa nguvu zaidi. Ki ukweli Kampuni zingine zote Tanzania na duniani sijawahi ona wakifanya kitu kama hicho. kwanza tokea flp imeanza kufanya biashara mwaka 1978 hakuna mtu binafsi aliyewahi pewa check (bonus) ya Dollar million 8.5 sawa na Billion 13 za kitanzania approximately kwa kazi aliyoifanya na sio kwa mtu mmoja wengi tu wengine wana miaka 2 au 3 kwenye biashara (Ni juhudi zako tu) !! ..Check (bonus) ya juu ninayoifamu mimi ya Forever Living ni ile ya Dollar laki 9.5 na ushenzi sawa Billion 1.5 approximately ya yule mjerumani Rolf Kipp unaweza linganisha mwenyewe. Mimi nilikua manager forever living products nikajitoa mwaka huu...mpaka nafanya hivyo mimi sio mjinga...kila kitu nakijua humo, hapafai basi tu. Ila siku shawishi uache wewe endelea nao kwa hiari yako. Mimi nasema lililo la kweli tu.

Biashara Njema !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…